Mapendekezo ya wanazuoni, Zanzibar ikitimiza miaka 60 elimu bila malipo

Mapendekezo ya wanazuoni, Zanzibar ikitimiza miaka 60 elimu bila malipo

Unguja. Wakati Zanzibar ikitimiza miaka 60 ya elimu bila malipo leo Jumatatu, Septemba 23, 2024, wanazuoni na wanataaluma wametoa mapendekezo namna elimu hiyo inavyotakiwa kuboreshwa, ili kuendana na mahitaji ya sasa ya kidunia.

Wamesema bado elimu inayotolewa inamlazimisha mwanafunzi asome kitu gani, badala ya mwanafunzi mwenyewe kuamua anachotaka kusoma, hivyo kuna haja ya kubadilisha mitalaa, isikilize mwanafunzi mahitaji yake.

Hayo yamebainishwa leo wakati wa kongamano la kitaaluma la miaka 60 ya elimu bila malipo lililoandaliwa na Chuo cha Taifa Zanzibar (Suza) na kuwashirikisha wanazuoni, wadau na wataluma wa elimu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Balozi Amina Salum Ali amesema moja ya tunu zilizopatikana kisiwani hapo ni elimu bila malipo, kwani viongozi wengi akiwemo mwenyewe amesoma shahada yake ya uzamivu bure.

Hata hivyo, amesema kwa sasa ipo haja kuangaliwa mahitaji ya msingi na vijana kuandaliwa katika ujuzi na namna wanavyoweza kuajiriwa katika soko la kimataifa badala ya kukaririshwa.

“Elimu iendane na mambo tunayotaka kufanya, leo tuna masuala ya bandari, miundombinu yake inapanuka, tunatakiwa kuwasomesha vijana wetu, tunazungumzia mambo ya akili mnemba, teknolojia kukua kwa hiyo tunatakiwa tujipange kuipeleka elimu yetu katika mfumo huo,” amesema Balozi Amin, ambaye ameshika nyidhifa mbalimbali serikalini zikiwamo za uwaziri.

Amesema elimu inatakiwa kushughulikia masuala ya ujuzi na kuondokana na mambo ya zamani: “Tunataka vijana wote wanaotoka Zanzibar wawe na uwezo wa kushindana na wengine wote duniani, tunashukuru tunapata elimu bure, lakini sasa tuongeze iwe na tija zaidi.”

Kwa upande wake, Mhadhiri mwandamizi Chuo Kikuu Huria, Dk Cosmas Mnyanyi amesema licha ya mipango na sera kuitaja elimu kuwa nzuri, lakini changamoto ipo kwenye mitalaa.

“Nilikuwa naangalia taarifa tofauti ni nzuri, mipango mizuri sera nayo nzuri, lakini kuna shida ya mitalaa rekebishi, bado mtu anasoma alichopangiwa sasa tunatakiwa kubadilika mtu asome kitu anachokipenda.

“Siku moja tufanye study ndogo hata kwenye makundi ya WhatsApp uulize wewe hicho unachokisoma unakipenda? Wengi watakwambia, sikipendi nimelazimika. Mtu atakwambia mimi napenda ngoma, napenda kucheza muziki, lakini havipo. Sasa sisi tunakimbilia za muziki za kizungu, kwani sisi hatuna vya kwetu?” amehoji.

Akizungumzia elimu mjumuisho, mwanazuoni huyo amesema lazima mtu awe na ujuzi kusomesha wenye mahitaji maalumu na wasio na mahitaji, kwa hiyo lazima mitaala iseme mwanafunzi anatakiwa kwenda kufanya nini ndio ajifunze.

Amesema kwa Zanzibar angalau imeongelewa kuhusu watu wenye ulemavu, lakini sasa wanasomaje, ilhali hakuna vifaa na maandalizi maalumu kwa ajili yao.

“Tuulizane watu wazima wanaopata ulemavu wanapata usaidizi gani, hata wale watoto wanasoma shuleni, je anapomaliza mazingira ya nje ya shule yameandaliwa vipi kwa ajili yake, haya yote lazima tuyaone,” amesema.

Naye mstaafu katika utumishi wa umma, Abdulla Mzee Abdulla amesema kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu tangu yalipotokea Mapinduzi mwaka 1964 ambapo Zanzibar ikikuwa na shule moja ya Maandalizi, shule za msingi 62 na sekondari nne jumla ya wanafunzi wakiwa 25,400 lakini kwa sasa kuna wanafunzi zaidi ya 600,000 wakiwa wanapata elimu bila malipo.

Pia amesema lazima elimu ijikite katika mafunzo ya amali, kwani inampa fursa nzuri mwanafunzi ajiajiri au hata akiajiriwa imsaidie kuwa mahiri katika kazi husika.

Katika mabadiliko hayo, Mzee Abdulla amesema lazima pia kada ya ualimu nayo ibadilike, ili kukidhi sifa zinazohitajika hivyo lazima pia kuwapo na maandalizi ya walimu na wawe tayari kubadilika.

“Mwalimu wa maandalizi na msingi sifa ya kwanza itakuwa ni awe amemaliza kidato cha sita na amefaulu daraja la tatu, mwalimu sekondari lazima awe kidato cha sita daraja la kwanza na la pili, tunafanya hivi kuimarisha sifa na heshima ya mwalimu,” amesema.

Amesema walimu wote watapimwa kupitia Tume ya Walimu na ndio itakayotoa kibali kwamba mtu ana sifa za kuwa mwalimu au hana sifa. Sifa nyingine ya mwalimu lazima ajue Kiigereza na Kiswahili na lugha maalumu kwa watu wenye ulemavu.

Naye Makamu Mkuu wa Suza, Profesa Moh’d Makame Haji amesema zaidi ya miaka 400 Zanzibar ilikosa elimu na ilikuwa inatolewa kwa ubaguzi, kwa hiyo uamuzi wa viongozi kutoa elimu bure ulikuwa wa busara na kusaidia watu wake wapate taaluma.

“Uamuzi huu ulileta ukombozi na kuleta uelewa kwa wananchi hata baada ya kuanzisha Chuo Kikuu cha Taifa mwaka 2001 ilikuwa kuondoa changamoto hii. Sasa tunaona namna gani miaka 60 ya elimu bila malipo imeleta tija kubwa katika maendeleo ya Zanzibar,” amesema.

Suza kina shule tisa za fani mbalimbali, ikiwa na programu 60 na kwa sasa kina wanafunzi zaidi ya 7,000 ikilinganishwa na wanafunzi 54 walioanza nao.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta ya elimu kutoka bajeti ya Sh256 bilioni mwaka 2022/23 hadi Sh830 bilioni mwaka 2023/24.

Mdau wa elimu, Said Ali Said amesema ni bora wanaoandaliwa kuwa walimu waanze kusomea fani husika wakiwa kwenye ngazi za awali, hivyo itakuwa rahisi kuwa mahiri katika ufundishaji.

“Mfano, mwanafunzi akitoka kidato che nne asome masomo ya utalii, aende kidato cha sita asome masomo hayo, kadhalika chuo kikuu na akimaliza arejee kusomesha utalii, hapa ndio tutapa matokeo chanya,” amesema.

Zanzibar ilipata Mapinduzi Januari 12, 1964 na elimu bila malipo ilitangazwa na aliyekuwa Rais wa Kwanza, hayati Abeid Aman Karume Septemba 23, 1964.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading