Mfumko Wa Waongeza Ugumu Wa Maisha Zanzibar Tanzania

Mfumko Wa Waongeza Ugumu Wa Maisha Zanzibar Tanzania

Read Story in English

MFUMKO WA BEI WAONGEZA UGUMU WA MAISHA ZANZIBAR & PEMBA ISLAND, TANZANIA

Mfumuko wa bei za bidhaa muhimu Zanzibar sasa unawaumiza wananchi wanyonge.

Mchele wa Mbeya daraja la kwanza unauzwa kg shilingi 3800 wakati Daraja la pili ukiuzwa kwa kg 1 shilingi 3500, daraja la tatu unauzwa kwa kilo 3000 huku daraja la mwisho kabisa Kg 1 shilingi 2800.

Bei hizo ni katika masoko ya Mwanakwerekwe C, Soko la Mombasa na katika maduka mengi ya Mjini na Mashamba.

Bei ya maharage aina ya soya Kg 1 ni shilingi 3500, maharage mengine Kg 1 ni shilingi 3200.

Kwa upande wa bei ya sukari nayo imepanda na kufikia Kg 1 ni kati ya shilingi 2400 hadi shilingi 2600 kutegemea na aina ya sukari.

Zanzibar: Kg 1 ni kati ya shilingi 2400 hadi shilingi 2600 kutegemea na aina ya sukari

” Hali imekuwa ngumu, kila kitu bei juu, vitu havinunuliki mchele wa Mbeya hauliki” Alilalamika Hamad Faki Jabu Mkaazi wa Darajabovu aliyekuwa akinunua bidhaa Soko la Mwanakwerekwe C.

Ukitembelea katika sehemu mbalimbali madukani, bei ya mchele aina ya Mapembe nao umepanda kutoka Kg 1 shilingi 1500 hadi Kg 1 shilingi 1800.

Unga wa ngano kwa sasa Kg 1 ni shilingi 2000. Wakati Mkate wa Boflo kipenzi cha Wazanzibari wengi unauzwa kwa shilingi 250 kutoka bei ya awali ya shilingi 200.

Katika mikahawa kadhaa ya Unguja na Pemba, bei ya chapati imefikia shilingi 700.


Kwa upande wa Mafuta ya kupikia nusu lita ilikuwa shilingi 1000 bei ya sasa ni shilingi 2000

Bei ya chipsi kavu nusu sahani ni shilingi 2000 ambaoo bei ya awali ilikuwa ikiuzwa shilingi 1500.

Bei ya chipsi zege sasa imefikia shilingi 3000 kutoka shilingi 2500.

Zanzibar: Bei ya chipsi zege sasa imefikia shilingi 3000 kutoka shilingi 2500

Tanzania inalenga mfumuko wa bei kubaki kati ya asilimia tatu hadi tano lakini kamati hiyo ilisema bei ya juu ya vyakula, nishati na mbolea katika soko la dunia inahatarisha kupanda kwa mfumuko wa bei siku zijazo.

Baadhi ya bidhaa za vyakula ambazo bei zimepanda hivi karibuni ni pamoja na unga wa ngano. Hii ni kutokana na ukweli kwamba wazalishaji wa Tanzania wengi wao huagiza nafaka ya ngano kutoka nchi za Urusi na Ukraine ambayo mauzo ya nje yalitatizwa na vita kati ya nchi hizo mbili.

Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya sera na utafiti wa umaskini ya Repoa, Dk Donald Mmari alielezea mfumuko wa bei wa sasa kama wa kimuundo, akimaanisha kuwa unasababishwa na usumbufu wa usambazaji uliosababishwa na Covid-19 na vita vya hivi majuzi vya Urusi na Ukraine.

“Usumbufu huu umeongeza mahitaji na hivyo kuongeza bei,” alisema Dk Mmari ambaye kitaaluma ni mchumi.

Alisema uhaba wa mvua nchini Tanzania katika msimu uliopita pia unaongeza uhaba wa chakula, hivyo kupandisha bei.

“Sera ya fedha ni hatua ya muda mfupi lakini katika muda wa kati tunahitaji kuhakikisha usambazaji wa bidhaa kama vile nafaka ya ngano na mafuta ya kula yanazalishwa vya kutosha nchini,” alisema.

Bei ya petroli pia imekuwa ikiongezeka tangu kuanza kwa vita vya Urusi na Ukraine mapema mwaka huu. Kwa mfano, bei ya petroli iliongezeka kutoka Sh2,480 kwa lita Februari 2022 hadi Sh3,410 mwezi huu wa Agosti, kulingana na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura).

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year’s Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading