MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

SWAHILI News Exclusive: Na Mwandishi Wetu

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mgao wa maji katika Mitaa mbalimbali ya Unguja huku baadhi ya Mitaa ikikosa kabisa huduma hiyo na kusababisha ugumu wa maisha kwa wananchi ambao wanalazimika ama kununua maji kwenye magari na wengine kwenye visima vya watu binafsi.

“Kama unavyoona watu wanahangaika na madumu ya maji, hapa mtaani petu hatupati kabisa maji ya ZAWA, hatuelewi tatizo hili litakwisha lakini tunateseka na maji” Alilalamika Ali Yussuf Mkaazi wa Sogea Mjini Unguja.

Maeneo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao ni urithi wa Kimataifa unaotambuliwa na Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na kwenye hoteli kadhaa za Kitali, huduma ya maji safi na salama ni ya kubahatisha.

“Hapa Hotelini sisi tunanunua maji kila siku, hatupati kabisa maji ya ZAWA… kwa kweli ni mzigo mzito kwetu gharama zimekuwa kubwa a uendeshaji” Alisema Meneja mmoja wa Hoteli ya kitalii yenye hadhi ya nyota tano ambae hakupenda kutaja jina lake.

Habari zaidi kutoka ZAWA zinasema kwamba wakati wananchi wakikosa huduma ya maji na wengine wakipata maji kwa mgao wa muda mrefu, kumekuwa na kutoelewana miongoni mwa wafanyakazi na uongozi wakiulalamikia uongozi wa Taasisi hiyo kutojali maslahi yao, uwezo wao kufikia ukingoni pamoja na masuala ya itikadi za kisiasa.

Inadaiwa kwamba makundi yaliyopo katika ZAWA ni miongoni mwa sababu zinazozorotesha utendaji kazi pamoja na ukosefu wa weledi katika usimamizi wa masuala ya maji. “Hapa kuna makundi, hatuko kitu kimoja, mkurugenzi ana kikundi chake fulani ndicho anachokiamini” Alisikika Fundi Mmoja akisema.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nishati na Madini, Mwanajuma Majid Abdullah amewaomba wananchi kuendelea kustahamili wakati Serikali ikishughulikia tatizo la ukosefu wa maji katika maeneo yao mbalimbali kupitia miradi ya maji inayotekelezwa na ZAWA.

“Nafahumu kwamba tatizo la maji halistahamiliki, lakini nawaomba wananchi kuendelea kupokea huduma ya maji kwa mgao kwani sio muda mrefu tatizo la maji litamalizika Zanzibar” Naibu Katibu Mkuu Mwanajuma Majid alieleza Kamati ya Ardhi, Mawasiliano na Nishati ya Baraza la Wawakilishi.

Naibu Katibu Mkuu huyo alisema tatizo la maji Zanzibar limetokana na uwepo wa visima vichache ambavyo vinatumika pamoja na uchakavu wa miondombinu ya maji.

Mkurugunzi Mkuu wa ZAWA Mhandisi Dkt Salha Mohammed Kassim alitaja ukosefu wa wataalam ni miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili Mamkala hiyo kwa sasa na kuiomba Serikali kutoa umuhimu katika kuajiri wafanyakazi wenye ujuzi kwani hata ikikamilika kwa miradi ya maji bado kutakuwa na changamoto kwa kukosekana kwa wataalam.

Haikuweza kufahamika mara moja ni kiasi gani cha fedha kilichotumika kutoka katika fedha za Uviko 19 zilizotolewa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuipatia SMZ pamoja na fedha za Exim Bank ya India ambapo fedha hizo zimepangwa kutumika katika ujenzi wa matangi, ulazaji wa mabomba ,uchimbaji wa visima.

MWISHO.

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year’s Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading