Rais Samia kufanya ziara Ethiopia, kushiriki mkutano AU

Rais Samia kufanya ziara Ethiopia, kushiriki mkutano AU

Rais Samia kufanya ziara Ethiopia, kushiriki mkutano AU

Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi nchini Ethiopia kuanzia Februari 15 hadi 16 sambamba na ziara hiyo atashiriki mkutano wa Umoja wa Afrika (AU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Februari 13, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga, imeeleza kuwa mkutano huo utamchagua mwenyekiti mpya wa AU.

“Rais Samia atashiriki mkutano wa kawaida wa 38 wa wakuu wa nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

“Mkutano huo unatarajia kuchagua mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika kwa mwaka 2025 atakayechukua nafasi ya mwenyekiti wa sasa Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Pia, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo mwenyekiti, makamu mwenyekiti na makamishna sita.

“Vilevile, mkutano utajadili taarifa ya ushiriki wa Umoja wa Afrika kwenye Mkutano wa Nchi Tajiri Duniani (G20), utekelezaji wa ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na taarifa kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

“Mbali na masuala hayo, Mkutano utajadili ajenda kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia iliyopendekezwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” imeeleza taarifa hiyo.

Kabla ya kushiriki mkutano wa 38, Rais Samia atashiriki mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika utakaofanyika Februari 14, 2025.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading