Sabasaba yamkumbusha Kikwete enzi za utawala wake

Sabasaba yamkumbusha Kikwete enzi za utawala wake

Dar es Salaam. Rais mstaafu Jakaya Kikwete amesema Maonyesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DIFT) yamekuwa ya kipekee kwa kuboreshwa miundombinu, hususani ya barabara tofauti na miaka ya nyuma.

Kikwete ameeleza hayo leo Julai 6, 2024 alipotembelea maonyesho hayo maarufu Sabasaba.

Katika mazungumzo yake alikuwa akilinganisha hali anayoiona na miaka ya nyuma, hususani wakati wa utawala wake.

“Kipindi changu wakati nakuja barabara zilikuwa za vumbi na maombi yangu yalikuwa ni kuhakikisha barabara zinawekwa lami maana ilikuwa unakuja huna mafua lakini unaondoka na mafua,” amesema.

Pia amesema alikuwa anaangalia uboreshaji wa mabanda na bidhaa zinazoonyeshwa kuanzia kwa wageni hadi wazawa na hata waelekezaji wamekuwa wakieleza kitu kwa ufasaha tofauti na miaka ya nyuma.

Akizungumzia nishati safi, Kikwete amesema wakati anapokea uongozi matumizi ya umeme yalikuwa asilimia 10 na matumizi makubwa yalikuwa mjini na siyo kijiji.

Amesema waliamua kuanzisha mradi wa umeme vijijini ambao ulianzia kwa hayati Rais Benjamin Mkapa na yeye alilikamilisha na alipokwenda kwenye ziara mkoani Mara alizindua umeme vijijini na wakati huo ukiwa kwenye vijiji 206.

Wakati huo watu walikuwa wanahitaji umeme vijijini na wangeachiwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambao wanafanya biashara wao wanaangalia sehemu ambayo walikuwa na uhakika wa biashara.

Kikwete ametoa wito kwa watoa huduma wa umeme na gesi kuangalia bei wanazotoza zisiwaumize watumiaji kwani inaweza kuwa sababu ya kurudi kwenye matumizi ya mkaa na kuni.

“Sijui kama takwimu zimebadilika Dar es Salaam walikuwa wanatumia magunia ya mkaa 40,000 kwa siku ni kwa kiasi gani miti imepotea hapo,” amehoji.

Kikwete ametumia zaidi ya saa tano kuzunguka viwanja vya maonyesho vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo Barabara ya Kilwa.

Aliingia uwanjani saa 5.30 asubuhi na hadi saa 11.00 jioni alikuwa bado akizunguka kwenye mabanda kuangalia bidhaa, kununua na kuacha maoni katika baadhi ya sehemu alizotembelea.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading