Majaliwa awapa ujumbe viongozi wa dini

Majaliwa awapa ujumbe viongozi wa dini

Manyara. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewasihi viongozi wa dini nchini waendelee kukemea vikali vitendo vyote ambavyo ni kinyume na maadili ya dini na utamaduni wa Mtanzania.

Majaliwa ametoa rai hiyo leo Jumapili Machi 9, 2025 alipomwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kuwekwa wakfu na kutawazwa kwa Askofu wa Pili wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Kiteto, Askofu Bethuel Mlula iliyofanyika Kanisa Kuu la Anglikana la Mtakatifu Mikaeli, Kiteto mkoani Manyara.

“Ninawaomba viongozi wetu wa dini tuendelee kuliweka suala la kuimarisha malezi na kidhibiti mmomonyoko wa maadili kuwa ajenda ya kudumu. Lazima tuwe na maadili mema ili Taifa liwe endelevu,” amesema.

Aidha, Majaliwa amesema pamoja na masuala ya kiroho amewaomba viongozi wa dini waendelee kuwahamasisha waumini kuunga mkono ajenda mbalimbali za kitaifa, ikiwamo ya uhifadhi wa mazingira, kampeni ya nishati safi na upandaji miti pamoja na kushiriki katika hatua zote za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amempongeza Askofu wa kwanza mstaafu wa kanisa hilo Askofu Isaiah Chambala kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi cha uongozi wake, pia ametumia fursa hiyo kumhakikishia ushirikiano wa kutosha kwa masilahi mapana ya Wana-Kiteto na Watanzania kwa jumla.

“Nitumie nafasi hii kuwahakikishia viongozi wetu wa dini kwamba Serikali ipo pamoja nanyi, tutaendelea kuwa na vikao vya pamoja na sisi tunathamini sana namna ambavyo mmejitoa kuiunga mkono Serikali hii”

Kwa upande wake, Askofu Mlula ameipongeza Serikali kwa jitihada kubwa zinazofanyika ili kuwaletea Watanzania maendeleo katika sekta mbalimbali nchini ikiwamo ya afya na elimu.

Aidha, Askofu Mlula ameipongeza Serikali kwa kusimamia amani umoja na utulivu iliyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.

New Content Item (1)
New Content Item (1)

 “Amani ni tunu ambayo Mwenyezi Mungu ametupatia, tuitumie amani hii kujiletea maendeleo,”amesema.

Naye, Askofu wa Tanga na Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Maimbo Mndolwa ametoa wito kwa wakazi wa Kiteto kwenda kuhakiki majina yao katika daftari la kudumu la wapiga kura ili waweze kushiriki uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani.

“Haki ya jina kuwepo kwenye daftari ni yako ila unaweza kuipoteza usipoitumia vizuri, tushiriki katika michakato iliyoandaliwa na Serikali.”

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Insecurity prompts Zanzibar to review its lucrative island leasing

The Tanzanian central government is planning to boost its security presence in the Zanzibar archipelago. A commission tasked with auditing the country’s security forces was appointed in July by President Samia Suluhu Hassan. It says it is concerned about the situation in the country’s Indian Ocean islands that are under the control of the semi-autonomous Zanzibar local government.Continue Reading

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’
Top News
Chief Editor

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Monrovia — The Rwanda Minister of State responsible for Health, Dr. Yvan Butera, cautioned that while the country is beginning to see positive signals in its fight against the Marburg virus, the outbreak is “not yet over”. He, however, expressed hope that  “we are headed in that direction”. The minister said the epidemiology trend, since the disease was first discovered in the country more than a month ago, is moving towards fewer cases.

Dr. Butera, who was giving updates during an online briefing yesterday, said in the past two weeks, only two deaths were recorded while 14 people recovered from the disease. He said Rwanda was expanding its testing capacity with 16,000 people already inoculated against the disease.

The priority right now, Butera said, is “rapid testing and detection”.

Marburg is a highly virulent disease transmitted through human-to-human contact or contact with an infected animal. The fatality rate of cases, which has varied over the period, is more than 50%, according to the World Health Organization.  WHO said the highest number of new confirmed cases in Rwanda were reported in the first two weeks of the outbreak. There’s been a “sharp decline” in the last few weeks, with the country now tackling over 60 cases.

At Thursday’s briefing, a senior official of the Africa Centers for Disease Control, Dr. Ngashi Ngongo, said mpox – the other infectious disease outbreak that countries in the region are fighting – was been reported in 19 countries, with Mauritius being the latest country to confirm a case. He said although no new cases have been recorded in recent weeks in several countries where outbreaks occurred previously –  including Cameroon, South Africa, Guinea, and Gabon – Uganda confirmed its first Mpox death. This, he said, is one of two fatalities reported outside Central Africa.

Dr. Ngashi revealed that there was an increase in cases in Liberia and Uganda. He said mpox cases were still on an upward trend.

“The situation is not yet under control.”

Source: allafrica.com

Continue Reading