‘Sasa ni vigumu kubishana dhidi ya Messi kuwa mchezaji bora wa soka’
Lionel Messi alitembea peke yake kwenye mwangaza mmoja huku kukiwa na giza kwenye Uwanja wa Lusail na hatimaye kutwaa tuzo hiyo ambayo ameitafuta kwa maumivu makali katika maisha yake ya soka.
Mchezaji huyu nyota wa Argentina mwenye umri wa miaka 35 alisugua mikono yake pamoja akitarajia utukufu wake wa taji, akivaa vazi la kitamaduni la Kiarabu linalojulikana kama bisht, kabla ya kuinua Kombe la Dunia angani huku kukiwa na mlipuko ya mwangaza.
Messi alikuwa amefikia ndoto yake. Pengo katika mkusanyiko wake wa tuzo lilikuwa limezibwa baada ya fainali ya Kombe la Dunia ya kuvutia zaidi katika historia.
Sasa anaweza kuongeza Kombe la Dunia kwenye Ballons d’Or saba, Ligi za Mabingwa nne, Copa America moja, mataji 10 ya La Liga akiwa na Barcelona na taji la Ligue 1 huko Ufaransa akiwa na Paris St-Germain.
Hili ndilo kombe ambalo mamilioni ya mashabiki wa Messi sasa watatumia kama mfano katika hoja yao kwamba yeye ndiye bora zaidi kuwai kucheza mchezo huo.
Hili ni taji, karibu inchi 15 za dhahabu safi, ambalo sasa litawafanya wengi kusema Messi ndiye bora zaidi – na wale walio na mabishano ya kupinga watakuwa na ugumu wa kutetea madai yao.
Ulinganisho unapanuliwa kwa vizazi vingi, jambo ambalo linaongeza sura tofauti kwa mabishano yote, lakini hakuna anayeweza kukataa kuwa Messi ni wa kiwango moja na Pele na ambaye picha yake ilikuwa kwenye mabango mengi ya Argentina kwenye Uwanja wa Lusail siku ya Jumapili.
Bila shaka, Diego Maradona, mtangulizi wake maarufu katika jezi namba 10 ya Argentina, alikuwa na fyrsa kubwa ya kuwa mchezaji bora. Tofauti ilikuwa siku zote ni ushindi wake wa Kombe la Dunia huko Mexico miaka 36 iliyopita – ushindi ambao Messi hakuwa nao. Sasa hilo limeondolewa.
Messi daima atakuwa katika mjadala wowote kuhusu mchezaji bora zaidi, na ukweli kwamba sasa ana heshima kubwa zaidi ambayo mchezo wa kimataifa unapaswa kutoa na kuufanya mjadala wenye nguvu zaidi kuhusu sifa zake.
Unaanzaje kusimulia hadithi ya jinsi Messi alivyofikia kilele chake? Je, unasimuliaje matukio ambayo hatimaye yalipelekea Argentina kushinda Kombe la Dunia na kilele cha mashindano ambayo yatakuwa na jina la Lionel Messi milele?
Messi alipaswa kujua, kwa kuzingatia historia yake ya huzuni ya Kombe la Dunia na kukatishwa tamaa iliyoanzia 2006 na ikiwa ni pamoja na kupoteza fainali dhidi ya Ujerumani huko Rio’s Maracana mnamo 2014, kwamba hii ilikuwa heshima ambayo haingeweza kushindwa kwa urahisi.
Ukweli kwamba usiku huu wa kuvutia kwenye Uwanja wa Lusail ulikuwa na mateso mengi kwa Argentina na Messi kufikia kilele cha ushindi wao wa tatu wa Kombe la Dunia huenda ukaufanya uwe mtamu zaidi.
Na yote yalifanyika mbele ya kipaji kutoka kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ambaye, kama hajafikia hapo tayari, ataungana na Messi katika mjadala wowote kuhusu nyota wa kweli wa mchezo huo katika miaka ijayo: Mfaransa Kylian Mbappe.
Ufaransa ilionekana kutandaza zulia jekundu kwa kutawazwa kwa Messi huku wakitishia kwa dakika 80. Lusail alikuwa uwanja wa michezo wa Messi alipoifungia Argentina bao la kwanza kwa mkwaju wa penalti, na kumfanya kuwa mchezaji wa kwanza katika historia ya Kombe la Dunia kufunga katika hatua ya makundi, hatua ya 16 bora, robo fainali, nusu fainali na fainali katika mchuano mmoja.
Messi kisha akasaidia kuandaa bao la pili la Angel di Maria, sherehe zilianza miongoni mwa mashabiki wa Argentina hadi pambano lililokuwa likitarajiwa na Mbappe lilipobadilika kwa mtindo wa kustaajabisha.
Mbappe alifunga zikiwa zimesalia dakika 10, kisha akapiga shuti kali sekunde chache baadaye. Tabasamu la Messi kwenye skrini kubwa katika kila kona ya uwanja lilikuwa la kutoamini “sio tena”.
Messi, bila shaka, aliivusha Argentina kwa bao lake la pili katika muda wa nyongeza lakini Ufaransa, walisawazisha tena kwa mkwaju wa penalti wa Mbappe.
Katika mazingira ya mshangao, kipa wa Argentina Emiliano Martinez aliokoa kwa mguu wake kutoka kwa Randal Kolo Muani na Kombe la Dunia likiwa mikononi mwake katika sekunde za mwisho, ingawa bado kulikuwa na wakati kwa Lautaro Martinez kufunga kwa kichwa kwa goli ambalo lilikuwa wazi.
Kusema kwamba muda wa ziada ulikuwa wenye kasi ya juu haitakuwa sawa, huku baadhi ya mashabiki hata wakificha macho yao wakati huo, huo ulikuwa mvutano usiovumilika.
Ilikuwa na mafadhaiko makubwa, ilienda kwenye mikwaju ya penalti ambayo Argentina ilishinda 4-2, njia chungu ya kusuluhisha mchezo ambao sasa utazungumzwa kila Kombe la Dunia litakapojadiliwa.
Wakati Gonzalo Montiel alipofunga kiki hilo la maamuzi, Messi alipiga magoti huku akitokwa na machozi katikati ya duara, mikono iliyoinuliwa kuelekea mbinguni kabla ya kuzikwa chini ya mashati yenye mistari ya rangi ya samawati na nyeupe.
Kisha aliomba kipaza sauti kuhutubia wafuasi wa Argentina huku kukiwa na sherehe na shangwe
Messi alitwaa Mpira wa Dhahabu kwa mchezaji bora wa michuano hiyo, mchezaji wa kwanza kushinda mara mbili tangu ilipoanzishwa mwaka 1982, baada ya kushinda tuzo hiyo mwaka 2014.
Sasa amehusika katika mabao 21 ya Argentina kwenye Kombe la Dunia – mabao 13 na ya kusaidia nane, idadi kubwa zaidi ya mchezaji yeyote kwa taifa lolote. Mabao katika fainali hii ya Kombe la Dunia yanampa mabao 793 katika maisha yake ya soka. Pia alikuwa mchezaji wa kwanza kufunga katika kila raundi katika mashindano yale yale ya Kombe la Dunia la wanaume.
Kulikuwa na takwimu moja ambayo ilikuwa muhimu zaidi ya nyingine zote usiku huu: Messi hatimaye alikuwa mshindi wa Kombe la Dunia .
Alikaa juu ya mchoro nane ambapo alipokea Kombe la Dunia na timu yake, akijivunia ukweli kwamba mwishowe anaweza kujaza nafasi hiyo kwenye kabati lake la kombe. Ilikuwa ni hatua iliyojaa marafiki na familia ya kikosi cha Argentina, nchi yao sasa imerejea kileleni mwa ulimwengu wa soka kwa mara ya kwanza tangu 1986.
Wafuasi wa Argentina walikaa kwenye viti vyao kwa zaidi ya saa moja, wakipitia kitabu cha nyimbo ambacho kimekuwa wimbo wa kampeni yao ya Kombe la Dunia, wakitoa heshima kwa mtu waliyemtegemea. Mwanaume aliyefanisha ndoto zao.
Mshtuko wa kupoteza mechi ya ufunguzi kwa Saudi Arabia ulionekana kuwa wa zamani. Alikuwa ni Messi ambaye aliweka gia ya Kombe la Dunia la Argentina kwa bao zuri dhidi ya Mexico na hakuweza kuzuilika alipolibeba hadi mwisho.
Messi alikuwa na kombe la dhahabu mikononi mwake. Ilikuwa ni dhamira iliyokamilika – dhamira iliyoanzia zaidi ya miaka 16 hadi alipoingia kama mchezaji wa akiba katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Serbia na Montenegro nchini Ujerumani.
Sura ya mwisho ya hadithi ya Messi ya Kombe la Dunia ilikuwa ya kusisimua kutoka ya kwanza hadi ya mwisho dhidi ya Ufaransa, na njama hiyo ikiwa na mabadiliko mengi. Ilitoa mwisho mzuri katika usiku usioweza kusahaulika nchini Qatar.
Share this news
This Year’s Most Read News Stories
New lawsuit as Zanzibar airport controversy continues
Another company joins the list as they file a petition challenging the exclusive rights granted to Dnata by Zanzibar Airports Authority.Continue Reading
Ali Hassan Mwinyi, Former President of Tanzania, Dies at 98
Ali Hassan Mwinyi, a schoolteacher turned politician who led Tanzania as its second post-independence president and helped dismantle the doctrinaire socialism of his predecessor, Julius K. Nyerere, died on Thursday in Dar es Salaam, the country’s former capital. He was 98.Continue Reading
Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.
President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.
“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”
A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.
“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.
WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.
“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”
Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.
“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”
Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.
Sign up for free AllAfrica Newsletters
Get the latest in African news delivered straight to your inbox
In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.
Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.
Source: allafrica.com