SWAHILI News Exclusive: Na Mwandishi Wetu
Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mgao wa maji katika Mitaa mbalimbali ya Unguja huku baadhi ya Mitaa ikikosa kabisa huduma hiyo na kusababisha ugumu wa maisha kwa wananchi ambao wanalazimika ama kununua maji kwenye magari na wengine kwenye visima vya watu binafsi.
“Kama unavyoona watu wanahangaika na madumu ya maji, hapa mtaani petu hatupati kabisa maji ya ZAWA, hatuelewi tatizo hili litakwisha lakini tunateseka na maji” Alilalamika Ali Yussuf Mkaazi wa Sogea Mjini Unguja.
Maeneo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar ambao ni urithi wa Kimataifa unaotambuliwa na Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na kwenye hoteli kadhaa za Kitali, huduma ya maji safi na salama ni ya kubahatisha.
“Hapa Hotelini sisi tunanunua maji kila siku, hatupati kabisa maji ya ZAWA… kwa kweli ni mzigo mzito kwetu gharama zimekuwa kubwa a uendeshaji” Alisema Meneja mmoja wa Hoteli ya kitalii yenye hadhi ya nyota tano ambae hakupenda kutaja jina lake.
Habari zaidi kutoka ZAWA zinasema kwamba wakati wananchi wakikosa huduma ya maji na wengine wakipata maji kwa mgao wa muda mrefu, kumekuwa na kutoelewana miongoni mwa wafanyakazi na uongozi wakiulalamikia uongozi wa Taasisi hiyo kutojali maslahi yao, uwezo wao kufikia ukingoni pamoja na masuala ya itikadi za kisiasa.
Inadaiwa kwamba makundi yaliyopo katika ZAWA ni miongoni mwa sababu zinazozorotesha utendaji kazi pamoja na ukosefu wa weledi katika usimamizi wa masuala ya maji. “Hapa kuna makundi, hatuko kitu kimoja, mkurugenzi ana kikundi chake fulani ndicho anachokiamini” Alisikika Fundi Mmoja akisema.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nishati na Madini, Mwanajuma Majid Abdullah amewaomba wananchi kuendelea kustahamili wakati Serikali ikishughulikia tatizo la ukosefu wa maji katika maeneo yao mbalimbali kupitia miradi ya maji inayotekelezwa na ZAWA.
“Nafahumu kwamba tatizo la maji halistahamiliki, lakini nawaomba wananchi kuendelea kupokea huduma ya maji kwa mgao kwani sio muda mrefu tatizo la maji litamalizika Zanzibar” Naibu Katibu Mkuu Mwanajuma Majid alieleza Kamati ya Ardhi, Mawasiliano na Nishati ya Baraza la Wawakilishi.
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema tatizo la maji Zanzibar limetokana na uwepo wa visima vichache ambavyo vinatumika pamoja na uchakavu wa miondombinu ya maji.
Mkurugunzi Mkuu wa ZAWA Mhandisi Dkt Salha Mohammed Kassim alitaja ukosefu wa wataalam ni miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili Mamkala hiyo kwa sasa na kuiomba Serikali kutoa umuhimu katika kuajiri wafanyakazi wenye ujuzi kwani hata ikikamilika kwa miradi ya maji bado kutakuwa na changamoto kwa kukosekana kwa wataalam.
Haikuweza kufahamika mara moja ni kiasi gani cha fedha kilichotumika kutoka katika fedha za Uviko 19 zilizotolewa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuipatia SMZ pamoja na fedha za Exim Bank ya India ambapo fedha hizo zimepangwa kutumika katika ujenzi wa matangi, ulazaji wa mabomba ,uchimbaji wa visima.
MWISHO.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI
Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading
For years, a UK mining giant was untouchable in Zambia for pollution until a former miner’s son took them on
For years, the people in the villages around Chingola in Zambia endured frequent health challenges and dead fish floating around in their water source, but that was just the beginning of their nightmare.Continue Reading
Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.
In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.
The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.
“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.
Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.
Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.
Source: allafrica.com