Sekta binafsi yalia wageni kuchukua fursa zao kibiashara

Sekta binafsi yalia wageni kuchukua fursa zao kibiashara

Sekta binafsi yalia wageni kuchukua fursa zao kibiashara

Dar es Salaam. Wasiwasi unaendelea kuongezeka kuhusu wafanyabiashara wa kigeni kuingilia biashara za wazawa, huku Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) likitaka hatua za haraka kulinda biashara za Watanzania.

Akizungumza katika tuzo za Wanawake Wajasiriamali wa Sekta ya Viwanda na Biashara Jumatano jioni, Rais wa TPSF, Angelina Ngalula, alisema raia wa Kichina, ambao awali huingia sokoni kama wawekezaji, wanazidi kujihusisha na biashara zinazopaswa kufanywa na wafanyabiashara wa ndani.

Tuzo za Wanawake Wajasiriamali wa Sekta ya Viwanda na Biashara ziliandaliwa na Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC).

Ngalula alisisitiza kuwa hali hiyo inatishia uhai wa wajasiriamali wa Kitanzania na kuhujumu uhuru wa kiuchumi wa taifa.

“Hakuna namna China inaweza kushindana na Tanzania, wala mfanyabiashara wa Kichina hawezi kushindana na mfanyabiashara wa Kitanzania katika biashara hizi zetu. China ni nchi yenye uchumi mkubwa; hawawezi kulinganishwa nasi.

“Inawezekanaje mfanyabiashara wa Kichina aje kushindana kibiashara na mfanyabiashara wa Kitanzania?” alihoji Ngalula.

Aliitaka Serikali kuwa na kanuni kali ili kuzuia wawekezaji wa kigeni kuendesha biashara katika sekta zilizotengwa kwa ajili ya wenyeji.

Februari 2025, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Selemani Jafo, aliteua kamati maalumu yenye wajumbe 15 kuchunguza uwepo wa wafanyabiashara wa kigeni wanaojihusisha na biashara ndogo ndogo zisizo rasmi, maarufu “Umachinga,” katika Soko la Kariakoo na maeneo mengine nchini.

Uamuzi huo ulitokana na ahadi ya Rais Samia Suluhu Hassan ikiwa ni moja ya hatua za kutatua malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara wa ndani, hususan wa Kariakoo, kuhusu ongezeko la wageni wanaofanya biashara katika sekta isiyo rasmi.

Dk Jafo alieleza kuwa, badala ya kuwekeza kwenye miradi mikubwa, baadhi ya wageni wanajihusisha na biashara ndogo zisizo rasmi, jambo linaloathiri biashara za wenyeji.

Kamati hiyo ilipomaliza kazi kwa siku zilizopangwa, ilibaini wafanyabiashara wengi wa kigeni wanafanya biashara zinazofanywa na wazawa, huku wakiuza bidhaa kwa bei ya chini, jambo linaloondoa ushindani sokoni.

Kamati hii pia ilibaini wageni kutumia vitambulisho vya uraia vya Watanzania kusajili biashara zao. Pia, katika maduka 75, walikutwa raia wa kigeni 152 waliajiriwa, huku asilimia 97 kati yao wakijihusisha na biashara za rejareja, 28 wakiishi nchini kinyume na sheria, na 24 wakiondolewa nchini.

Katika kushughulikia suala hilo, kamati hiyo ikiongozwa na Profesa Edda Lwoga, ilipendekeza ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kuanzisha kanda maalumu ya biashara Kariakoo na kanzidata na kulifanya eneo hilo kuwa na hadhi maalumu ya biashara.

“Hilo liende sambamba na kutenga maeneo ya biashara za jumla na rejareja, kuwa na huduma za utoaji huduma za Serikali sehemu moja. Pia, inashauriwa Wizara ya Viwanda na Biashara ipitie na kurekebisha Sera ya Maendeleo ya Biashara ya mwaka 2003, toleo la mwaka 2023, ili iainishe aina ya biashara ambazo wageni wanapaswa kufanya,” alisema Profesa Lwoga.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dk Jafo aliunga mkono maoni ya Ngalula, huku akiwahakikishia wajasiriamali kuwa Serikali inachukua hatua kudhibiti ushindani usio wa haki.

Alisema kuwa Serikali, kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara, imeweka mikakati ya kusimamia shughuli za biashara kwa watu wa jinsia zote, wakiwemo wanawake wajasiriamali, ambao wanapata msaada mkubwa kutokana na umahiri wao wa kusimamia fedha za mitaji.

“Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuboresha mazingira ya biashara. Hata hivyo, wanawake ni nguvu kubwa, na tunatambua ujuzi wenu wa kipekee katika kusimamia biashara, mitaji, na fedha. Kwa hiyo, Serikali itawaunga mkono popote na wakati wowote mtakapoonesha dhamira ya kusonga mbele kibiashara kwa manufaa ya taifa,” alisema Dk Jafo.

Ngalula pia aliwataka wanawake wajasiriamali kuwa makini, kushikilia misingi imara ya biashara, na kupigania nafasi yao halali katika uchumi.

Kwa upande wake, Mwajuma Hamza, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa TWCC, alisema tuzo za Wanawake Viwandani Tanzania ni fursa ya kusherehekea wanawake wa kipekee wanaoleta mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali, ambao wanachangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi kupitia ubunifu na ujasiriamali.

“Maadhimisho ya mwaka huu pia yana umuhimu maalumu, kwani yanaambatana na maadhimisho ya miaka 30 ya Jukwaa la Beijing la utekelezaji, ni hatua muhimu ya kimataifa katika kuendeleza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake,” alisema.

Alisema tukio hilo ni la kihistoria, lililopitishwa mwaka 1995, na limekuwa msingi wa mikakati mbalimbali ya kuimarisha haki za wanawake na uongozi wao duniani.

“Tanzania imekuwa kinara katika kutekeleza Jukwaa la Beijing, jambo ambalo limechangia maendeleo makubwa kwa wanawake katika sekta mbalimbali. Moja ya matokeo ya kuvutia zaidi ni ongezeko la wanawake wajasiriamali mabilionea ambao wamebadilisha taswira ya biashara nchini, wakionesha matokeo chanya ya sera zinazolenga kuwawezesha wanawake,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading