Mwakilishi afariki dunia akipatiwa matibabu India

Mwakilishi afariki dunia akipatiwa matibabu India

Unguja. Mwakilishi wa viti maalumu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Panya Ali Abdalla (60) amefariki dunia akipatiwa matibabu nchini India.

Akizungumza hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (Sera, Utaratibu na Baraza la Wawakilishi), Hamza Hassan Juma amesema Serikali kwa kushirikiana na familia, inaendelea kuratibu mipango ya mazishi na kurudisha mwili wa marehemu nchini.

Mwakilishi Panya amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kabla ya kupelekwa India alianza kupatiwa matibabu katika hospitali tofauti nchini.

Kwa mujibu wa Hamza, Panya amefariki dunia usiku wa kuamkia Julai 25,2024   na kwamba mwili unatarajiwa kupokewa Julai 27, 2024 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar na kukabidhiwa kwa ndugu kisha kuzikwa siku hiyohiyo.

“Kwa upande wetu Serikali tumekamilisha mipango ya kusafirisha mwili na watu ambao walimuuguza. Tunatarajia mwili huo utapokewa Jumamosi mchana na watakabidhiwa familia yake, kisha kwenda moja kwa moja kuzikwa,” amesema Hamza.

Baadhi ya wawakilishi wamesema wamepoteza mtu muhimu aliyekuwa na mchango mkubwa siyo tu katika Baraza la Wawakilishi bali Serikali kwa ujumla.

Mwakilishi wa kuteuliwa, Juma Ali Khatib amesema wamepokea taarifa za msiba huo kwa mshutuko kwani alikuwa mahiri na aliyesaidia kwa kiasi kikubwa kufanikisha mipango ya Serikali.

“Ni msiba mzito, tumempoteza mtu muhimu ndani ya baraza, mchango wake utakumbukwa ndani na nje ya baraza na serikalini,” amesema.

Amesema wajumbe wa baraza walikuwa Arusha kwa shughuli za michezo lakini baada ya taarifa za msiba huo imewalazimu kuzisitisha.

“Wajumbe wote tulikuwa Arusha kwenye mafunzo maalumu na michezo lakini baada ya kupata taarifa hizi leo Julai 26 tunarudi Zanzibar kwa ajili ya kushiriki shughuli za kumuaga mwenzetu,” amesema.

Katika Baraza la Wawakilishi amekuwa mwenyekiti wa kamati mbalimbali ikiwemo ya maadili.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopo katika tovuti ya Baraza la Wawakilishi, Panya aliyezaliwa Februari 5, 1964 alikuwa mjumbe wa baraza hilo tangu mwaka 2010.

Kabla ya kuwa mwakilishi alishika nyadhifa mbalimbali za Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) ikiwemo mwenyekiti wa wazazi Wilaya ya Kaskazini B, Unguja mwaka 2003 hadi 2012.

Pia alikuwa mjumbe wa kamati ya siasa mwaka 2003 hadi 2012, mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mwaka 2012/17 na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) mwaka 2012/17.

Ni mwakilishi wa pili kufariki dunia tangu uchaguzi mkuu umalizike mwaka 2020 akitanguliwa na mwakilishi wa Mtambwe, Kisiwani Pemba kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Habib Ali Mohammed aliyefariki dunia Machi 3, 2023 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Saifee, jijini Dar es Salaam.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading