Magonjwa nyemelezi yanavyowatesa vijana wenye VVU

Magonjwa nyemelezi yanavyowatesa vijana wenye VVU

Magonjwa nyemelezi yanavyowatesa vijana wenye VVU

Dar es Salaam. Wakati dunia ikiadhimisha siku ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele leo Januari 30, 2025 nchini Tanzania, hali ya waviu wasiotambua hali zao mpaka kufikia hatua ya kupata magonjwa nyemelezi (Ukimwi) bado ipo huku vijana wakitajwa kuathirika zaidi.

Magonjwa nyemelezi yanayosababishwa na virusi vya Ukimwi (VVU) hatua ya juu kitaalamu yakitambulika kama Advanced HIV Diseases au AHD, hivi karibuni yameingizwa katika orodha ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), mviu atahesabika amepata AHD ikiwa kiwango cha kinga mwili au CD4 kitashuka mpaka chini ya 200 inayoitwa hatua ya tatu au ya nne ya ugonjwa, ikijumuisha wanaokuja kupata matibabu kwa mara ya kwanza wakiwa hawajaanza matibabu ya kufubaza makali ya VVU (ARV) na wale wanaorejea kwenye matibabu baada ya kukatisha tiba.

Wakati changamoto hiyo ikitajwa, imani za dini, tabia ya kujitibu na imani za kishirikina vimetajwa kuwa chanzo kwa vijana wengi kutofika mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa uchunguzi, huku wengi wakifikishwa na wazazi, ndugu wakiwa na dalili za Ukimwi.

Simulizi za wahanga

Ni zaidi ya mshtuko! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya wazazi wa Johari Johnson (si jina lake halisi) kuelezwa na daktari kuwa binti yao alikuwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU).

“Sikuamini. Nilimpigia mume wangu akaja hosptali na wakati huo sikujua nitamweleza vipi anielewe, binti yangu wakati huo alibainika pia na kifua kikuu (TB),” anaanza kusimulia mama wa Johari ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Mama wa Johari amesema hili lilikuwa jaribio pekee, ili yeye na mumewe wapewe upya majibu mbele ya mtaalamu wa afya.

Johari (20) alibainika kuwa na maambukizi ya VVU baada ya kuugua kifua kwa muda za miezi miwili huku uzito wake ukizidi kupungua.

“Mwanangu alikua msiri sana, lakini alipofikia hatua ya kurudi nyumbani na kuacha masomo hali yake ilikuwa imedhoofu sana, nilihisi ni kifua pekee lakini baada ya vipimo zaidi tuliambiwa CD4 zake zimeshuka sana na hivyo alianza kutibiwa kifua kikuu na kuanzishiwa dawa.

“Alikuwa na afya nzuri kilo zake zilikuwa 64 wakati wote. Lakini aliporudi nyumbani wakati ule nakumbuka alikuwa amefikisha kilo 49,” amesema.

Johari anasema hakuwahi kudhani kama ana maambukizi ya VVU na alipoanza kuumwa miezi sita nyuma kabla ya kuzidiwa alikuwa akijitibu kwa dawa za famasi kabla ya kuamua kwenda hospitali.

“Nilianza kupata vipele vidogo vidogo nikahisi losheni niliyoitumia. Nilipewa vipodozi vingine lakini hali haikutulia. Nikahisi mabadiliko ya mwili.

“Baadaye nikaanza kuona sina hamu ya kula, na ghafla nikaanza kupungua uzito. Nilidhani sababu sipendi kula lakini kama unavyojua vyuoni nikajikuta sasa napendelea vyakula vile ninavyoona ninaweza kula.

“Nilikuwa na kilo 63 mpaka 64 lakini ilifika hatua mpaka nguo zilianza kunivuka. Wengi walidhani hali yangu ilitokana na kusoma sana lakini haikuwa hivyo, nikaanza kupata wasiwasi. Miezi michache baadaye nilianza kukohoa kifua kisichopona hata nilipoenda kupata tiba famasi. Ilibidi niende hospitali nako walinipa dawa za kunywa antibaotiki,” anasimulia.

Johari anasema hakupata nafuu na alianza kukohoa mfululizo mpaka miezi miwili, hali hiyo ilimfanya niamue kurudi nyumbani kwa ajili ya matibabu.

Kisa cha Johari, kinaungwa mkono na Mratibu wa Kitengo cha huduma za tiba na matunzo ya Ukimwi CTC katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Amana, Dk Joshua Kajula anayesema changamoto hiyo huwakuta baadhi ya vijana.

Amesema mwaka 2023 mpaka 2025 wagonjwa wote kwa ujumla walikuwa 390 ambao walianza huduma waliokutwa na Advanced HIV Disease walikuwa 170 watu wazima na watoto ambao ni chini ya miaka 24  walikuwa 42 na ambao walikuwa na ugonjwa huo ni 12.

“Kwanza wengi wanakuwa wamejipima na kugundua hali zao kiakili, wengi wanaogopa majibu. Anaumwa lakini kwenda kupima anaogopa, hivyo anajikuta anakwenda kwa namna mbili.

“Wwingine atapita kwenye kila aina ya waganga, hataanzia hospitali anaenda kwa waganga wa kienyeji anatibiwa famasi kwa kununua dawa na wengine wanakwenda kwenye imani za kidini huko kwa manabii mbalimbali.

“Wanapoona imeshindikana na wengi unakuta hajaja mwenyewe ameletwa na ndugu,  wamekuja naye  akifika hospitali hajiwezi kwahiyo ndiyo tunaanza kumtibu na kuona namna ya kupandisha CD4 zake,” amesema Dk Kajula.

Kwa upande wa watoto amesema wanawatambua mpaka miaka 24 kuanzia mwaka sifuri, huku akisema wengi wamepata maambukizi ukubwani na wengine wamezaliwa nao kutoka kwa wazazi.

Amesema baadhi ya watoto wazazi wengine wameshindwa kuwaambia watoto hali zao za kiafya hivyo wakifariki mtoto hapati tiba na hivyo kupata magonjwa nyemelezi.

“Wengine baba, mama wamefariki wapo kwa bibi na babu, kwahiyo bibi hasa ndiyo anakabaki na watoto hawana muda wa kuwapa huduma, hivyo akija anakuja na hali mbaya.

Mtu anakuja na kifua kikuu na wengine wanakuja tayari wana saratani ya ngozi.

“Wiki hii nilimuona mmoja ana saratani ya ngozi kabisa na alienda kupima miaka mingi nyuma,  alipoambiwa amekutwa na virusi vya ukimwi  akakataa akasema yeye hana ni mlokole.

“Akaoa. Anapoenda kuoa wakaenda kupima na mke wake, akakutwa ameambukizwa na mwanamke hana maambukizi. Mwenzake akajua kabisa akamwambia yeye anahangaika na maisha ya ndoa,” amesema.

Dk Kajula amesema mgonjwa huyo amerudi na dalili ya  saratani ya ngozi.

“Nilipomuona moja kwa moja nikawaambia tukampime, wakanidanganya danganya, baadaye tukaenda kuwapima tukakuta tayari ana saratani ya ngozi lakini tukakuta ameathirika na kumpima  mwanamke naye ameshaathirika,” amesema na kuongeza;

“Tukamrudia mwanamke tunamwambia labda tumpe ushauri aanze dawa, naye akasema ‘hapana hakuna shida Yesu atahangaika nayo  situmii chochote, kwa sababu hata mwanzo nilijua naolewa na mwanaume ameathirika, mimi nilisema hii ni ndoa na mimi ndoa yangu nilisema sitatumia na sitatumia’ alitujibu hivyo tukamuacha.”

Dk Kajula amesema huo ni mfano na mviu huyo amegoma kutumia dawa, lakini atakuja kuletwa na ndugu wakati amezidiwa.

Amesema wagonjwa wa aina hiyo huwa wanakutana nao sana, kwa sababu hawana uwezo pia wa kuwalazimisha kuanza dawa, hufikishwa kituo cha afya akiwa katika hatua mbaya.

“Kwa mfano toka mwaka 2023/24 walikuwa 42 lakini kati yao 12 waliokutwa na ugonjwa wa juu wa Ukimwi walikuwa na kifua kikuu TB wengine walikuja wakiwa CD4 ambazo zimefikia hatua mbaya na wengi waliletwa na ndugu lakini tukiwaangalia kwa status za HIV hatua ya juu ya ugonjwa yaani hatua ya nne na tatu,” amesema Dk Kajula.

Hata hivyo Dk Kajula anasema wagonjwa wenye advanced HIV deseases wengi huwa wanakuwa hawako vizuri, kiafya na afya ya akili.

Kwa mujibu wa WHO upimaji wa kiwango cha seli za CD4, ingawa hauhitajiki tena ili kuanzisha matibabu, bado ni nyenzo muhimu kwa kubaini watu walio na AHD.

Watoto wote walio chini ya miaka mitano wanachukuliwa kuwa na AHD kwa sababu ya hatari yao kubwa ya maendeleo ya ugonjwa na vifo.

Watu wenye AHD wako kwenye hatari kubwa ya kifo, hata baada ya kuanza ARV,  hatari hii huongezeka kadri kiwango cha CD4 kinavyopungua.

Sababu za kawaida za magonjwa makali na vifo ni kifua kikuu (TB), maambukizi makali ya bakteria na ugonjwa wa meningitis unaosababishwa na fangasi wa cryptococcus.

Ili kupunguza magonjwa na vifo kwa watu wanaopatikana na AHD, WHO inapendekeza kutoa kifurushi cha afua zikiwemo uchunguzi, matibabu na kinga dhidi ya maambukizi makuu nyemelezi, kuanzisha ART kwa haraka na kuimarisha msaada wa ufuasi wa matibabu. Kifurushi cha AHD kinalenga kupanua upatikanaji wa dawa na vipimo muhimu vya kushughulikia sababu za kawaida za magonjwa na vifo.

WHO ina mwongozo maalum kwa watoto na vijana wenye ugonjwa wa VVU hatua ya juu na kwa usimamizi wa kifua kikuu, ugonjwa wa cryptococcal meningitis, histoplasmosis, na hali za ngozi na mdomo zinazohusiana na VVU.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading