Mambo matatu kuchochea uwekezaji Zanzibar

Mambo matatu kuchochea uwekezaji Zanzibar

Unguja. Wakati Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (Zipa) ikisajili miradi mipya ya uwekezaji 353 yenye thamani ya Dola za 5.5 bilioni za Marekani (Sh14.99 trilioni), uwepo wa amani na kuimarika kwa miundombinu ya kiuchumi na huduma za kijamii vinatajwa kuvutia mitaji mikubwa ya uwekezaji kutoka nje.

Miradi hiyo iliyosajiliwa kwa kipindi cha miaka mitatu ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Nane, inatarajiwa kutoa ajira 20,000. Mingi kati ya miradi hiyo ni ya sekta ya utalii.

Akizungumza leo Septemba 21, 2024 wakati wa kuzindua Hoteli ya Shukran Palace, Michanvi mkoani Kusini Unguja, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amesema uwepo wa miradi mikubwa umechangiwa zaidi na amani na usalama uliopo Zanzibar, pamoja na sera nzuri.

“Uwepo wa amani na usalama katika nchi yetu umekuwa chachu kwa wawekezaji wengi wa kigeni kuona visiwa vyetu vya Unguja na Pemba ndiyo sehemu sahihi ya kuwekeza mitaji yao,” amesema.

Dk Mwinyi amewataka wananchi kudumisha amani na kuendelea kuiunga mkono Serikali ili uwekezaji huo katika miradi ya maendeleo uwe na tija katika kuimarisha uchumi wa Taifa.

Ameipongeza sekta binafsi nchini kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali katika nyanja za maendeleo ikiwemo sekta ya biashara na uwekezaji.

“Serikali inatambua mchango unaotolewa na sekta binafsi katika kusaidia maendeleo ya nchi yetu,” amesema.

Dk Mwinyi amesema wanaendelea kwa kasi kutekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa Bandari ya Mangapwani ambayo itajumuisha shughuli za bandari ya uvuvi, uhifadhi wa mafuta na gesi, viwanda vya kusindika mazao na ujenzi wa mji wa kisasa.

Mbali ya hayo, amesema Serikali inaendelea kuimarisha na kujenga miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege, kuimarisha upatikanaji wa huduma za nishati, majisafi na salama, elimu bora, afya na huduma nyingine za kijamii.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Shariff Ali Shariff amesema sekta ya uwekezaji imekuwa na mchango mkubwa katika kutekeleza falsafa na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2050 yenye lengo la kukuza uchumi, kuzalisha ajira na kupunguza umasikini kwa Wazanzibari.

“Katika kuthibitisha hili ndiyo mafaniko hayo ambayo yametajwa na tunaendelea kuyashuhudia,” amesema.

Amesema miradi 16 ya uwekezaji yenye mtaji wenye thamani ya Dola 377.5 milioni (Sh1 trilioni) imesajiliwa kwa ajili ya uwekezaji katika visiwa vidogo.

“Maono ya uwekezaji katika visiwa vidogo-vidogo yameanza kuzaa matunda, hatimaye mradi wa kwanza katika uwekezaji wa visiwa umekamilika katika Kisiwa cha Bawe, Unguja wenye thamani ya Dola milioni 38 (Sh100 bilioni). Tunategemea kuuzindua rasmi muda wowote kuanzia hivi sasa,” amesema.

Eneo lingine lenye mafanikio amesema ni kuifungua Pemba kama eneo la kimkakati la uwekezaji.

Amesema mfumo wa kisheria ulibadilishwa kushajihisha uwekezaji katika kisiwa hicho uliombatana na utoaji wa vivutio maalumu kwa wawekezaji.

Katika kuhakikisha uwekezaji unaokuja nchini una tija ya moja kwa moja kwa wananchi, amesema wizara inafanya utafiti wenye lengo la kutathmini ajira zilizozalishwa katika miradi ya uwekezaji na kutambua athari zake katika uchumi.

Mkurugenzi wa Mamlaka za Kukuza Uwekezaji Zanzibar (Zipa), Saleh Saada Mohamed amesema mradi wa hoteli hiyo ni miongoni mwa miradi ya hoteli zenye hadhi ya nyota tano katika Mkoa wa Kusini Unguja, ikiwa na majengo 10 yenye jumla ya vyumba 100. Mradi huo umeshatoa ajira rasmi 245 kwa wenyeji.

Mkoa wa Kusini ndiyo unaongoza kupokea uwekezaji mwingi wa sekta ya hoteli.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

ZAA to audit ground handlers
Popular
Investment News Editor

Zanzibar Airport Authority to audit ground handlers

Unguja. The Zanzibar Airports Authority (ZAA) is set to conduct an audit on ground handling companies that currently operate at the Abeid Amani Karume Airport with effect from Monday. The week-long audit is set to include Transworld, ZAT and the newcomer Dnata Zanzibar who were licensed in June plus exclusive rights to manage Terminal 3 building by ZAA.Continue Reading

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading