Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Unguja. Wakati mafuta ya petroli na dizelI yakishuka bei, Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kuhakikisha upatikanaji wa huduma hiyo unazidi kuimarika.

Lakini pia imesema inawakaribisha wawekezaji zaidi kuwekeza katika nishati hiyo hususani kisiwani Pemba.

Bei ya petroli imeshuka kutoka Sh2,882 hadi Sh2,775 ikiwa ni tofauti ya Sh107 sawa na asilimia 3.72, huku dizeli ikishuka kutoka Sh3,033 hadi Sh2,892 tofauti ya Sh141 sawa na asilimia 4.65.

Kwa mujibu wa  taarifa ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (Zura), mafuta ya ndege yameshuka bei kutoka Sh2,538 hadi Sh2,414 ikiwa ni tofauti ya Sh124 sawa na asilimia 4.88.

Meneja wa kitengo cha Uhusiano Zura, Mbaraka Haji akizungumza leo Jumatatu Desemba 9, 2024, amesema kupungua kwa nishati hiyo kumetokana kupungua kwa wastani wa bei za mafuta kwenye soko la dunia.

“Pia Serikali imekuwa ikichukua jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupunguza tozo, na kuweka fidia ili kuwapuguzia makali wananchi,” amesema Haji.

Naye Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shaib Hassan Kaduara akizungumza wakati akifungua kituo cha Mafuta cha Puma Unguja mapema leo, amesema katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati nafuu na zenye ubora kisiwani humo, kunahitajika kujengwa vituo vya mafuta ambavyo vitasaidia kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali za kupata nishati safi kwa wote.

“Katika kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa ya nishati nafuu na zenye ubora kisiwani hapa, ni lazima kujengwe vituo vya mafuta kwa lengo la kuwasogezea wananchi hiduma hizi na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali kupata nishati safi kwa wote,” amesema Kaduara.

Pia, amefurahishwa kuona lengo la kampuni hiyo ni kuimarisha huduma zake katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa ya huduma za nishati ikiwemo kisiwani Pemba.

“Nimetaarifiwa kuwa mnafanya tathmini maeneo ambayo hayajafikiwa ikiwemo Kisiwa cha Pemba, ninaomba huduma hizo zianzie Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba, na wengine waige waje kuwekeza upande wa nishati katika ksiwa hicho,” amesema Kaduara.

Amesema Serikali ipo tayari kushirikiana kupeleka huduma hizo kisiwani Pemba, ili wananchi wanufaike kupata huduma za uhakika za nishati.

Vilevile, amesema kampuni hiyo imeonesha uwajibikaji wa huduma za nishati na kuimarisha huduma za kijamii ikiwemo kuajiri wafanyakazi wazawa.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdalla amesema kituo hicho kimegharimu Sh2.5 bilioni hadi kukamilika kwake na kituo hicho ni ishara ya kujizatiti na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Pia, amesema kituo hicho kipya cha huduma ni mwendelezo wa kuisaidia Zanzibar kukidhi mahitaji ya nishati kwa wakazi na wafanyabiashara wake.

“Zanzibar inaendesha shughuli za utalii, uchumi wa buluu, kilimo na usafirishaji wakati sekta hizo zikishamiri mahitaji ya ufumbuzi wa nishati ya kuaminika  yanahitajika,” amesema Fatma.

Amesema ajenda ya kampuni ni kuifanya Zanzibar kuwa suluhisho la nishati kwa kiwango cha kimataifa na kuchangia katika ajira za ndani, na kujiimarisha kuwa mshirika wa kutegemewa katika maendeleo.

Katika kuendeleza utoaji wa huduma, kampuni hiyo imeiomba Serikali iwapatie maeneo ya uwekezaji ya nishati mbalimbali ikiwemo mafuta ya gari na anga.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi  Kampuni hiyo, Dk Majige Selemeni amesema wanatambua kwamba upatikanaji wa huduma za nishati ndio  msingi imara wa maendeleo.

Kituo hicho ni sehemu ya mkakati wa kupanua wigo katika kanda zote kuhakikisha huduma zao zinafikiwa ili kutoa mafuta yenye ubora na salama.

Naye, Bodaboda wa kituo cha Fuoni Melitano, Asaa Shaaban amesema awali ilikuwa wanaenda masafa marefu kupata huduma hiyo ila kwa sasa itakuwa ahueni kwa upande wao.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading

ZAA to audit ground handlers
Popular
Investment News Editor

Zanzibar Airport Authority to audit ground handlers

Unguja. The Zanzibar Airports Authority (ZAA) is set to conduct an audit on ground handling companies that currently operate at the Abeid Amani Karume Airport with effect from Monday. The week-long audit is set to include Transworld, ZAT and the newcomer Dnata Zanzibar who were licensed in June plus exclusive rights to manage Terminal 3 building by ZAA.Continue Reading