Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameruhusu mikutano ya hadhara iiliyokuwa ikililiwa kwa muda mrefu na vyama vya upinzani kutaka ruhusiwe.
Leo Jumanne, Januari 3, 2023 Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesema; “uwepo wangu leo hapa mahali nimekuja kufanya ruhusa ya mikutano hii, nimekuja kutangaza kuondoa zuio la kuzuia mikutano ya hadhara na ninasema kwamba, sasa linaondoka.”
Rais Samia amesema mikutano hiyo kisheria, ni haki haki kwa vyama vya siasa kuiendesha huku akisema kwa upande wa Serikali wamejipanga kutekeleza wajibu wao wa kulinda mikutano hiyo.
Ili kuendelea na mikutano hiyo, Rais Samia amesema jukumu sasa linabaki kwa vyama vya siasa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola kama sheria na kanuni zinavyoelekeza ili vipatiwe ulinzi.
Rais amesema hatua waliyoifikia katika mazungumzo baina ya vyama hivyo na Serikali kwa sasa, mikutano hiyo haitazuiliwa tena.
“Ruhusa ya mikutano ya kisiasa itatolewa, wajibu wetu sisi Serikali ni kuwalinda mfanye mikutano yenu salama mmalize vizuri, kufuata kanuni ndio wajibu wenu vyama vya siasa,” amesema.
Ikumbukwe kuwa hatua hiyo ya Rais Samia inakuja ikiwa ni takribani mwezi mmoja umepita tangu akabidhiwa ripoti ya kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi, ambapo katika ripoti hiyo, viongozi wa vyama vya siasa waliweka bayana hitaji namba moja kuwa ni mikutano ya hadhara ambayo ilizuiliwa.
Akiwasilisha mapendekezo ya kikosi kazi mwezi uliopita kwa Rais Samia, Mwenyekiti wa Kikosi Kazi hicho, Profesa Rwekaza Mukandala alisema kuwa kilipendekeza mikutano ya hadhara iruhusiwe kufanyika kwa mujibu wa katiba na sheria.
“Yafanyike marekebisho ya sheria ili kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika kwa ufanisi, sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258, Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma Saidizi Sura 322, Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa za mwaka 2019,” alisema Profesa Mukandala.
Leo akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa, Rais Samia amesema atazungumza na vyombo vya dola ili kuhakikisha suala hilo linatekelezwa kwa ufanisi.
“Ni haki kwa vyama vya siasa kuendesha mikutano ya hadhara lakini ndugu zangu tuna wajibu. Kwa upande wa serikali tumeshajipa wajibu wetu kuwa ni kulinda mikutano ya vyama vya siasa, wajibu wenu vyama vya siasa ni kutupa taarifa kama sheria na kanuni zinavyosema kisha vyombo vinatoa ruhusa,” amesema
“Wakiona kuna hatari hawatoi ruhusa kwa hatua tuliyofika ruhusa za kufanya mikutano zitatolewa kwa sababu wajibu wetu ni kuwalinda mfanye mikutano kwa usalama, mmalize vizuri muondoke vizuri.”
Pia, amesema, “mimi siwaiti nyie vyama vya upinzani, vyama vya kuwaonyesha changamoto zilipo, mnapinga nini, mnampinga nani, ndani ya Tanzania tunapingana kwei, tunaonyeshana changamoto ziko wapi, kasoro ziko wapi na mkinionyesha nikiwa msikivu nikazitekeleza nitaongeza imani kwa wananchi.”
Rais Samia ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM amesema; “mazungumzo baina ya Serikali na vyama vya siasa bado yanaendelea, kuna mambo mengi ambayo itabidi tuitane, tuzungumze, tushauriwe, tukubali, tukatae kwa hoja lakini hivyo mazungumzo na maridhiano bado yanaendelea.”
“Mimi imani yangu, vyama vya siasa tutaendelea kukaa tuzungumze mambo yanayohisu nchi yetu,” amesema
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.
In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.
The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.
“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.
Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.
Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.
Source: allafrica.com
Zanzibar’s tourism body chairman Rahim Bhaloo resigns
Bhaloo, who is also Chairman of the Zanzibar Commission for Tourism (ZCT), cited pressing family issues as the reason for his departure.Continue Reading
Zanzibar liquor importers face fresh hurdle despite court order
The liquor shortage in Zanzibar is far from over, even after a court order granted relief to the three importers.Continue Reading