Samia akutana na mabalozi, azungumzia mafanikio 2024

Samia akutana na mabalozi, azungumzia mafanikio 2024

Samia akutana na mabalozi, azungumzia mafanikio 2024

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan, amesema mwaka 2025 Tanzania itaendelea kuimarisha ushirikiano na uhusiano wa kimataifa, ikiwa ni pamoja na kutengeneza mazingira yatakayohamasisha biashara na uwekezaji.

Amesema hayo leo Januari 14, 2025 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kusherehekea Mwaka Mpya iliyowakutanisha mabalozi wa mataifa mbalimbali waliopo nchini.

Akitoa tathmini ya mwaka 2024, amesema ulikuwa wa kihistoria ambao pato la Taifa lilikua kwa asilimia 5.4 kutoka asilimia 5.1 ya mwaka 2023.

Amesema katika uwekezaji, Tanzania ilivutia uwekezaji wenye thamani ya Dola 7.7 bilioni za Marekani mwaka 2024.

“Ukuaji huu umeonekana pia Zanzibar ambako tumeshuhudia zaidi ya miradi 160 ya uwekezaji iliyotengeneza ajira 3,376. Ukuaji wa uwekezaji huu unaashiria namna ambavyo mataifa yamekuwa na imani na Tanzania, hivyo tutaendelea kuweka mazingira ya kuvutia uwekezaji,” amesema.

Amesema mbali na kuongezeka kwa uwekezaji pia kumekuwa na maendeleo katika sekta mbalimbali, ikiwamo uuzaji wa bidhaa nje ya nchi ambao hadi kufikia Septemba 2024 thamani yake ilikuwa Dola 15 bilioni kutoka Dola 13.5 bilioni mwaka 2023.

Kwenye sekta ya utalii amesema kwa mwaka 2024 mapato yameongezeka kufikia Dola 3.6 bilioni kutoka Dola 3.4 bilioni mwaka 2023.

“Ukuaji huu umeenda kuchangia asilimia 17 ya pato ya Taifa na asilimia 25 ya fedha za kigeni. Tunaahidi kuendelea kusimamia ukuaji wa sekta hii ili kufikia lengo letu la kupata watalii milioni tano kwa mwaka,” amesema.

Rais Samia amesema eneo  lingine la kipaumbele ni kusimamia vyema mfumo wa kodi, akieleza mwaka 2024 Serikali iliunda kikosi kazi ambacho kimepewa jukumu la kuufanyia mapitio mfumo wa kodi na ripoti inatarajiwa kutoka Machi, mwaka huu.

Katika eneo la utawala Rais Samia amesema falsafa ya 4R imeendelea kuwa mwongozo wa Serikali ambayo imetengeneza mazingira yanayoruhusu majadiliano yanayolenga kuhamasisha umoja na mshikamano kwa faida ya Watanzania wote.

“Hili limetusaidia katika uchaguzi wa Serikali za mitaa (ulifanyika Novemba 27, 2024), amani na utulivu vilitawala na sasa tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu, tumejipanga kuhakikisha uwazi, uwajibikaji na utawala wa sheria vinazingatiwa,” amesema.

Balozi wa Comoro nchini Tanzania, Dk Ahamada El Badaoui akizungumza kwa niaba ya mabalozi wenzake, amesema wako tayari kuunga mkono jitihada zinazofanyika nchini.

Amezitaja jitihada hizo ni pamoja na mapambano dhidi ya ufisadi, kuboresha ustawi wa Watanzania kupitia maendeleo jumuishi, mapambano dhidi ya umaskini, kuboresha mfumo wa elimu na kuhakikisha watu wote wananufaika na utajiri na rasilimali za Tanzania.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading