Rais Samia awapa mbinu wamiliki wa mabasi kukabili ushindani wa SGR

Rais Samia awapa mbinu wamiliki wa mabasi kukabili ushindani wa SGR

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amesema licha ya athari zilizoanza kujitokeza kwa wamiliki wa mabasi na malori, bado Tanzania ina fursa nyingi za wasafirishaji hao kunufaika.

Msingi wa kauli ya mkuu huyo wa nchi ni kile alichoeleza, kuanza kwa mradi wa treni ya umeme ya abiria kwa namna fulani kumesababisha kupungua kwa mabasi barabarani katika njia unakopita mradi huo.

Amesema hali kama hiyo inatarajiwa katika usafirishaji wa mizigo kwa malori, pale treni hiyo itakapoanza kusafirisha.

Pamoja na athari hizo, Rais Samia amesema bado wasafirishaji hao wana fursa ya kunufaika hasa katika njia nyingine ambazo mradi huo haujafika.

Rais Samia ameyasema hayo leo Alhamisi Agosti 1, 2024 alipozungumza na vyombo vya habari akiwa ndani ya treni ya SGR kuelekea Stesheni ya Pugu, ikiwa ni uzinduzi wa safari za treni ya umeme kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma.

Hata hivyo, amesema kupungua kwa mabasi barabarani inaweza kuwa athari mbaya kwa wafanyabiashara lakini nzuri kwa Serikali kwa kuwa itapunguza ajali.

“Hasara moja ambayo imeanza kuonekana ni kupungua kwa mabasi barabarani, kwa wafanyabiashara ni mbaya lakini kwa nchi ni nzuri kwa sababu inapunguza ajali pia na sasa usafiri barabarani unadhibitiwa vizuri,” amesema.

Hata hivyo, ameeleza bado wasafirishaji hao hawataathirika kwa kuwa kuna njia nyingine treni hiyo haijafika na hivyo wanayo nafasi ya kupeleka mabasi huko.

“Lakini sasa wanapunguza mabasi eneo moja ambalo tayari kuna maendeleo haya, lakini Tanzania ni kubwa kuna maeneo ambayo yanahitajika kwa hiyo sasa yatakwenda kule,” amesema.

Athari pia, amesema zitashuhudiwa katika usafirishaji wa mizigo kupitia malori, hasa pale ambapo treni hiyo itaanza kubeba mizigo, lakini bado kutakuwa na maeneo ambayo hayatakuwa na mradi huo.

Katika maungumzo yake akiwa ndani ya treni kutoka stesheni ya Posta kwenda ile ya Pugu, mkuu huyo wa nchi ameeleza furaha yake ya kufanikiwa kukamilisha miradi waliyoanzisha akiwa na mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.

“Nina faraja kusema kwamba yale ambayo niliyaanza na mwenzangu marehemu (Magufuli) nimeyakamilisha kwa hiyo ni miradi ambayo kwa Tanzania ni muhimu sana,” amesema.

Hata hivyo, aliusifu uamuzi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuanza safari za kwenda Dodoma Julai 25, mwaka huu akisema alivyoona alifurahia, akidokeza: “(Kadogosa, Mkurugenzi Mkuu wa TRC) alikuwa anaogopa kutumbuliwa.”

Katika hatua nyingine, amesema hautazami mradi huo kwa sura ya kibiashara pekee, bali wakati mwingine anautazama kama huduma kwa kuwa una manufaa katika maeneo mengine.

Sababu ya kupambania utekelezwaji wa mradi huo ni kile alichoeleza, analenga kuiunganisha Tanzania na mataifa ya Burundi na Jamhuri ya Demokrasi ya Congo ili kupata soko la bidhaa.

Amesimulia zamani aliwahi kupanda treni la awali (MGR) kutoka Dar es Salaam hadi Moshi na akiwa njia alikumbwa na changamoto lukuki likiwemo vumbi.

“Hadi kufikia hatua iliyofikiwa sasa namshukuru Mungu na kwamba namuomba Mungu njia yote imalizwe hadi kufikia Burundi,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Insecurity prompts Zanzibar to review its lucrative island leasing

The Tanzanian central government is planning to boost its security presence in the Zanzibar archipelago. A commission tasked with auditing the country’s security forces was appointed in July by President Samia Suluhu Hassan. It says it is concerned about the situation in the country’s Indian Ocean islands that are under the control of the semi-autonomous Zanzibar local government.Continue Reading

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading