Mwelekeo mpya matumizi ya magari ya umeme Tanzania

Mwelekeo mpya matumizi ya magari ya umeme Tanzania

Mwelekeo mpya matumizi ya magari ya umeme Tanzania

Dar es Salaam. Wakati mwamko wa matumizi ya vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme ikiwemo pikipiki na magari ukiongezeka nchini, wadau kwa kushirikiana na Serikali wamekutana kujadili mfumo utakaotoa mwongozo wa uingizaji na utumiaji wa vyombo hivyo.

Uwepo wa mafundi wabobezi, uingizaji wa vyombo hivyo, gharama, taratibu za usajili, utambuzi na uelewa ni miongoni mwa yaliyojadiliwa katika warsha hiyo.

Warsha hiyo ya maendeleo ya mfumo wa kitaifa wa kuhamia matumizi ya umeme (e-mobility) imefanyika leo Desemba 17, 2024 jijini Dar es Salaam.

 Imeelezwa moja ya faida ya matumizi ya vifaa mwendo vinavyotumia umeme ni pamoja na kutochafua mazingira, gharama ndogo za kuchajisha na kupunguza hewa ukaa na hewa joto.

Miongoni mwa vigingi vinavyoikabili sekta hiyo hapa nchini ni uhaba wa wataalamu, kodi kubwa na changamoto za kisera.

Kwa mujibu wa ripoti ya E-Mobility Alliance iliyotolewa Machi 2023, Tanzania ina vyombo vya moto vinavyotumia umeme 5,000 idadi ambayo ni ndogo kutokana na uelekeo wa dunia katika matumizi ya nishati safi, lakini ni kubwa kwa nchi za Afrika Mashariki.

Pengine idadi ya vyombo hivyo ingekuwa zaidi ya hiyo, lakini ripoti hiyo inaeleza uwepo wa changamoto hizo kama kodi kubwa katika bidhaa hizo, uelewa mdogo wa jamii, umbali wa huduma za umeme na kutokuwepo kwa sera za wazi.

Akizungumza na Mwananchi Digital kwenye warsha hiyo, Meneja wa Ubunifu na Teknolojia kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk Gerald Kafuku amesema kwa sasa muundo wa kisera unatengenezwa na utaunganishwa kisha utapelekwa wizara za fedha na uchukuzi kwa ajili ya kuingizwa kwenye mwaka ujao wa fedha 2024/25.

 “Ziingizwe kwenye sheria ya kodi ili kuwe na mazingira wezeshi yatakayofahamika kitaifa kwa ajili ya kutumika kusajili vyombo hivyo na hata miundombinu ya kuchajia. Tunafikiria hata watu wenye vituo vya mafuta wawe na sehemu za kuchajia hivyo inabidi waelewe ndio maana tumekutana ili kujadili,” amesema Dk Kafuku.

 “Wenzetu Taasisi ya Nishati Jadidifu ya Elico Foundation tuliokutana nao hii leo wanaandaa muundo wa kisera kwa upande wa pikipiki za matairi mawili na matatu, halafu kama Taifa tunaandaa muundo wa kisera wa ujumla kwa vyombo vyote,” amebainisha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Elico, Sisty Basil amesema wameamua kushirikiana na Serikali kuanzia kujifunza kwa nchi zilizoendelea kwenye uendeshaji wa vyombo hivyo.

Amesema waliamua kwenda na Serikali kujifunza kwa nchi zilizoendelea kama China juu ya changamoto, vituo vya kuchajia, sehemu za kubadilishia betri ili kupata ujuzi zaidi.

“Baada ya kujifunza tukagundua tuwe na sera moja ya kushusha bei ya uingizaji, kuwa na vyuo vitakavyozalisha mafundi pale tutakapokuwa na magari, hivyo tumeamua kukutana kujadiliana tuliyoyaona huko na mapendekezo yetu kwenye rasimu ya sera ikiwemo kutatua changamoto,” amesema.

Amesema Tanzania bado haina sera inayosimamia magari ya umeme hivyo mawasilisho hayo yataenda kwenye mapendekezo ya sera ya Tanzania ya magari ya umeme, kisha kwenda bungeni na baadaye kuwa sheria.

Mkuu wa idara ya umeme wa Chuo cha Ufundi Arusha, Mhandisi Ally Ngulugulu amesema kupatikana na teknolojia hiyo mpya ya E-Mobility wamejiandaa kuhuisha mitaala kwa ajili ya kuzalisha wataalamu watakaoendana na teknolojia hiyo ya kisasa.

Ofisa usafiri wa  Wizara ya Uchukuzi Idara ya huduma za uchukuzi, Mario Kazimoto amesema suala la vyombo vya usafiri vya umeme, linapaswa kuungwa mkono kutokana na kuwa na faida kemkem ikiwemo kutokuwa na kelele.

Amesema hata Serikali inaunga mkono akitolea mfano kuanza kwa treni ya umeme ya (SGR).

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading