Sababu baadhi ya wabunifu kupeleka bunifu zao nje ya nchi

Sababu baadhi ya wabunifu kupeleka bunifu zao nje ya nchi

Sababu baadhi ya wabunifu kupeleka bunifu zao nje ya nchi

Dar es Salaam. Kukosekana kwa mazingira rafiki ambayo yanaweza kuleta faida kwa mwekezaji imetajwa kuwa moja ya sababu inayofanya baadhi ya wabunifu kuendeleza mawazo yao katika nchi nyingine tofauti na zile wanazotoka kama Tanzania.

Hili limesemwa leo Jumatano katika mkutano uliowakutanisha wadau wa elimu kutoka vyuo mbalimbali kujadili masuala ya uhaulishaji na namna wanavyoweza kuyafanya matokeo ya utafiti na bunifu kuwa biashara.

Mkutano huo wa siku tatu umeandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) na Programu ya funguo iliyo chini ya Shirika la Kimataifa la Maendeleo (UNDP) ukikutanisha wataalamu kutoka nchini Kenya, India, Uingereza, Uganda na Tanzania.

Kauli hii imekuja wakati ambao Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeshuhudia baadhi ya bunifu za raia wake kufanya vizuri katika mataifa mbalimbali ambako zimeendelezwa jambo ambalo linaifanya nchi kushindwa kunufaika moja kwa moja.

Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa National Innovation Agency, Dk Tonny Omwansa amesema mara nyingi wabunifu wamekuwa wakipata fedha kutoka Ulaya na Marekani hata hivyo wawekezaji wanataka fedha zao zirudi kupitia faida itakayotengenezwa.

Amesema jambo hilo linafanya sasa mwekezaji kuangalia mazingira ambayo wazo hilo litakwenda kutekelezwa, Ikiwa mazingira hayatakua ya kuvutia na wamepata wazo zuri, watamwambia mbunifu kusajili wazo lake katika soko jingine ili waweze kuwekeza.

“Hiyo ndiyo maana ya uwekezaji, wanawekeza fedha ili waweze kupata fedha zao tena. Wanataka kuona faida kutokana na mawazo yanayotekelezwa, sasa hapa sera na motisha ndiyo vinaingia. Wawekezaji wanatafuta motisha ili kuwa na uhakika kwamba rasilimali zao zitaongezeka,” amesema Dk Tonny.

Amesema ikiwa motisha haziko vizuri inatengeneza uwezekano mkubwa wa kumhamishia mbunifu katika soko lingine ndiyo waweke fedha zao.

 Amesema jambo jingine linaloweza kufanya bunifu kuhamishwa ni nchi za Afrika kuwa na utamaduni ambao unafanya watu kushindwa kuaminiana.

Utamaduni huu pia unaenda hadi katika kujenga timu na mtandao utakaowafanya wawekezaji kuwa na uhakika kwamba mawazo yanasimamiwa na timu nzuri ya watu inayoweza kuleta matokeo chanya.

“Kwa sababu wazo halitakuwa lenyewe, unahitaji ujuzi mbalimbali, unahitaji ujuzi wa masoko, unahitaji ujuzi wa kiufundi, unahitaji ujuzi wa kisheria, unahitaji ujuzi wa maendeleo ya biashara hivyo ni lazima ujenge timu inayoweza kukuza mawazo hayo kwa njia hiyo. Na hivyo, wawekezaji watakuwa na uhakika zaidi wanapoona aina hizo za timu,” amesema.

Jambo jingine ambalo ni changamoto ni namna wabunifu wanavyofikiri, huku akifafanua kuwa wawekezaji huangalia namna anavyoweza kutengeneza fedha zaidi kwa kuangalia soko kubwa liko wapi.

“Wao huwa wanajua kwamba soko haliko tu hapa labda Kenya au Tanzania, wanaangalia soko la kimataifa, hivyo, ikiwa tutafanya mawazo yetu kuwa ya kuvutia soko la kimataifa hii inamaanisha kuwa tunahitaji baadhi ya maonyesho, tunahitaji mitandao, tunahitaji ushirikiano ili kuleta suluhisho hizi kwenye masoko mengine,” amesema.

Amesema ikiwa wazo haliwezi kupanuliwa katika soko la ndani na nje basi linakuwa si la kuvutia hivo ni lazima kuhakikisha mawazo yanayotengenezwa yanakuwa ya kuvutia zaidi kwa wawekezaji wa ndani ya nchi husika na hata kimataifa.

Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dk Amos Nungu amesema Serikali imeweka fedha nyingi kuhakikisha bunifu na tafiti zinakuwa na matokeo chanya hivyo ni wakati wa kuangalia namna zinavyoweza kwenda sokoni.

“Dunia ni kijiji hatufanyi kazi peke yetu tunafanya kazi kwenye ulimwengu hivi sasa hivyo tukikutana kama hivi tunabadilishana uzoefu kwa sababu Tanzania tukiwa na utafiti na ubinfu unaweza kutumika Tanzania na nje, hivyo tunapoona mapungufu kwetu tunajitahidi tuyaondoe pale kwenye fursa tubadilishane uzoefu,” amesema Dk Nungu.

Amesema kinachofanyika sasa kinaendana na kasi ya serikali ya kuhakikisha matokeo ya tafiti na bunifu yanafika sokoni.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading