Rais Samia ateua Katibu wa Bunge, Jaji wa Mahakama Kuu

Rais Samia ateua Katibu wa Bunge, Jaji wa Mahakama Kuu

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Baraka Leonard kuwa Katibu wa Bunge, kuchukua nafasi ya Nenelwa Mwihabi, aliyeteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Uteuzi huo umetangazwa leo Jumatatu, Septemba 16, 2024 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais-Ikulu ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka.

Taarifa hiyo ya uteuzi imeeleza, viongozi hao wawili wataapishwa Alhamisi ya Septemba 19, 2024, saa 9n alasiri, Ikulu ya Dar es Salaam.

Katika taarifa hiyo, haikuweka wazi Leonard ametoka wapi. Nenelwa anakwenda kuwa Jaji baada ya kuhudumu nafasi ya Katibu wa Bunge kwa takribani siku 1,220 sawa na miaka mitatu na miezi minne. Kabla ya uteuzi huo, Nenelwa alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Shughuli za Bunge.

Uteuzi huo wa Nenelwa uliofanywa na Rais Samia, Mei 15, 2021 ulimfanya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo.

Nenelwa aliteuliwa kuchukua nafasi ya Stephen Kagaigai ambaye wakati huo, aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Kwa sasa Mkuu wa mkoa huo ni Nurdin Babu na Kagaigai ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading