Sababu tatu zachangia kuua mamia ya vichanga Mwanza

Sababu tatu zachangia kuua mamia ya vichanga Mwanza

Sababu tatu zachangia kuua mamia ya vichanga Mwanza

Mwanza. Zaidi ya watoto wachanga 1,452 walifariki dunia mwaka 2023 mkoani Mwanza huku sababu ya kukosa hewa na maambukizi, zikitajwa kuchangia vifo hivyo.

Akizungumza Novemba 5, 2024 wakati wa uzinduzi wa programu ya utoaji huduma za afya kwa watoto wachanga (NEST360) katika halmashauri tano za Mkoa wa Mwanza, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dk Silas Wambura amesema watoto hao walifia tumboni na wengine kufariki muda mchache baada ya kuzaliwa.

“Na sababu kubwa zinazochangia watoto hawa kufariki ni kukosa hewa, maambukizi na wakati mwingine wajawazito wanakuja wamechelewa kwenye vituo wakati wa kujifungua na wakati mwingine wanakuja vituo vya afya wakiwa wametumia dawa za kienyeji kuongeza uchungu,” amesema Dk Marwa.

Ameongeza kuwa wajawazito hao wanatumia dawa za kienyeji ili kuharakisha uchungu, hivyo dawa hizo zinawaathiri watoto wakiwa tumboni na wengine kufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.

“Na wakati mwingine hizo dawa zinasababisha kizazi kuchanika na kuhatarisha uhai wa mtoto kabla hajazaliwa, wakati mwingine ni maambukizi kwa sababu wanapotumia hizo dawa wengine wanaziweka ukeni, zile dawa zinaleta maambukizi yanayoweza kuwapata watoto wanapozaliwa na kufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa,” ameeleza Dk Marwa.

Dk Marwa amewataka wajawazito kuwahi vituo vya afya wanapohisi dalili za uchungu kwa kuwa kuchelewa kwao husababisha wakati mwingine mtoto kumeza maji ya tumboni na kukisababishia kichanga kupata shida ya upumuaji.

“Mtoto asipopata huduma ya haraka anaweza kufariki kwa sababu mfumo wake wa kupumua una changamoto, kwa hiyo mpango huu utasaidia kuondokana na vifo hivi kwa sababu kwanza utawajengea uwezo watumishi wetu, pili utatusaidia kununua vifaa na vifaa tiba ambavyo kwa maeneo mengine bado ni changamoto,” amesema.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkazi wa NEST360 nchini, Dk Mariam Johari zaidi ya asilimia 80 ya watoto huzaliwa hospitalini, lakini bado watoto milioni 2.3 hufariki kila mwaka duniani.

“Asilimia 80 ya vifo hivi vinaweza kuzuilika. Tanzania imechukua hatua kubwa ya kupunguza vifo vya watoto wachanga ambavyo kwa mwaka 2004/5 vilikuwa vifo 32 kwa kila vizazi hai 1,000 na kupungua hadi vifo 24 kwa kila vizazi hai 1,000 mwaka 2002. Ili kufikia lengo la Maendeleo Endelevu la kuwa na vifo vya watoto wachanga visivyopungua 12 kwa kila vizazi hai 1,000 ifikapo mwaka 2030, Tanzania inapaswa kuimarisha juhudi zake,” amesema Dk Mariam.

Amesema awamu ya kwanza mpango huo ulitekelezwa mkoani Dar es Salaam, Mbeya na Kilimanjaro ambapo vitengo vya huduma za watoto wachanga vilipanuliwa, kutoa vifaa muhimu vya huduma, pamoja na kuwajengea uwezo wahudumu wa afya, awamu ya pili Zanzibar na Mwanza zikiongezwa.

 “Katika awamu ya Pili nchini Tanzania, NEST360 imewekeza dola milioni 7.1 kusaidia juhudi za Serikali za kupunguza vifo vya watoto wachanga. Ufadhili huu utazinufaisha moja kwa moja hospitali 28. Hospitali 25 kati ya hizo ni katika mikoa minne ya Tanzania Bara na hospitali tatu Zanzibar,” amesema Dk Johari.

Amesema mpango huo unahusisha ukarabati miundombinu, ununuzi na utoaji wa vifaatiba, kujenga uwezo kwa madaktari na wahandisi wa vifaatiba ili kutoa huduma bora.

Akizindua mpango huo wa miaka minne kuanzia 2024 hadi 2028 katika Halmashauri za Buchosa, Sengerema, Misungwi, Nyamagana na Ilemala, Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Chagu Nghoma amewataka wataalamu wa afya kutumia utaalamu wao ipasavyo kudhibiti vifo vya watoto wachanga.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading