Miaka 10 ya Eyakuze Twaweza: Safari ya milima na mabonde

Miaka 10 ya Eyakuze Twaweza: Safari ya milima na mabonde

Dar es Salaam. Baada ya miaka 10 ya milima na mabonde katika ushawishi wa sera na kusikiliza sauti za wananchi, sasa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza East Africa, Aidan Eyakuze anastaafu.

Eyakuze anayestaafu Machi, 2025 anakwenda kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ubia wa Serikali ya Uwazi (OGP) yenye makao makuu nchini Marekani.

Katika mahojiano maalumu na Mwananchi jana Jumatano Januari 8, 2025 jijini Dar es Salaam, Eyakuze amesema safari yake ya miaka 10 ndani ya Twaweza East Africa imejaa milima na mabonde, akisimamia misingi ya taasisi hiyo ambayo ni uwazi, ushirikishwaji wananchi na uwajibikaji.

Mkurugenzi Mtendaji anayemaliza muda wake katika Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze akizungumza wakati wa mahojiano maalumu na mwandishi wa Mwananchi (Hayupo pichani). Picha na Sunday George

Kazi chini ya uongozi wake

Eyakuze anasema katika kipindi cha uongozi wake wametatua changamoto za wananchi kwa kuwasilisha sauti zao.

 “Kabla sijajiunga na Twaweza walikuwa wameanzisha Mradi wa Sauti za wananchi ambao tunawahoji kuhusu uelewa wa mambo tofauti, masuala ya kiuchumi, kipato na elimu.

“Baada tu ya kuanzisha hilo, Serikali ya Jakaya Kikwete (Rais awamu ya nne) ikapitisha bajeti ambayo ilitaka itoze kodi ya kadi za simu ya Sh1,000,” anasema.

“Tukaenda kwa wananchi tukawahoji, wananchi wakasema hii ina utata, ndipo ikabadilishwa kutoka kwenye kodi ikawa excise duty (ushuru wa bidhaa) kwenye muda wa maongezi, ambayo ikawa na usawa zaidi, haimuumizi mwananchi wa chini au kumpendelea wa juu,” anasema Eyakuze.

Anasema utafiti kama huo waliurejea mwaka 2022 baada ya Serikali ya Awamu ya Sita kuja na tozo ya miamala ya simu.

“Tukaenda tukawauliza wananchi, mnaionaje hii kodi, ilikuwa Agosti, 2022. Serikali na mawaziri wakasikiliza wakaanza kujieleza kwa nini tunafanya kitu hiki, lakini baada ya muda, ilipofika Oktoba, 2022 ikapunguzwa.

“Kwa hiyo, naona ni ishara kwamba, kazi zetu zimepaza sauti za wananchi wa kawaida kabisa wakaishawishi Serikali kubadilisha sera,” anasema.

Katika kipindi chake, Eyakuze ambaye ni mchumi kitaaluma, anasema taasisi ilibuni mfumo wa kuwapa motisha walimu ambao wanafunzi wao wanafaulu katika stadi za msingi kama vile kusoma, kuandika na kuhesabu.

“Tunachokifanya ni kuwapa ahadi walimu wakati shule zinafunguliwa. Awali, tulianza na shule 100 na sasa tumechukua shule 265 kwenye mikoa 10 ambayo ina changamoto lubwa ya elimu, tofauti na mikoa kama Dar es Salaam na Kilimanjaro ambako angalau miundombinu ya elimu msingi haina shida sana.

“Hatuwapi mafunzo, nyezo zaidi, vitendea kazi hapana. Tunawaambia wanafunzi wako wakifaulu katika stadi hizi, utapata motisha hii ambayo ni fedha taslimu,” anasema.

Mbali na hayo, Eyakuze anasema walitafuta maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya Katiba na matokeo yake wameyapeleka kwenye mchakato wa kutengeneza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

“Ndiyo maana ukisoma Dira, msingi wake ni utawala bora, usalama, amani na utulivu, kwa sababu wananchi walisema hayo ni muhimu,” anasema Eyakuze ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Kitaifa ya maandalizi ya dira hiyo.

Eyakuze amewahi kutajwa kuwa miongoni mwa watu 50 wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani waliofanya mapinduzi katika Serikali na Apolitical na World Economic Forum mwaka 2021.

Akielezea hatua hiyo, anasema kutambuliwa huko kulitokana na ubunifu uliofanywa na Twaweza wa kutoa simu kwa wananchi kwa ajili ya kupata maoni yao.

“Tulibuni kitu ambacho kinatumiwa na Benki ya Dunia (WB) na kinatumika kwa nchi nyingine. Wakasema huu ni ubunifu wa taasisi ambao una ushawishi katika nchi nyingine,” anasema.

Kuhusu changamoto

Eyakuze aliyejiunga na Twaweza East Africa mwaka 2015, anasema moja ya changamoto alizokumbana nazo ni mabadiliko ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO) mwaka 2019. 

“Hata hapa, Tanzania tumepitia vikwazo kwa sababu tulikuwa tumejisajili kwa Sheria ya Kampuni ya mwaka 2019 na ikabidi tujisajili kwa Sheria ya Mashirika yasiyo ya kiserikali,” anasema huku akieleza misimamo tofauti ya nchi inavyoyumbisha malengo ya taasisi hiyo.

“Twaweza iko Kenya na Uganda, unaweza kukuta Serikali zinachukua msimamo tofauti kuhusu asasi za kiraia,” anasema.

Kutokana na madiliko ya sheria hizo, Eyakuze anasema asasi za kiraia zinakosa uhuru wa kufanya kazi zake.

Mkurugenzi Mtendaji anayemaliza muda wake katika Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze akizungumza wakati wa mahojiano maalumu na mwandishi wa Mwananchi. Picha na Sunday George

“Ukisema sana mambo au ukifanya kitu kikaonekana hauendi na mwenendo fulani wa wanaoupenda au ukiwa unakaza sauti sana, unaweza kuingiliwa na sheria zinaruhusu.

“Kuna Sheria ya Makosa ya Mtandao, kuna sheria ya NGO na nyinginezo zinazoruhusu Serikali kuingilia au kukudhibiti,” anasema.

Utafiti uliomweka matatani

Anasema mwaka 2018 hadi 2020 ilikuwa yenye changamoto kwake baada ya Idara ya Uhamiaji kumnyang’anya pasi ya kusafiria kutokana na wasiwasi kuhusu uraia wake.

Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya kutoa matokeo ya utafiti ambao pamoja na mambo mengine, ulionyesha kushuka kwa umaarufu wa hayati Rais John Magufuli.

“Kazi yangu inanihitaji nisafiri kwenye ofisi za Kenya na Uganda, kwa hiyo kwa karibu miaka mitatu sikuweza kusafiri nje ya Tanzania. Ikaniwia vigumu kufanya kazi,” anasema.

Anasema mwaka 2020 yalipotangazwa maambukizi ya Uviko-19 yaliyozuia watu wengi kusafiri, alikuwa na uzoefu wa kufanyia kazi mitandaoni.

Katika kipindi hicho anasema mwajiri wake alimuunga mkono.

“Nimekuwa na bodi na wakurugenzi ambao wamenipa ushirikiano kwa asilimia 200 siyo 100 ili kusimamia misingi yetu ambayo ni uwazi, ushiriki na uwajibikaji,” anasema.

Anasema walichukua hatua ya kufungua kesi kudai pasipoti.

“Tulikwenda Mahakama Kuu tukapigwa chini, tukaenda Mahakama ya Rufaa tukasikilizwa, wakafuta uamuzi wa Makama Kuu, ilikuwa Desemba 4, 2020, wakaitaka Serikali irudishe pass (pasipoti) ndani ya siku 60 na siku ya 61 nikapewa,” amesema. 

Baada ya misukosuko, Eyakuze anasema walijadiliana na kuja na mikakati mipya ya kiutendaji iliyopunguza chokochoko kwa Serikali.

“Tukasema tunawezaje kuhakikisha Sauti za wananchi zinasikika bila kuchokoza mkono wa Serikali? Kumbuka tumetoka kwenye sheri ya kampuni tumeletwa kwenye sheria ya NGO,” anasema.

Pia, anasema ni ya Twaweza si kutafuta umaarufu kwa kugombana na Serikali bali kutafuta matokeo ya wananchi.

Fahamu kuhusu OGP

Eyakuze anayekwenda kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi  ya Ubia wa Serikali ya Uwazi (OGP) aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya uendeshaji ya taasisi hiyo.

OGP ni mpango wa kimataifa unaolenga kupata ahadi kutoka kwa Serikali za kitaifa za kukuza uwazi, kupambana na ufisadi na kuboresha utawala. Unasimamiwa na kamati ya uongozi inayojumuisha wawakilishi kutoka serikalini na mashirika ya kiraia.

Ilianzishwa mwaka 2011, Ofisa Mtendaji Mkuu wa kwanza alikuwa Sanjay Pradhan. Eyakuze anakuwa wa pili akiwa wa kwanza kutoka Bara la Afrika.

OGP inahusisha nchini 75 na mamlaka 150 za ndani ambazo zinafanya kazi pamoja na maelfu ya mashirika ya kiraia.

Tanzania iliyojiunga na OGP Septemba 2011, New York nchini Marekani chini ya aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiamo wa Afrika Mashariki, hayati Bernard Membe ilijitoa Julai 2017.

Septemba 20, 2017 aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki alipoulizwa kuhusu sababu ya Tanzania kujiondoa OGP aliahidi kuwa Serikali ingetoa ufafanuzi muda utakapowadia.

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Aziz Mlima alikiri Tanzania kujiondoa katika mpango huo.

“Ndiyo ni kweli lakini ni kwa muda tu kwa sababu Serikali inataka kuutathimini mpango huo kama unaendana na masilahi ya Taifa. Kuna mambo tunahitaji kwanza kuyatekeleza kabla ya kutekeleza mpango huu,” anasema

“OGP inailazimu Serikali mwanachama, kila baada ya miaka miwili kutoa taarifa ya mipango na ahadi za mabadiliko yatakayofanywa na kuhakikisha kuna uwajibikaji,” anasema Eyakuze.

Eyakuze pia amewahi kuwa mjumbe wa bodi za Taasisi ya Ushirikiano wa Kimataifa kwa Ajili ya Takwimu za Maendeleo Endelevu (GPSDD) na Taasisi ya Ushirikiano kuhusu Uwazi wa Mikataba (OCP).

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading