Polisi Iringa yawashikilia wawili kwa kukutwa na magobore matano

Polisi Iringa yawashikilia wawili kwa kukutwa na magobore matano

Iringa. Jeshi la Polisi mkoani Iringa linawashikilia watu wawili kwa tuhuma ya kukutwa na bunduki za kienyeji aina ya gobore tano wanazodaiwa kuzitumia kufanyia ujangili.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Iringa, Kamishna Msaidizi, Alfred Mbena amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika operesheni za  mara kwa mara zinazoendelea kufanyika mkoani humo.

Watuhumiwa hao  ambao ni Afya Kityega (47), mkazi wa Idodi na Fredy Lukosi  (25) mkazi wa Kijiji cha Ugwachanya, baada ya kupekuliwa walikutwa na chupa mbili za baruti, kamba ya manila, rissington za gobore  ambavyo ni vipande vya nondo na begi dogo jeusi.

Amesema watuhumiwa baada ya kuhojiwa wamekiri kuzitumia silaha hizo kutekeleza vitendo vya ujangili.

Wakati huohuo Jeshi hilo linamshikilia Thomas Ngoti (37) mjasiriamali na mkazi wa Mgera Kihwele mkoani Iringa akiwa na kofia, suruali moja, mkanda mmoja na begi ambazo ni sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania  (JWTZ ).

Amesema mtuhumiwa alikamatwa  eneo la makazi ya Mkuu wa Mkoa  wa Iringa, Kata ya Gangilonga  na baada ya kuhojiwa alidai  kuwa nguo hizo ni mali yake na amewahi kuwa askari  wa Jeshi hilo kabla ya kuacha kazi.

Katika tukio lingine, Polisi wanawashikilia watu watano wakiwa na vipande vinne vya meno ya tembo.

Amesema watuhumiwa wamekamatwa wakiwa kwenye mkakati wa kufanya biashara  hiyo ndani ya nyumba moja ya kulala wageni eneo la Ruaha Mbuyuni wilayani Kilolo.

Kamanda Mbena amesema watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading