Sarafu mtandao zawaingiza matatani walimu wanne, mfanyabiashara

Sarafu mtandao zawaingiza matatani walimu wanne, mfanyabiashara

Dodoma. Walimu wanne na mfanyabiashara mmoja wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwatapeli wananchi kwa kuwadanganya kuwekeza katika sarafu za kimtandao (cryptocurrency), kisha kutoweka na fedha walizowekeza.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime, ametoa taarifa leo Septemba 11, akieleza kuwa watuhumiwa walikamatwa Septemba 7, 2024, katika Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza kufuatia malalamiko ya wananchi waliodhulumiwa.

Ingawa Misime hakuwataja walimu hao wala shule wanazotoka, amefafanua kuwa watuhumiwa wamehusishwa na ulaghai kwa kufungua mifumo ya kampuni bandia ili kuvutia uwekezaji wa wananchi.

Majina ya baadhi ya kampuni hizo ni MEME BANK, DIGITAL WEALTH INTERNATIONAL, OCTOQUANT AI TRADING, NPAMA FUND, MINDFUL TRADE, na CELESTRIAL TG CRYPTOCURRENCY.

Misime amesema kuwa matapeli hao huanzisha kampuni hizo na kuwapa wawekezaji wa awali fedha kidogo kama faida ili kuvutia wengine wawekeze zaidi.

Hata hivyo, baada ya kukusanya kiasi kikubwa cha fedha, kampuni hizo hufungwa na matapeli hao kutoweka mtandaoni, na kuwafanya wawekezaji kushindwa kuwasiliana nao.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuchukua tahadhari na kuepuka kujiingiza kwenye udanganyifu huu, kwani teknolojia ya uwekezaji wa sarafu za kimtandao bado haijaidhinishwa rasmi nchini.

Wananchi wanashauriwa kutoa taarifa wanapoona ulaghai wowote unaohusisha uwekezaji mtandaoni au biashara za aina hiyo, ili kuepusha kupoteza fedha zao.

Misime amesisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha uhalali wa makampuni au watu wanaohamasisha biashara za mtandaoni kabla ya kujiingiza, kwani wengi wamejikuta wakiibiwa fedha kutokana na kuingia kwenye matapeli wa mtandaoni.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading