Muswada Sheria ya Fedha watenga asilimia mbili Bima ya Afya kwa Wote

Muswada Sheria ya Fedha watenga asilimia mbili Bima ya Afya kwa Wote

Dodoma. Serikali ya Tanzania imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Fedha kwa mwaka 2024 ambao unapendekeza asilimia mbili ya mapato yanayotokana na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji laini, vileo na vipodozi ziwekwe katika Mfuko wa Bima wa Afya kwa Wote (UHC).

Muswada huo umewasomwa mara kwanza bungeni leo Alhamisi, Juni 20, 2024, unapendekeza marekebisho kwenye Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote, ambapo kifungu cha 25(3) kinapendekezwa kurekebishwa ili kuainisha kiwango cha ushuru wa bidhaa ambacho kitapelekwa katika Mfuko wa Bima ya Afya kwa Wote.

“Aidha, inapendekezwa kiasi cha asilimia mbili kinachotokana na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji laini, vileo na vipodozi kiwekwe katika mfuko huo,” amesema Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba katika maelezo ya muswada huo.

Amesema asilimia 100 ya ushuru wa bidhaa unaotokana na dau la kamari pia utatumika kama chanzo cha mapato ya UHC.

Sakata la sukari

Muswada huo, unapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Tasnia ya Sukari, ambapo kifungu kipya cha 14A kinapendekezwa kuongezwa kwa lengo la kuiwezesha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kuingiza ndani ya nchi, kuhifadhi na kusambaza sukati kwa matumizi ya ndani ya nchi wakati wa upungufu.

“Lengo la hatua hii ni kuwezesha upatikanaji wa sukari nchini na kuondoa uhodhi kwa baadhi ya wenye viwanda bila kuathiri dhamira ya Serikali ya kulinda viwanda vya ndani,” amesema Dk Mwigulu.

Pia, Muswada huo unapendekeza marekebisho katika Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta, Sura ya 220, ambapo kifungu cha 3 kinarekebishwa kwa kuiandika upya tafsiri ya msamiati “nishati” ili kujumisha gesi asilia katika tafsiri hiyo.

Aidha, vifungu vya 4, 4A na Jedwali la Pili vinarekebishwa ili kutoza ushuru wa Sh382 kwa kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari na mapato yatakayotokana na ushuru huo yatapelekwa katika Mfuko wa Barabara.

Dk Mwigulu amesema lengo la marekebisho haya ni kuongeza mapato yatakayotumika katika kufanya matengenezo ya barabara pamoja na kuleta usawa kwa kuwa magari yanayotumia mafuta tayari yanachangia mapato kwa ajili ya matengenezo ya miundombinu ya barabara.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading