Mikakati yaandaliwa, tumbaku ikishika namba mbili mauzo ya bidhaa asili nje

Mikakati yaandaliwa, tumbaku ikishika namba mbili mauzo ya bidhaa asili nje

Dar es Salaam. Tumbaku ikishika nafasi ya pili katika mauzo ya bidhaa za asili nje ya nchi mwaka 2023, wadau wanashauri itafutwe njia mbadala ya kukausha zao hilo hasa kwa wakulima wadogo ili kuepusha ukataji miti unaoweza kuligharimu Taifa.

Hata hivyo, Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) katika mazungumzo na Mwananchi imesema tayari kuna aina mbili za mbegu zinazotumia hewa na jua kukauka zimeanza kutumiwa na wakulima katika baadhi ya mikoa.

Ripoti ya Takwimu za Msingi Tanzania 2023 inaeleza kuongezeka uzalishaji wa tumbaku nchini ni moja ya sababu ya mauzo ya nje ya nchi kukua zaidi ya mara mbili,  kati ya mwaka 2021 hadi 2023.

Inaelezwa katika ripoti hiyo kuwa, kukua kwa mauzo kutoka Sh291.4 bilioni mwaka 2021 hadi Sh824.9 bilioni mwaka 2023 kunaifanya tumbaku kushika nafasi ya pili katika mauzo ya bidhaa za asili nje ya nchi na kuleta mapato mengi nchini, ikiipiku korosho ambayo mwaka 2023 ilishika nafasi hiyo.

Ripoti hiyo iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inafafanua kuwa siyo mauzo tu ya zao hilo yaliyoongezeka, bali hata bidhaa zinazotokana na tumbaku nazo uzalishaji wake umeongezeka.

Uchambuzi unaonyesha uzalishaji sigara uliongezeka kutoka sigara bilioni 7.02 mwaka 2021 hadi bilioni 11.86 mwaka 2023.

Ongezeko la uzalishaji sigara unaifanya kuwa bidhaa ya pili miongoni mwa baadhi ya bidhaa zilizotengenezwa viwandani zilizoainishwa na ripoti upande wa Tanzania Bara kati ya mwaka 2019 hadi 2023 ikitanguliwa na bidhaa za  rangi.

Agosti 8, 2024 Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe alimweleza Rais Samia Suluhu Hassan kuwa, kama si mvua za El-Nino, Tanzania ingekuwa mzalishaji mkubwa wa tumbaku duniani kwa kuwa hivi sasa inashika nafasi ya pili ikitanguliwa na Zimbabwe.

“…Umechukua uongozi wa nchi yetu uzalishaji wa tumbaku ukiwa ni tani elfu 65 na malengo yetu kwa sasa ilikuwa ni kuzalisha tani 170,000 hadi tani 200,000 lakini tumefikisha tani 122,000,” alisema Bashe.

Mtaalamu wa Uchumi na Biashara kutoka Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa Aurelia Kamuzora amesema Taifa linapaswa kuangalia namna linavyoweza kutumia zaidi fursa ya uzalishaji na uuzaji tumbaku nje ya nchi ili kujiingizia fedha za kigeni.

Amesema fursa hiyo inaweza kutumika zaidi hasa katika kipindi hiki ambacho baadhi ya nchi duniani zinapunguza uzalishaji kutokana na kampeni zinazofanywa kupiga marufuku matumizi ya sigara katika maeneo yao.

“Sisi tunaweza kuimarisha uzalishaji kwa kufanya utafiti kuangalia sehemu ambazo watu wanaweza kulima zaidi tumbaku na kufanya uzalishaji ili kutumia fursa iliyopo,” amesema.

Kuhusu uzalishaji wa sigara kuongezeka, Profesa Kamuzora amesema athari zake kwa watumiaji ni bayana na huainishwa hata kwenye pakiti, akisema kisanyansi kitu chochote kinapotumiwa kupita kiwango kinaweza kumuathiri mtu.

“Kama mtu unakunywa supu ya nyama yenye mafuta mengi kila siku utaishia kupata tatizo, kila kitu unapotumia kwa wingi kina madhara,” amesema Profesa Kamuzora.

Hata hivyo amesema ni vyema kuangalia kama nikotini inaweza kuwaathiri hadi wakulima, kwa kufanya tafiti katika moja ya mkoa unaozalisha kwa wingi tumbaku na kulinganisha na ule ambao hauzalishi.

Amesema moja ya kitu kinachoweza kuangaliwa ni umri wa mtu kuishi.

Ukataji miti

Ukataji miti kwa ajili ya kupata kuni za kukaushia tumbaku ni suala linalojadiliwa hapa na pale, kwamba kadri uzalishaji unavyoongezeka ndivyo nchi inakuwa kwenye hatari ya kuwa jangwa.

Profesa Kamuzora amependekeza kuwapo mipango ya njia zinazoweza kutumika kukausha zao hilo bila kutumia kuni zinazosababisha ukataji miti.

 “Kuna baadhi ya kampuni niliona zinaotesha miti kwa ajili ya kufidia uharibifu nafikiri tunahitaji kujipanga zaidi kwa kuangalia wapi tunaweza kurekebisha, ikiwemo kupanda miti kwa wingi,” amesema.

Akizungumza na Mwananchi, Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB), Stanley Mnosya amesema njia pekee ya kuzuia ulimaji tumbaku kuathiri mazingira ni kuangalia namna ya kudhibiti ukataji miti.

Amesema kwa sasa wamebadili majiko ya kukaushia tumbaku kwa kuondoa yenye uwezo wa kuingiza magogo na kuweka yanayotumia matawi matawi ya miti pekee.

Amesema wameingia mkataba wa miaka mitatu na moja ya kampuni itakayokuwa ikiwajengea wakulima majiko.

“Lakini ukiacha hili, tuna mbegu mpya aina mbili za tumbaku ambazo zitakuwa hazihitaji moto kukaushia, badala yake zitatumia hewa na mwanga wa jua,” amesema Mnosya.

Amesema mbegu inayokaushwa kwa kutumia hewa huhitaji kivuli, hivyo mkulima atafunika  na nyavu na kuacha sehemu ya kupitisha hewa.

Pia kama mtu ana  miti ya kivuli ana uwezo wa kuweka tumbaku chini yake na ikakauka vizuri.

“Mbegu hizi tayari zimeanza kutumika katika maeneo ya Iringa, Singida na baadhi ya sehemu ya Tabora, lengo letu ni kuona mwaka huu asilimia 30 ya tumbaku yote itokane na mbegu hizi na tutakuwa tukiongeza kidogokidogo hadi zao hili nchi nzima litakapokuwa linatokana na mbegu hizi,” amesema.

Kutokana na baadhi ya tumbaku kuendelea kukaushwa kwa moto amesema kupitia Mfumo wa Usimamizi wa Misitu unaotegemea Jamii (CBFM) wanalinda watu kutoingia kiholela kukata misitu, bali kwa kufuata utaratibu ambao unaenda sambamba na watu kufundishwa namna ya kuvuna misitu.

Amesema kuna kampeni maalumu inayowataka wakulima kupanda miti 500 anapolima hekta moja, huku vikundi vya kinamama na vijana vimeundwa kusimamia na kutunza miti inayopandwa.

Mikakati mingine

Wakati hayo yakifanyika, bajeti ya Wizara ya Kilimo ya mwaka 2024/2025 inataja mkakati katika zao hilo ni kuratibu upatikanaji wa tani 127,316 za mbolea na kusambaza kwa wakulima kwa mpango wa ruzuku.

Hilo litaenda sambamba na usambazaji wa viuatilifu lita 236,329 na pakiti 1,664,286, vifungashio belo 11,709 na nyuzi 166,429 kwa ajili ya kuimarisha uzalishaji wa tumbaku.

Mbolea ya NPK (10:18:24) itaagizwa na Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) na kusambazwa kwa wakulima wa tumbaku.

“Bodi ya Tumbaku Tanzania itajenga mabani ya kisasa 2,353 katika mikoa ya Tabora, Shinyanga, Geita, Kigoma, Ruvuma, Katavi, Mbeya, Songwe, Iringa, Morogoro na Mara. Mabani hayo yatasaidia kupunguza upotevu wa majani, kuongeza ubora wa tumbaku na kutunza mazingira,” imeeleza wizara katika bajeti hiyo.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading