Miaka minne ya Magufuli kaburini, Chato kumkumbuka leo

Miaka minne ya Magufuli kaburini, Chato kumkumbuka leo

Miaka minne ya Magufuli kaburini, Chato kumkumbuka leo

Dar es Salaam. Jumatano ya Machi 17, 2021, Tanzania iligubikwa na wingu zito la kumpoteza Rais aliyekuwa madarakani, Dk John Pombe Magufuli maarufu JPM.

Ni kwa mara ya kwanza Taifa hilo la Afrika Mashariki kushuhudia Rais aliyekuwa madarakani akifariki dunia. Kifo chake kilitangazwa na Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Makamu wa Rais.

Dk Magufuli aliyezaliwa Chato mkoani Geita, Oktoba 29, 1959 alihitimisha utawala wake wa miaka mitano na miezi minne aliouanza Novemba 5, 2015 katika Hospitali ya Mzena, Kijitonyoma jijini Dar es Salaam kwa maradhi ya moyo.

Leo Jumatano ni miaka minne imetimia tangu alipovuta pumzi ya mwisho dunia. Mwili wake, ulizikwa katika makaburi ya familia, nyumbani  kwao Chato, Machi 26, 2021.

Kutokana na kifo chake,  Samia Suluhu Hassan aliyekuwa Makamu wake wa Rais aliapishwa Machi 19, 2021, Ikulu ya Dar es Salaam na Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma kuwa Rais wa Tanzania, hivyo kuwa Rais wa kwanza mwanamke kati ya watano waliomtangulia.

Marais waliopita kwa kuanza na awamu ya kwanza ni Julius Nyerere (1964-1985), Ali Hassan Mwinyi (1985-1995), Benjamin Mkapa (1995-2005), Jakaya Kikwete (2005-2015) na John Magufuli (2015-2021).

Dk Magufuli aliyekuwa na falsafa ya Hapa Kazi Tu, baada ya kuapishwa kwa Samia kuwa Rais akaitambulisha  falsafa yake ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania…Kazi Iendelee.

Akimaanisha kuendelea miradi mbalimbali aliyokuwa ameianzisha mtangulizi wake na kuanzisha mipya.

Miongoni iliyoachwa ni Bwawa la Umeme la Nyerere, Daraja la Tanzanite, Daraja la Kigongo- Busisi, ununuzi wa ndege ili kulifufua Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) na barabara mbalimbali nchini.

Dk Magufuli aliacha watoto na mjane, Janeth Magufuli.

Harakati za kisiasa za Dk Magufuli zilianza mwaka 1995 alipogombea kiti cha ubunge katika jimbo la Chato na baadaye kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi. Mwaka 2000, Magufuli aligombea na kushinda tena ubunge na kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi.

Aidha, katika chaguzi za mwaka 2005 na 2010, aliendelea kuwania kiti hicho cha ubunge katika jimbo la Chato na kushinda na kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi hadi mwaka 2008 alipohamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambayo aliiongoza hadi mwaka 2010. Mwaka 2010 alipochaguliwa tena kuwa mbunge wa Chato aliteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi.

Mwaka 2015, alikuwa miongoni mwa makada zaidi ya 40 wa CCM waliojitosa kuchukua fomu kuwania kumrithi Rais Kikwete aliyekuwa akimaliza muda wake madarakani.

Ni makada 38 pekee ndio walirejesha fomu, wakiwemo mawaziri wakuu wastaafu,  maofisa ngazi za juu za jeshi, mawaziri na makada wa kawaida. Baada ya michakato yote CCM ikampitisha  Magufuli kuwania urais na baadaye akashinda urais wa Tanzania.

Safari yake ya kielimu inaonyesha, Magufuli alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria akianzia Makutupora, Dodoma (Julai – Desemba 1983), kisha akaenda kambi ya Makuyuni, Arusha (Januari hadi Machi 1984) na akamalizia katika kambi ya Mpwapwa mkoani Dodoma (Machi – Juni 1984). Mwaka 1985 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akisomea Shahada ya Sayansi ya Elimu akibobea kwenye masomo ya Kemia na Hisabati na alihitimu mwaka 1988.

Kati ya mwaka 1991 na 1994 alijiunga na masomo ya Shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Chuo Kikuu cha Salford nchini Uingereza na baadaye mwaka 2006-2009 alijiunga na masomo ya Shahada ya Uzamivu ya Kemia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kutokana na taaluma yake Magufuli ameandika vitabu na machapisho mbalimbali.

Leo Jumatano, ndugu, jamaa na marafiki watamkumbuka kwa Ibada itakayofanyikia Chato ambayo imeandaliwa na familia yake.

Endelee kufuatilia Mwananchi kujua kinachoendelea kutoka huko

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading

Zanzibar Commerce
Top News
Investment News Editor

Zanzibar Airports Authority enforces Dnata monopoly

. Airlines that have not joined the Zanzibar Airports Authority’s (ZAA) preferred ground handler, Dnata, at the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA) face eviction from the Terminal Three building Dnata is the sole ground handler authorised to provide services for flights that operate at Terminal 3.Continue Reading