Mapendekezo ya wanazuoni, Zanzibar ikitimiza miaka 60 elimu bila malipo

Mapendekezo ya wanazuoni, Zanzibar ikitimiza miaka 60 elimu bila malipo

Unguja. Wakati Zanzibar ikitimiza miaka 60 ya elimu bila malipo leo Jumatatu, Septemba 23, 2024, wanazuoni na wanataaluma wametoa mapendekezo namna elimu hiyo inavyotakiwa kuboreshwa, ili kuendana na mahitaji ya sasa ya kidunia.

Wamesema bado elimu inayotolewa inamlazimisha mwanafunzi asome kitu gani, badala ya mwanafunzi mwenyewe kuamua anachotaka kusoma, hivyo kuna haja ya kubadilisha mitalaa, isikilize mwanafunzi mahitaji yake.

Hayo yamebainishwa leo wakati wa kongamano la kitaaluma la miaka 60 ya elimu bila malipo lililoandaliwa na Chuo cha Taifa Zanzibar (Suza) na kuwashirikisha wanazuoni, wadau na wataluma wa elimu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Balozi Amina Salum Ali amesema moja ya tunu zilizopatikana kisiwani hapo ni elimu bila malipo, kwani viongozi wengi akiwemo mwenyewe amesoma shahada yake ya uzamivu bure.

Hata hivyo, amesema kwa sasa ipo haja kuangaliwa mahitaji ya msingi na vijana kuandaliwa katika ujuzi na namna wanavyoweza kuajiriwa katika soko la kimataifa badala ya kukaririshwa.

“Elimu iendane na mambo tunayotaka kufanya, leo tuna masuala ya bandari, miundombinu yake inapanuka, tunatakiwa kuwasomesha vijana wetu, tunazungumzia mambo ya akili mnemba, teknolojia kukua kwa hiyo tunatakiwa tujipange kuipeleka elimu yetu katika mfumo huo,” amesema Balozi Amin, ambaye ameshika nyidhifa mbalimbali serikalini zikiwamo za uwaziri.

Amesema elimu inatakiwa kushughulikia masuala ya ujuzi na kuondokana na mambo ya zamani: “Tunataka vijana wote wanaotoka Zanzibar wawe na uwezo wa kushindana na wengine wote duniani, tunashukuru tunapata elimu bure, lakini sasa tuongeze iwe na tija zaidi.”

Kwa upande wake, Mhadhiri mwandamizi Chuo Kikuu Huria, Dk Cosmas Mnyanyi amesema licha ya mipango na sera kuitaja elimu kuwa nzuri, lakini changamoto ipo kwenye mitalaa.

“Nilikuwa naangalia taarifa tofauti ni nzuri, mipango mizuri sera nayo nzuri, lakini kuna shida ya mitalaa rekebishi, bado mtu anasoma alichopangiwa sasa tunatakiwa kubadilika mtu asome kitu anachokipenda.

“Siku moja tufanye study ndogo hata kwenye makundi ya WhatsApp uulize wewe hicho unachokisoma unakipenda? Wengi watakwambia, sikipendi nimelazimika. Mtu atakwambia mimi napenda ngoma, napenda kucheza muziki, lakini havipo. Sasa sisi tunakimbilia za muziki za kizungu, kwani sisi hatuna vya kwetu?” amehoji.

Akizungumzia elimu mjumuisho, mwanazuoni huyo amesema lazima mtu awe na ujuzi kusomesha wenye mahitaji maalumu na wasio na mahitaji, kwa hiyo lazima mitaala iseme mwanafunzi anatakiwa kwenda kufanya nini ndio ajifunze.

Amesema kwa Zanzibar angalau imeongelewa kuhusu watu wenye ulemavu, lakini sasa wanasomaje, ilhali hakuna vifaa na maandalizi maalumu kwa ajili yao.

“Tuulizane watu wazima wanaopata ulemavu wanapata usaidizi gani, hata wale watoto wanasoma shuleni, je anapomaliza mazingira ya nje ya shule yameandaliwa vipi kwa ajili yake, haya yote lazima tuyaone,” amesema.

Naye mstaafu katika utumishi wa umma, Abdulla Mzee Abdulla amesema kuna mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu tangu yalipotokea Mapinduzi mwaka 1964 ambapo Zanzibar ikikuwa na shule moja ya Maandalizi, shule za msingi 62 na sekondari nne jumla ya wanafunzi wakiwa 25,400 lakini kwa sasa kuna wanafunzi zaidi ya 600,000 wakiwa wanapata elimu bila malipo.

Pia amesema lazima elimu ijikite katika mafunzo ya amali, kwani inampa fursa nzuri mwanafunzi ajiajiri au hata akiajiriwa imsaidie kuwa mahiri katika kazi husika.

Katika mabadiliko hayo, Mzee Abdulla amesema lazima pia kada ya ualimu nayo ibadilike, ili kukidhi sifa zinazohitajika hivyo lazima pia kuwapo na maandalizi ya walimu na wawe tayari kubadilika.

“Mwalimu wa maandalizi na msingi sifa ya kwanza itakuwa ni awe amemaliza kidato cha sita na amefaulu daraja la tatu, mwalimu sekondari lazima awe kidato cha sita daraja la kwanza na la pili, tunafanya hivi kuimarisha sifa na heshima ya mwalimu,” amesema.

Amesema walimu wote watapimwa kupitia Tume ya Walimu na ndio itakayotoa kibali kwamba mtu ana sifa za kuwa mwalimu au hana sifa. Sifa nyingine ya mwalimu lazima ajue Kiigereza na Kiswahili na lugha maalumu kwa watu wenye ulemavu.

Naye Makamu Mkuu wa Suza, Profesa Moh’d Makame Haji amesema zaidi ya miaka 400 Zanzibar ilikosa elimu na ilikuwa inatolewa kwa ubaguzi, kwa hiyo uamuzi wa viongozi kutoa elimu bure ulikuwa wa busara na kusaidia watu wake wapate taaluma.

“Uamuzi huu ulileta ukombozi na kuleta uelewa kwa wananchi hata baada ya kuanzisha Chuo Kikuu cha Taifa mwaka 2001 ilikuwa kuondoa changamoto hii. Sasa tunaona namna gani miaka 60 ya elimu bila malipo imeleta tija kubwa katika maendeleo ya Zanzibar,” amesema.

Suza kina shule tisa za fani mbalimbali, ikiwa na programu 60 na kwa sasa kina wanafunzi zaidi ya 7,000 ikilinganishwa na wanafunzi 54 walioanza nao.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Lela Muhamed Mussa amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika sekta ya elimu kutoka bajeti ya Sh256 bilioni mwaka 2022/23 hadi Sh830 bilioni mwaka 2023/24.

Mdau wa elimu, Said Ali Said amesema ni bora wanaoandaliwa kuwa walimu waanze kusomea fani husika wakiwa kwenye ngazi za awali, hivyo itakuwa rahisi kuwa mahiri katika ufundishaji.

“Mfano, mwanafunzi akitoka kidato che nne asome masomo ya utalii, aende kidato cha sita asome masomo hayo, kadhalika chuo kikuu na akimaliza arejee kusomesha utalii, hapa ndio tutapa matokeo chanya,” amesema.

Zanzibar ilipata Mapinduzi Januari 12, 1964 na elimu bila malipo ilitangazwa na aliyekuwa Rais wa Kwanza, hayati Abeid Aman Karume Septemba 23, 1964.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading