Usiku wa fahari kwa Morocco – Qatar 2022

Usiku wa fahari kwa Morocco – Qatar 2022

Ufaransa kukutana na Argentina baada ya kuilaza Morocco

Ufaransa ilisukumwa na wachochole wa Kombe la Dunia Morocco kabla ya mabingwa hao kufuzu katika fainali ya Jumapili dhidi ya Argentina.

Kikosi cha kwanza cha Afrika kutinga nusu fainali ya Kombe la Dunia kilikataa kufurukuta licha ya kupata vipigo vya mapema vya kumpoteza mlinzi wake Nayef Aguerd aliyepata jeraha  baada ya kutajwa kwenye kikosi cha kwanza, na kisha kwenda nyuma kwa bao la Theo Hernandez dakika ya tano.

Ufaransa, kwa juhudi na ari ya Morocco, walifanya vyema zaidi na mchezaji wa akiba Randal Kolo Muani alihakikisha kwamba wanatetea taji lao dhidi ya Argentina na Lionel Messi katika Uwanja wa Lusail siku ya Jumapili alipofunga kombora la Kylian Mbappe dakika 11 kabla ya mchezo kumalizika.

Morocco pia walimpoteza Romain Saiss ambaye hakuwa fiti kwa kuumia kabla ya kipindi cha kwanza kwenda mapumziko lakini, wakishangiliwa na maelfu ya mashabiki , walikaribia kufikia kiwango chao, hasa pale shambulio la Jawad El Yamiq lilipopanguliwa na kipa wa Ufaransa, Hugo Lloris.

Ufaransa, ikiwa na mlinzi wa Liverpool Ibrahima Konate aliyekuwa thabiti mbele ya kipa wao , walidumisha utulivu katika anga ya Al Bayt Stadium na wakapata nafasi zao, huku Olivier Giroud akigonga mwamba wa lango katika kipindi cha kwanza.

Kikosi cha Didier Deschamps kilitishia wakati wote wa mapumziko na hivyo kilidhihirika kuwa Muani aliyekuwa akinyemelea hatimaye alivunja safu ya ulinzi ya Morocco kwa mguso wake wa kwanza, sekunde 44 na kufunga bao lake la kwanza la Ufaransa na la pili kwa mabingwa hao watetezi.

Ufaransa yacheza kwa utulivu

Ufaransa ililazimika kucheza kwa utulivu ili kuwa nchi ya kwanza kuhifadhi Kombe la Dunia kwa miaka 60 kufuatia ushindi wa Brazil mwaka 1958 na 1962.

Walikumbana na ukuta wa kelele kutoka kwa mashabiki wa Morocco, Pamoja na filimbi za kupasua masikio kila walipokuwa wakimiliki, na licha ya kushindw kuonesha mchezi mzuri kama ilivyo kawaida yao, Ufaransa ilijizatiti na kuhakikisha kuwa inatinga fainali dhidi ya Argentina siku ya Jumapili

Konate, aliyeingia katika nafasi ya Dayot Upamecano ambaye alikuwa anauguza jeraha alidhibiti ngome ya ulinzi ya Ufaransa na kocha Didier Descahmps hakupata shinikizo yoyote ya kufanya mabadiliko katika safu hiyo. siku ya Jumapili.

Na bila shaka, simulizi ya Mbappe dhidi ya Messi itafikia kilele chake siku ya Jumapili huku Ufaransa ikijaribu kurudia ushindi wao wa 2018 mjini Moscow ilipoifunga Croatia katika fainali.

Deschamp ambaye amekuwa hatambuliwi amefanikiwa kuweka pamoja timu ya Ufaransa inayoongozwa na Mbappe na walifanikiwa kuonyesha umahiri wao wakati mwingine.

Ufaransa, hata hivyo, imejikatia tiketi ya fainali nynegine ya kombe la Dunia na Deschamps mwenye umri wa miaka 54, ambaye alikuwa nahodha walipotwaa taji katika ardhi ya nyumbani mwaka 1998, sasa ana nafasi ya kuweka historia kwa kushinda michuano hiyo mara mbili mfululizo akiwa kocha.

Usiku wa fahari kwa Morocco

Mashabiki wa Morocco kote ulimwenguni wakishangilia kwa fahari timu yao

Wachezaji wa Morocco na timu ya wakufunzi walikuwa wakitoa shangwe kubwa na la muda mrefu kutoka kwa mashabiki wao, ambao wamekuwa kivutio cha kweli katika Kombe hili la Dunia, walipokwenda kwao kuwapatia shukran baada ya filimbi ya mwisho.

Na ilistahili kabisa baada ya utendaji mwingine wa talanta na tabia ambayo ilionyesha kwa nini wamekuwa kifurushi cha kushangaza kwenye Kombe hili la Dunia.

Kocha wa Morocco Walid Regragui angeweza kusamehewa kwa kuhisi hatima ilikuwa dhidi yao baada ya kupoteza wachezaji muhimu muda mfupi kabla ya mechi kuanza, pamoja na kurudi nyuma.

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year’s Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Insecurity prompts Zanzibar to review its lucrative island leasing

The Tanzanian central government is planning to boost its security presence in the Zanzibar archipelago. A commission tasked with auditing the country’s security forces was appointed in July by President Samia Suluhu Hassan. It says it is concerned about the situation in the country’s Indian Ocean islands that are under the control of the semi-autonomous Zanzibar local government.Continue Reading

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading