Rais Samia ataka ushirikiano Serikali, sekta binafsi kuboresha huduma za afya

Rais Samia ataka ushirikiano Serikali, sekta binafsi kuboresha huduma za afya

Rais Samia ataka ushirikiano Serikali, sekta binafsi kuboresha huduma za afya

Unguja. Rais Samia Suluhu Hassan amesema licha ya jitihada zinazochukuliwa na Serikali kuboresha huduma za afya kwa wananchi bado kuna changamoto ya utoaji huduma, hivyo ushirikiano wa sekta binafsi utasaidia kuziimarisha.

Ametaja changamoto hizo kuwa ni uhaba wa wafanyakazi wenye ujuzi, upungufu wa vifaatiba na uchakavu kwa baadhi ya miundombinu.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Oktoba mosi, 2024 kupitia hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 11 la Afya Tanzania (THS) lililofanyika Fumba, wilayani Magharibi B, Unguja.

Kongamano hilo limewakutanisha wataalamu zaidi ya 1,500.

“Ni vyema mkafahamu pamoja na hatua zinazofikiwa bado kuna changamoto katika utoaji wa huduma, hivyo Serikali itaendelea kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma kwa wananchi ambao ushirikiano huo unakusudia kuimarisha huduma bora za afya nchini,” amesema Rais Samia.

Amesema Serikali itaendelea kuboresha elimu kwa wataalamu wa afya kwa kutoa kipaumbele na kuongeza ufadhili kwa mafunzo ya ubingwa na ubingwa bobezi katika taaluma za kimkakati.

Kuna umuhimu wa kushirikiana na sekta binafsi katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Rais Samia amesema Serikali zote mbili zinaendelea kuimarisha matumizi ya mifumo ya utoaji wa taarifa ili iweze kusomana kutoka kituo kimoja cha afya kwenda kingine katika ngazi zote za utoaji wa huduma kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa taarifa za wagonjwa, zikiwamo vipimo na matibabu.

Pia, kutoa fursa ya kupata matibabu zaidi katika maeneo yote ya nchi.

“Serikali zote (SMT na SMZ) zinaendelea kuchukua hatua za kuimarisha huduma za kinga, kuwekeza katika miundombinu ya afya kwa kujenga na kukarabati hospitali zote na vituo vya afya ili ziweze kutoa huduma bora na za kisasa kwa wananchi wa pande zote mbili za Muungano,” amesema Rais Samia.

Ametoa wito kwa taasisi za Serikali na binafsi kushirikiana na THS kuongeza nguvu ya majadiliano katika sekta ya afya na kuboresha utoaji huduma za afya mijini na vijijini.

Awali, akitoa taarifa ya kitaalamu kwa niaba ya bodi ya THS, Dk Grace Magembe amesema imekuwa ni chachu ya kuleta mabadiliko endelevu katika sekta ya afya hasa katika kuhamasisha utoaji huduma kwa mifumo ya kidijitali ili kuendana na wakati.

Dk Grace amesema THS imewawezesha vijana kupitia programu ya kuwajengea uwezo kwa kuwapatia mafunzo, kuwaendeleza kitaaluma na kuwaunganisha watumishi wa afya na fursa zilizopo nje ya nchi.

“THS ina jukumu kubwa la kuendelea kushirikiana na Wizara ya Afya katika kuboresha na kuimarisha sekta hasa katika eneo la kutoa elimu ya afya kwa jamii,” amesema Dk Grace.

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama amezikaribisha sekta binafsi kushirikiana na Serikali katika kujenga huduma za kibingwa ili kuifanya Tanzania kuwa kituo cha utalii wa tiba.

Amesema bado Serikali inahitaji ushirikiano na sekta binafsi katika maeneo mbalimbali.

Kuhusu bima ya afya kwa wote, Jenista  amesema Serikali inapokwenda katika utekelezaji, sekta binafsi inapaswa kushirikiana nayo kwa kuhakikisha huduma bora na rahisi zinapatikana.

“Pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali lazima kuhakikisha sekta binafsi inaimarishwa ili kulinda usalama wa wananchi,” amesema.

Waziri wa Afya Zanzibar, Ahmed Mazrui amesema ubia wa sekta binafsi umekuwa na mafanikio makubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya vifaatiba vya kisasa.

Amesema hospitali binafsi zimewekeza na kuhakikisha zinatoa huduma bora kwa wananchi.

Waziri Mazrui amesema changamoto zilizopo zinaendelea kushughulikiwa hatua kwa hatua hivyo zinazidi kupungua.

Amesema wameimarisha vituo vya afya ya msingi 52 na kujenga vipya 96 ili kufikia mwakani huduma za afya ziwe bora zaidi kwa wananchi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading