Othman atangaza nia kugombea urais Zanzibar

Othman atangaza nia kugombea urais Zanzibar

Othman atangaza nia kugombea urais Zanzibar

Unguja. Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman ametangaza nia ya kugombea urais wa Zanzibar kwenye uchaguzi mkuu ujao endapo chama chake kitaridhia na kumpa jukumu hilo ili awasaidie Wazanzibari.

Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, amebainisha hayo leo Januari mosi, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi huo huku akiuita mwaka 2025 ni “mwaka wa maamuzi.”

Katika mkutano huo uliofanyika Unguja, Zanzibar, Othman ameangazia miaka minne ya Serikali ya Rais Hussein Ali Mwinyi, akisema imetawaliwa na ufisadi wa fedha za umma hasa kwenye miradi ya maendeleo ambayo zabuni zake hazitangazwi popote kwa kushindanisha wazabuni.

Hata hivyo, Msemaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Charles Hillary amesema hivi karibuni Rais Mwinyi atafanya mkutano na vyombo vya habari kuzungumzia tuhuma za ufisadi zinazotolewa na kiongozi huyo.

“Hayo anayoeleza ndiyo hayo kila siku anayaeleza na mheshimiwa Rais alishayajibu. Issue ya tender (zabuni), ukiweka tenda kwa hali yetu ilivyo, hii ni Januari, ule mchakato ukiisha itakuwa ni Septemba na sisi tunataka vitu viende kwa haraka. Lakini tusubiri, Rais ataongea,” amesema Hillary.

Atangaza nia ya urais

Othman amesema amejipima binafsi na kubaini ingawa yeye si mtimilifu wala mkamilifu, lakini anaamini hana kikwazo cha kuyatafuta yale aliyopungukiwa katika sifa za mtu sahihi wa kuinusuru Zanzibar. 

“Napenda kwa heshima kubwa kutumia fursa hii kutangaza rasmi kwamba nimekusudia, Inshaallah itapofika wakati wa kuanza mchakato wa kutafuta wagombea katika chama changu, kwa kufuata taratibu ziliopo, kukiomba chama changu cha ACT Wazalendo kinibebeshe dhamana ya kukiwakilisha kwenye nafasi ya kuwania uongozi wa juu wa nchi yetu, ule wa Rais wa Zanzibar ili muda ukifika tuje tuwaombe Wazanzibari, watupe sisi ACT Wazalendo jukumu la kuwatoa hapa mahala walipo na tuwapeleke kwenye maendeleo, uhuru wa kweli na ustawi,” amesema Othman.

Amesema watachukua jukumu hilo kwa sababu wanajua nini kifanyike ili kuipata Zanzibar ya aina hiyo huku akisema imebaki miezi kumi kabla ya uchaguzi mkuu, hivyo ataendeleza wajibu wake wa kuwaelimisha wale ambao wamewatia hofu.

Ametolea mfano nchi za visiwa kama Mauritius, Singapore, Seychelles, Hong Kong, Taiwan na nyinginezo kwamba, zimefika si kwa kuongozwa na itikadi zilizojaa ufisadi, dhulma na ubaguzi bali, kwa sababu yalifanya kazi hiyo kwa manufaa ya watu katika mataifa hayo ya visiwa ikiwamo kujenga Serikali zenye ufanisi, uadilifu na uwajibikaji.

Amesema akiwa Mzanzibari na kiongozi wa chama chake, amejaribu kukiambia chama tawala kuwa sera zake za kizamani zilikuwa zikiwafukarisha Wazanzibari.

Othman amedai itikadi ya kuendesha Muungano kwa misingi wa siasa ya kuidhibiti Zanzibar, haiwezi kulisaidia Taifa hilo, hivyo ni wakati wa kuzingatia masilahi mapana ya kiuchumi na ustawi kwa wananchi na kila upande kuwa na fursa ya kuendelea.

Kiongozi huyo wa chama amesema imebakia miezi 10 kabla ya uchaguzi, hivyo ataendelea na wajibu wa kuwaelimisha wale ambao wamewatia wananchi hofu kwa miongo sita huku akiwaeleza mbadala wa kukabiliana na changamoto zilizopo.

“Tunaukaribisha mwaka huu mpya kwa lengo moja tu, ambalo ni kuinusuru Zanzibar kutoka mikononi mwa utawala uliojengwa katika misingi ya ufisadi uliopora matumaini ya kila kitu; ya kiuchumi na raia kutendewa haki. Sote ni mashahidi, Zanzibar imepitia katika misukosuko mingi,” amesema Othman.

Udhaifu wa SUK

Othman amesema Serikali ya Umoja wa Kitaifa(SUK)  imekuwa ikisuasua kutokana na kukosekana kwa dhamira ya dhati ya kushirikiana na ACT Wazalendo.

Kiongozi huyo amedai kuwa, ACT Wazalendo hawashirikishwi kwenye baadhi ya mambo kama ilivyotarajiwa.

“Mkwamo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa umesababishwa na kukosekana kwa dhamira. SUK ilipoanzishwa baada ya kurekebisha Katiba, ililenga ushirikiano wa vyama vinavyounda Serikali, lakini hilo wenzetu hawalitaki.

“Ilitakiwa kama mwenyekiti wa halmashauri ni wa CCM, basi makamu wake atoke ACT Wazalendo. Kama mwenyekiti wa kamati ya Baraza la Wawakilishi ni CCM, basi makamu wake atoke kwetu, haya yote hayafanyiki,” amesema Othman.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading