Reli tatu kufungamanishwa Tanzania, gharama usafirishaji kupungua

Reli tatu kufungamanishwa Tanzania, gharama usafirishaji kupungua

Dodoma. Kilio cha gharama za usafirishaji wa mizigo, mfumuko wa bei na uharibifu wa barabara nchini, Serikali imevipatia ufumbuzi kwa kufungamanisha reli zote tatu za MGR (ya zamani), Tazara na reli ya kisasa (SGR) kupitia Kidatu mkoani Mogororo.

Mpango huo ni moja ya kazi zitakazotekelezwa na Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2024/25.

Tangu ubinafsishaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) na shughuli za uendeshaji wa huduma za usafiri wa reli kuchukuliwa na kampuni ya RITES ya India kwa kipindi cha miaka 25, kampuni hiyo haikuweza kufanya vizuri na Serikali iliamua kusitisha mkataba wa ukodishwaji mwaka 2010 na kuanzia Julai 22, 2011 kampuni ilirudi mikononi mwa Serikali kwa umiliki wa asilimia 100.

Lakini hali usafiri haikuwa nzuri na mizigo mingi ilisafiri kwa malori huku abiria wakitumia mabasi.

Wizara ya Uchukuzi leo Jumatatu, Mei 6, 2024 imeliomba Bunge kuidhinisha Sh2.7 trilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na uekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya fedha hizo Sh114.7 bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh2.6 trilioni ni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wazi wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa ameliambia Bunge katika mwaka wa fedha 2023/24, wizara hiyo ilitengewa Sh1.9 trilioni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na hadi kufikia Machi, 2024 Sh1.7 trilioni sawa na asilimia 89.12 ya bajeti ya Maendeleo iliyoidhinishwa zilitolewa.

Amesema katika mwaka ujao wa fedha Serikali itaanza kutekeleza mkakati wa kuhakikisha SGR inaanza kufanya kazi na kujiendesha kibiashara.

“Lengo la Serikali ni kutoendelea kutumia ruzuku kuendesha reli ya SGR mara baada ya kukamilika,” amesema.

Profesa Mbarawa amesema ili kufikia azma hiyo, miongoni mwa hatua zitakaochukuliwa na Serikali ni kufungamanisha reli zote tatu za MGR, Tazara na SGR kupitia kituo cha usafirshaji cha Kidadu (Kidatu Transhipment).

“Reli zote hizo zitawasiliana kwa kuweka ‘Gantry Crane Storage Facilities’ pamoja na kuimarisha reli ya Morogoro, Kilosa hadi Kidatu kilometa 108. Uunganishaji huu utawezesha usafirishaji wa mizigo kutoka kusini mwa Afrika mpaka mikoa yote ya Tanzania pamoja na nchi jirani.

“Kufungamanisha Bandari Kavu za Kwala, Isaka, Bandari za Mwanza na Kigoma na hatimaye Bandari za Dar es Salaam na Tanga kwa kuunganishwa na MGR na SGR,” amesema Profesa Mbarawa.

“Njia hii pamoja na manufaa mengine itaongeza wigo wa matumizi ya reli kwa mizigo ya ndani pamoja na inayotoka na kuingia nchini,” amesema Profesa Mbarawa.

Amesema tofauti na ilivyozoeleka Tanzania imekuwa ikitegemea mizigo inayoletwa kutoka nje ya nchi, hivyo ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na upatikanaji wa mizigo ndani ya nchi, Serikali kupitia Wizara itatekeleza mkakati wa kuchochea upatikanaji wa mizigo kwa kuhamasisha shoroba za kiuchumi.

Profesa Mbarawa amesema kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Taasisi ya Ushoroba wa Kati (Central Corridor Transit Transport Facilitation Agency – CCTTFA), Mfuko wa Chakula Duniani (WFP), na Watumiaji wakubwa wa Bandari za Tanzania wa ndani na nje wamebaini Shoroba kubwa tatu ambazo zitaweza kuchochea upatikanaji wa mizigo ndani ya nchi.

“Shoroba zilizobainishwa kuwezesha upatikanaji ni Ushoroba wa Baridi  ambao utahamasisha mizigo ya  nyama, samaki, matunda, mboga na maua; Ushoroba wa Njano  kwa ajili ya mizigo ya madini; na Ushoroba wa Kichele  ambao utahusisha mizigo mingine, hususan mizigo mikubwa   pamoja na mizigo ya viwandani na kilimo ikiwemo pembejeo.

Amesema utekelezaji wa mkakati huu utawezesha kupatikana kwa mizigo mingi ndani ya nchi na kuwezesha TRC kuingia makubaliano na kampuni kubwa na wateja wa muda mrefu.

“Hatua hii itawezesha TRC pia kuendelea kuratibu usafirishaji kwa kutumia wabia wa sekta binafsi kupitia utaratibu wa Open Access,”alisema.

Vipaumbele vya Wizara

Profesa Mbarawa aliliambia Bunge vipaumbele vya wizara kwa mwaka wa fedha 2024/2025, vinajumuisha kuendeleza ujenzi na uendeshaji wa SGR na kuboresha miundombinu ya reli ya MGR na CGR, pamoja na ununuzi wa vifaa.

Amesema pia Wizara itaboresha uendeshaji wa ATCL, kuimairisha miundombinu ya viwanja vya ndege na kujenga viwanja vipya, kuimarisha usafiri, usalama na mawasiliano katika maziwa makuu nchini.

Kuhusu usafiri wa ardhini, alisema Serikali itaendelea kuimarisha usalama, udhibiti na utoaji wa huduma za usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo, kuboresha miundombinu na uendeshaji wa bandari nchini ikiwa ni pamoja na uendelezaji wa bandari kavu.

Profesa Mbarawa alizungumzia changamoto katika utekelezaji wa majukumu yao kwa mwaka 2023/24, Wizara ya Uchukuzi inakabiliwa na changamoto mbalimbali.

“Baadhi ya changamoto hizo na mikakati ya kuzitatua ni mahitaji makubwa ya fedha za utekelezaji wa miradi mingi ya uchukuzi kuhitaji fedha  nyingi (capital intensive) katika utekelezaji wake.

“Mathalan, mradi wa SGR utagharimu takriban Sh23 trilioni hadi kukamilika kwake,” alisema.

New Content Item (2)

Alisema mkakati wa kulitekeleza hilo ni kuendelea kuhamasisha sekta binafsi kutekeleza baadhi ya miradi inayohitaji uwekezaji mkubwa na hivyo kupunguza gharama kwa Serikali.

Maoni ya wabunge

Wakichangia mjadala wa bajeti hiyo, Mbunge wa Segerea (CCM) jijini Dar es Salaam, Bonnah Kamoli alisema mradi wa SGR umefunga barabara kwa zaidi ya miaka miwili na nusu na kusababisha shida kwa wananchi, wakiwamo wafanyabishara.

Pia, amesema mradi huo umesababisha maji kujaa kwenye makazi ya watu na amemuomba Waziri Mbarawa kulishughulikia tatizo hilo.

Kamoli pia amesema malipo ya fidia kwa wakazi wa Kipunguni waliopisha ujenzi wa uwanja wa ndege hayajalipwa na Serikali kwa takriban miaka 27 sasa huku, wakazi wake wakiishi kama wakimbizi ndani ya nchi yao.

Mbunge wa Nkasi (Chadema), Aidan Kenan amelalamikia kukosekana usafiri kwenye Ziwa Tanganyika akisema ni miaka minane sasa Wizara hiyo imekuwa ikiwataja kwenye vitabu lakini hakuna utekelezaji.

Kenan amesema kukosekana kwa meli ya mizigo kunaikosesha Serikali mapato kwa kuwa asilimia 60 ya mizigo kutoka Tanzania inakwenda Jamhuri ya Kidemokrasi ya Cong (DRC).

Naye mbunge wa Kilombero (CCM), Abubakar Asenga aliomba Wizara hiyo kulipa madeni ya wakandarasi kwa kuwa miradi mingi imekwama.

Amesema wameshuhudia kuwepo madeni ya wakandarasi maeneo mengi ya nchi na wanalalamika hawajalipwa na ameiomba Serikali ipunguze madeni yao ili sekta iweze kwenda vizuri.

 Maoni ya Kamati

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Miundombinu, Moshi Kakoso akisoma maoni ya kamati alibainisha uchache wa fedha katika baadhi ya miradi ulivoyosababisha kusuasua kwa miradi hiyo.

Ameutaja mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kikanda cha Kuratibu Utafutaji na Uokoaji Majini (MRCC) kwamba unatakiwa kukamilika ifikapo Novemba, 2024, lakini hadi kufikia Machi, 2024 fedha iliyolipwa kutekeleza mradi ilikuwa Sh953.9 bilioni sawa na asilimia 20 tu.

“Mapokezi yasiyoridhisha ya fedha za mradi, kwa sehemu kubwa yameathiri utekelezaji wa mradi ambapo hadi Kamati inafika uwandani kwa ajili ya ukaguzi, ujenzi wa mradi ulikuwa ni asilimia 10.

Kakoso aliutaja ujenzi wa mradi wa SGR kipande cha tano (Isaka- Mwanza) kwamba hadi kamati inatembelea Machi, 2024, Serikali ilikuwa imeshafanya malipo kwa Mkandarasi ya Sh1.3 trilioni sawa na asilimia 40.53 ya gharama za mradi huku maendeleo ya mradi yakiwa yamefikia asilimia 54.01.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading