Mwakagenda na safari yake ya siasa za Tanzania

Mwakagenda na safari yake ya siasa za Tanzania

Mwakagenda na safari yake ya siasa za Tanzania

Dar es Salaam. Alipojitosa kuwania ubunge, Sophia Mwakagenda anasema moja ya neno ambalo hawezi kulisahau ni namna baadhi ya watu walivyomshambulia binafsi na si katika hoja alizokuwa akitoa kama mgombea kwenye majukwaa ya kisiasa.

Anasema ilitengenezwa kampeni watu wakihamasishana wasimchague kwa madai kwamba ana nyonyo moja, wakimaanisha titi.

“Niliwauliza kwani bungeni nakwenda kunyonyesha? jibu likawa hapana, hata hivyo sikurudi nyuma kwa maneno yao, niliwambia wanipime kwa uwajibikaji na utendaji na si mwili wangu,” anasema Mwakagenda ambaye kwenye uchaguzi wa 2020 aligombea Rungwe kwa tiketi ya Chadema na kupata kura zaidi ya 30,000.

Mwakagenda ni miongoni mwa wanasiasa wengi wanawake waliokutana na changamoto kadha wa kadha kwa sababu ya uanamke wao, lakini hawakurudi nyuma.

Katibu Mkuu wa UDP, Saumu Rashid anasema jamii ndiyo inapaswa kubadilika kuhusu udhalilishaji wa wanawake wanaoingia kwenye siasa.

Akitolea mfano alioutaja kuwa ni mfano hai, anasema mwanamke ambaye hajaolewa na mwanaume ambaye hajao wakikutana kwenye majukwaa ya kisiasa kila mmoja anagombea, mwanamke ataonekana hafai.

“Huyu mwanamke atapewa majina mengi na maneno ya udhalilishaji wakati yule mwanaume jamii itamuona ni mpambanaji, hali hii inavunja moyo na kuwarudisha wanawake wengi wenye uwezo nyuma kujitosa kugombea.

Saumu anasema japo changamoto za kisiasa kwa wanawake nchini zinapungua, bado jamii inapaswa kubadilika na kuwa na mapokeo chanya pale mwanamke anapogombea nafasi mbalimbali za uongozi. “Japo kwa kiasi fulani imebadilika, viongozi wa juu wa vyama vya kisiasa wanawake wapo kwa wingi, kuna tija, vilevile wanawake walioopo madaraka wanaofanya vizuri, kumewatia moyo wengine na kuona inawezekana,” anasema.

Saumu anasema pia amsha amsha ya wanaharakati katika kupaza sauti, imekuwa ni chachu ya mabadiliko na kuonyesha wanawake wanaweza.

“Hivi sasa kuna wagombea Urais wanawake, haya ni matunda ya mikutano ya Beijing, wanawake tumepambana kutafuta usawa, japo si kwa asilimia mia moja, lakini matunda yanaonekana,” anasema. Saumu anasema bado kuna changamoto ya kuaminika kwa wanawake na kuingia kwenye nafasi za juu akitolea mfano majimboni.

“Mfano utakuta kwenye jimbo kuna mgombea mwanamke na mwanaume, kutokana na itikadi na mifumo yetu, huo labda wanaona akigombea mwanamke hana rasilimali ya kutosha au anaweza asishinde, hivyo kwa fikra hizo wanamuengua,” anasema.

Anasema wapo wanawake pia ni waoga kutokana na mfumo dume uliokuwepo, hivyo hata akiambiwa agombee, yeye mwenyewe anajiona hatoshi wakati uwezo huo tunaomtizama tunauona ndani yake. “Kikubwa ni kuendelea dumisha utulivu na kuonyesha uthubutu ili kuwachochea wanawake wengi kuingia kwenye siasa, zinapotokea changamoto ndogo ndogo wanawake wengi wanarudi nyuma,” anasema.

Simulizi ya Mwakagenda

Katika mahojiano na Mwananchi yaliyofanyika hivi karibuni, Mwakagenda mbunge mwakilishi wanawake mkoa wa Mbeya anasema wanawake wa Tanzania wanaponzwa na mfumo dume. Akijitolea mfano yeye, anasema alipojitosa kwenye siasa, wapo waliomdhihaki na kusema asichaguliwe. “Walitumia lugha ngumu, walisema Msimchague Mwakagenda ana nyonyo moja! Kwa kuwa Nami nilikuwa jasiri, sikuyumbishwa na maneno yao, niliwauliza kwani huko Bungeni nakwenda kunyonyesha?. “Tunapaswa tushindane kwa hoja na sera, sio kwa maneno ya kum-attack mtu, yote hiyo ni kwa sababu ya mfumo dume, japo kadri siku zinavyosonga unakwenda unabadilika. “Unabadilishwa na sisi wanawake tuliopo kwenye siasa na wale waliotutangulia ambao walifanya vizuri na kuthibitisha uwezo na nguvu ya mwanamke akipata nafasi,” anasema.

Mwakagenda anasema alipogombe jimbo la Rungwe mwaka 2020, alionywa kwamba haijawahi kutokea jimbo hilo likawa na mgombea mwanamke. “Nilisema naweza, nilipambana na wanaume saba kwenye kura za maoni nikawashinda, nikasimama kuiwakilisha Chadema kwenye uchaguzi mkuu na kupata kura elfu 37. “

Anasema mgombea mwanamke ukijiwakilisha kwa hoja, achilia mbali mfumo dume uliopo, watu watakuamini na kukuchagua.

“Watu wanaishi kwa kuona, wakiona mbunge au diwani unawajibika, watakuamini, ishu ni je unajenga hoja? hapa sio 50 kwa 50 bali quality. “Wapo wanawake wanauwezo wa kusimama na kujenga hoja kwa jamii, wanaume hawafui dafu,” anasema.

Wanawake na uongozi

Akizungumzia uongozi, Mwakagenda anasema kwa miongo zaidi ya mitatu wanawake walikuwa wakipambana kutafuta uongozi.

“Baada ya muda sasa tuna viongozi tena wajuu katika ngazi za uamuzi, wanatuwakilisha vizuri na hata waliopita wametuwakilisha vizuri, Bungeni tulianza na Anne Makinda, sasa Dk Tulia Ackson ni Rais wa IPU.

“Zanzibar sasa ina Katibu mkuu kiongozi mwanamke (Zena Said) anafanya vizuri, tuna Rais mwanamke, alikuwa ni makamu wa Rais, aliaminika na amefanya vizuri

“Tunajua nchi za Kiafrika nyingi zina mifumo dume, lakini kwa walichokifanya viongozi wanawake hadi sasa, hao wanaume watasema alipita mwanamke fulani, alifanya moja mbili tatu, tunaamini uongozi ni taasisi, anayesimamia akiwa imara anaiendeleza taasisi,” anasema.

Dorothy Semu wa ACT afunguka

Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu anasema maneno ya ubaguzi kwa wanawake yapo, japo hayapaswi kuwarudisha nyuma. “Unapoingika kutaka mamlaka, maana yake ni kutaka kuongoza watu kwa kubadilisha maisha yao iwe kwa uzuri au kwa ubaya.

“Ukiingia kwenye sasa uwe tayari kukubaliana na changamoto zote na kuamua lipi ulichukue na lipi uachane nalo, na namna unavyoweza kusimama jukwaani usidhalilishwe,” amesema. Anasema imezoeleka katika majukwaa ya kisiasa, akijitokeza mwanaume watu wanampokea na kumsikiliza, lakini ikitokea ni mwanamke atapigiwa miluzi na vitu kama hivyo. Ninachoweza kuwasisitiza wanawake wenzangu, ikitokea hali hiyo, waitumie kama fursa wasirudi nyuma kwa kuwa mwanamke ukisimama kwenye majukwaa ya kisiasa unaangaliwa Macho matatu. Hata ikitokea umesimama jukwaani, anza kutafuta kueleweka kwa jamii, kupokea kila neno, liwe zuri lichukue na baya achana nalo huku ukijua haitakuwa rahisi, jifunze kujikaza na kukabiliana na changamoto,” anasema.

Semu hakutofautiana na watangulizi wake naye akieleza kuwepo kwa tofauti kubwa kwenye siasa ya zamani kwa wanawake na sasa.

“Mikutano ya Beijing na namna kazi inavyofanyika kwa wanawake waliopewa fursa, inadhihirisha tunaweza,” amesema.

Anasema matamanio ya wanawake wengi ni kutaka kuona idadi ya ikiongezeka kwenye nafasi za uamuzi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading