Meli iliyozama bandarini Dar TPA yaambulia fidia Sh100 milioni

Meli iliyozama bandarini Dar TPA yaambulia fidia Sh100 milioni

Dar es Salaam. Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imekwama kupata fidia iliyoomba na kuambulia kiduchu kwenye kesi ya meli iliyozama bandarini Dar es Salaam mwaka 1999.

TPA ilifungua kesi dhidi ya Reza Company Limited, ikidai fidia ya fedha ilizodai kuzitumia wakati meli ya kampuni hiyo ilipopinduka, kuzama na kumwaga mafuta yaliyochafua mazingira.

TPA iliomba ilipwe zaidi ya Sh515.4 milioni ikiwa ni fidia ya gharama ilizodai kutumia kuiibua na kuiondoa meli hiyo mahali ilikozama, kusafisha mazingira ya bahari yaliyochafuliwa na mafuta yaliyomwagika na hasara ya kushindwa kuendesha shughuli zake mahali ilipozama.

Kesi hiyo ilisikilizwa upande mmoja wa TPA pasipo kampuni hiyo kufika mahakamani kujitetea.

Hata hivyo, Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imekataa madai ya fedha ambazo TPA inadai kuzitumia ikabakiza hasara ya jumla ya Sh100 milioni.

Katika hukumu ya Mahakama iliyotolewa Aprili 15, 2024, Jaji Awamu Mbagwa amesema TPA imeshindwa kuwasilisha uthibitisho wa gharama hizo, hivyo ilipwe Sh100 milioni za fidia ya hasara ya jumla, kiwango ambacho ni hiyari ya Mahakama kukadiria inachoona kinafaa kwa madhara aliyoyapata mwathirika kwa tukio au jambo alilotendewa na mdaiwa.

“Kwa kuwa mdai ameshindwa kuwasilisha nyaraka hata moja kuthibitisha malipo ya gharama alizodai kuingia au hasara halisi ya kibiashara, ni uamuzi wangu kwamba, ameshindwa kuthibitisha hasara halisi,” amesema Jaji Mbagwa.

Amesema baada ya kutathmini ushahidi wote, kwa kuiibua na kuiondoa meli hiyo ilikozama kuna gharama ambazo TPA iliingia pamoja na usumbufu, japo mamlaka hiyo ilishindwa kuthibitisha kwa uhakika.

Jaji Mbagwa amesema katika hali ya kawaida kitendo cha meli kuziba gati namba 10 na 11 (mahali ilikozama), shughuli za TPA zilivurugika na kwa sababu hizo, ama ilipata usumbufu au ilikosa mapato kwa njia moja au nyingine.

Amesema kisheria hasara ya jumla haihitaji kuwa imeombwa na kuthibitishwa kiuhalisia, bali inaweza kutolewa na Mahakama hata kwa kuzingatia maelezo pekee.

“Kwa kuzingatia ushahidi wa mdai ninampa fidia ya hasara ya kiujumla ya Sh100 milioni,” amesema Jaji Mbagwa.

“Hatimaye kwa uchambuzi huo, ninatoa hukumu na tuzo kwa manufaa ya mdai.  Ninatoa amri kwamba mdaiwa anaamuriwa kumlipa mdai Sh100 milioni zikiwa ni fidia ya hasara ya kiujumla, riba ya asilimia saba ya kiasi hicho kuanzia tarehe ya hukumu hii mpaka tarehe ya kukamilisha malipo yote na atalipa gharama za kesi,” amesema.

Meli hiyo ya M.V. Mytham, ambayo ndiyo chimbuko la kesi, ilizama Machi 4, 1999 ilipokuwa ikipakia mizigo katika gati namba 11.

Kwa mujibu wa hukumu hiyo, baada ya meli kupinduka na kuzama ilisababisha mafuta kumwagika baharini ambayo yalikuwa miongoni mwa bidhaa zilizokuwa zimepakiwa ndani, hivyo kusababisha uharibifu wa mazingira ya bahari katika eneo hilo.

Pia ilizuia gati namba 10 na 11 hali iliyosababisha shughuli katika magati hayo kusimama kwa muda, jambo ambalo liliilazimu TPA kuingia gharama kukabiliana na tatizo hilo.

Baada ya jitihada za pande zote kumaliza suala hilo kwa amani kushindikana, TPA ilichukua hatua za kisheria na kufungua kesi mahakamani dhidi ya kampuni ya Reza.

Katika kesi hiyo ya madai namba 374 ya mwaka 1999, TPA ilidai kupinduka na hatimaye kuzama kwa meli hiyo kulisababishwa na uzembe wa maofisa wa kampuni hiyo, hususan nahodha na ofisa mkuu.

TPA ilibainisha uzembe uliofanywa na viongozi wa meli hiyo kuwa ni kutokuzingatia taratibu za upakiaji makontena melini, kutokuwa na uwezo na maarifa, kushindwa kuchukua tahadhari muhimu, na meli ilikuwa na matundu.

TPA iliomba ilipwe fidia ya Sh515.49 milioni, ikiwa ni gharama ilizoingia kutokana na kuzama kwa meli hiyo bandarini, riba ya asilimia 31 ya kiasi hicho kuanzia Machi 4, 1999 mpaka tarehe ya hukumu.

Ilichanganua kuwa gharama zikitokana na vifaa vilivyohusika katika uvutaji meli, Sh29.76 milioni, gharama za kuondoa na kudhibiti uchafuzi wa mazingira (Sh1.44 milioni), gharama za vifaa na nguvu kazi wakati wa ukarabati meli hiyo katika karakana kuu ya TPA (Sh7.66 milioni).

Nyingine ni gharama za malighafi na nguvu kazi wakati meli ikiwa gatini (Sh1.66 milioni), gharama za kukodi vifaa na kuwahusisha wataalamu kwa ajili ya kuiibua meli hiyo na kuiondoa (Sh94.63 milioni).

TPA ilibainisha gharama nyingine zilikuwa ni hasara ya kukosa mapato (Sh100 milioni), fidia iliyoilipa kwa kampuni yenye mzigo uliozama na meli hiyo (Sh280.2 milioni), pamoja na gharama za kesi.

Miaka 22 baadaye, Mei 5, 2021, TPA iliiondoa mahakamani kesi hiyo kwa kibali cha kuirejesha na Mei 27, 2021 iliifungua upya na kusajiliwa kama kesi ya madai namba 81 ya mwaka 2021. Ilianza kusikilizwa upande mmoja Februari 20, 2024.

TPA iliwakilishwa na mawakili wa Serikali, Erighi Rumisha na Mwantumu Selle.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading