Mwabukusi aenguliwa kugombea urais TLS

Mwabukusi aenguliwa kugombea urais TLS

Dar es Salaam. Ikiwa imebaki siku moja kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Kamati ya rufaa za uchaguzi ya chama hicho, imemuengua wakili Boniface Mwabukusi kugombea urais, ikisema ana doa la kimaadili kinyume na kanuni za uchaguzi huo.

Katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Agosti mwaka huu, Mwabukusi alikuwa miongoni mwa wagombea sita waliopitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo.

Wengine ni pamoja na Ibrahim bendera (Ilala), Emmanuel Muga, (Ilala), Revocatus Kuuli (Mzizima), Paul Kaunda (Kanda ya Magharibu) na Sweetbert Nkuba (Kinondoni).

Mwabukusi aliyejipatia sifa kwa kupinga mkataba wa uwekezaji na uendelezaji wa bandari kati ya Serikali ya Dubai na ya Tanzania, alifikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Mawakili na Mwanasheria Mkuu wa Serikali akimlalamikia kwa kukiuka maadili ya uwakili.

Baada ya shauri lake kusikilizwa, hatimaye alikutwa na hatia na kupewa onyo Mei mwaka huu.

Akizungumza na Mwananchi leo Julai 5, 2024, Mwabukusi amesema rufaa yake ilisikilizwa kwa njia ya mtadao na kuambiwa na kamati hiyo kuwa amepoteza sifa ya kugombea.

“Nimejulishwa jioni hii, kwa sababu rufaa imeendeshwa kwa mtandao kwamba inabidi nienguliwe kwa masilahi ya Taifa,” amesema Mwabukusi.

Hata hivyo, amesema hajaridhishwa na uamuzi huo na ataeleza hatua zaidi atakazochukua.

Mwananchi imezungumza na Katibu wa Kamati ya uchaguzi ya TLS, Nelson Frank na kumuuliza sababu ya wakili huyo kuenguliwa.

“Tangazo la chama cha wanasheria GN 598 la mwaka 2022 kanuni ya 13c, zinataka miongoni mwa mambo mengine, mgombea anayegombea nafasi ya urais asiwe na doa lolote la kimaadili.

“Kuna hukumu ambayo ipo ambayo Mwabukusui alitiwa hatiani na haijawahi kutenguliwa na chombo chochote kwa hiyo bado ipo. Kwa hiyo Kamati ya Rufaa ya uchaguzi ya TS ikaona kwamba ana doa la kimaadili kwa hiyuo hajakidhi vigezo vya kugombea urais,” amesema.

Alipoulizwa sababu ya Kamati ya Uchaguzi kumpitisha wakili huyo kama alikuwa na maadili, Frank amesema uchaguzi ni mchakato.

“TLS huwa kuna Kamati ya Uchaguzi halafu kuna Kamati ya Rufaa ya uchaguzi, hivyo ni vyombo viwili tofauti. Awali kamati ya uchaguzi katika mchakato ule, wao waliona kwa namna moja au nyingine amekidhi vigezo wakamwona anafaa kugombea urais, lakini kuna chombo cha juu ya ile kamati, kwa hiyo ilipofika kwenye ngazi ya juu zaidi ambayo ni kamati ya rufaa za uchaguzi ya TLS, ikaona kwamba kwa mantiki kwamba kuna hukumu ambayo ipo na alitiwa hatiani kwa sababu ya maadili wakaona ana doa,” amesema.

Bila kumtaja aliyekata rufaa, Frank amesema mpaka kamati imefikia hapo, kuna watu ambao hawakuridhika wamekata rufaa.

Amesema rufaa hizo ni mchakato wa ndani wa chama na sasa hatua inayofuata ni kampeni. “Kama mtu hajaridhika na uamuzi ndani ya chama basi atachukua hatua nyingine nje ya chama.”

Alipoulizwa sababu ya rufaa yake kuamuliwa siku ya mwisho, amesema huo ni mchakato ambao kama mtu hataridhishwa na mchakato wa chini, Kamati ya rufaa hukata rufaa na ndio yenye uamuzi wa mwisho.

“Kanuni zinaeleza kuwa, msiende kwenye hatua nyingine kabla ya kumaliza na kutoa uamuzi kwenye hatua ya nyuma. Kwa mfano, kama kulikuwa na rufaa, ni lazima zisikilizwe na ziamuliwe kabla ya kwenda kwenye kampeni.

“Ndio maana umeona Juni 24, 2024 Kamati ya Uchaguzi ilisema hawa wanafaa kugombea kwenye chama, lakini kuna wale ambao hawakuridhishwa, wakakata rufaa kwenye kamati ya rufaa, kwa hiyo leo ilikuwa ni lazima maamuzi yatolewe, kwa mfano mpaka leo kulikuwa na rufaa saba imebidi zisikilizwe, kwa sababu ndio sheria inavyoeleza kwamba uamuzi utoke kabla ya kampeni,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Zanzibar Commerce
Top News
Investment News Editor

Zanzibar Airports Authority enforces Dnata monopoly

. Airlines that have not joined the Zanzibar Airports Authority’s (ZAA) preferred ground handler, Dnata, at the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA) face eviction from the Terminal Three building Dnata is the sole ground handler authorised to provide services for flights that operate at Terminal 3.Continue Reading