Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Mafuta yashuka Zanzibar ikikaribisha uwekezaji zaidi

Unguja. Wakati mafuta ya petroli na dizelI yakishuka bei, Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kuhakikisha upatikanaji wa huduma hiyo unazidi kuimarika.

Lakini pia imesema inawakaribisha wawekezaji zaidi kuwekeza katika nishati hiyo hususani kisiwani Pemba.

Bei ya petroli imeshuka kutoka Sh2,882 hadi Sh2,775 ikiwa ni tofauti ya Sh107 sawa na asilimia 3.72, huku dizeli ikishuka kutoka Sh3,033 hadi Sh2,892 tofauti ya Sh141 sawa na asilimia 4.65.

Kwa mujibu wa  taarifa ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (Zura), mafuta ya ndege yameshuka bei kutoka Sh2,538 hadi Sh2,414 ikiwa ni tofauti ya Sh124 sawa na asilimia 4.88.

Meneja wa kitengo cha Uhusiano Zura, Mbaraka Haji akizungumza leo Jumatatu Desemba 9, 2024, amesema kupungua kwa nishati hiyo kumetokana kupungua kwa wastani wa bei za mafuta kwenye soko la dunia.

“Pia Serikali imekuwa ikichukua jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupunguza tozo, na kuweka fidia ili kuwapuguzia makali wananchi,” amesema Haji.

Naye Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shaib Hassan Kaduara akizungumza wakati akifungua kituo cha Mafuta cha Puma Unguja mapema leo, amesema katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati nafuu na zenye ubora kisiwani humo, kunahitajika kujengwa vituo vya mafuta ambavyo vitasaidia kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali za kupata nishati safi kwa wote.

“Katika kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa ya nishati nafuu na zenye ubora kisiwani hapa, ni lazima kujengwe vituo vya mafuta kwa lengo la kuwasogezea wananchi hiduma hizi na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali kupata nishati safi kwa wote,” amesema Kaduara.

Pia, amefurahishwa kuona lengo la kampuni hiyo ni kuimarisha huduma zake katika maeneo ambayo bado hayajafikiwa ya huduma za nishati ikiwemo kisiwani Pemba.

“Nimetaarifiwa kuwa mnafanya tathmini maeneo ambayo hayajafikiwa ikiwemo Kisiwa cha Pemba, ninaomba huduma hizo zianzie Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba, na wengine waige waje kuwekeza upande wa nishati katika ksiwa hicho,” amesema Kaduara.

Amesema Serikali ipo tayari kushirikiana kupeleka huduma hizo kisiwani Pemba, ili wananchi wanufaike kupata huduma za uhakika za nishati.

Vilevile, amesema kampuni hiyo imeonesha uwajibikaji wa huduma za nishati na kuimarisha huduma za kijamii ikiwemo kuajiri wafanyakazi wazawa.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdalla amesema kituo hicho kimegharimu Sh2.5 bilioni hadi kukamilika kwake na kituo hicho ni ishara ya kujizatiti na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Pia, amesema kituo hicho kipya cha huduma ni mwendelezo wa kuisaidia Zanzibar kukidhi mahitaji ya nishati kwa wakazi na wafanyabiashara wake.

“Zanzibar inaendesha shughuli za utalii, uchumi wa buluu, kilimo na usafirishaji wakati sekta hizo zikishamiri mahitaji ya ufumbuzi wa nishati ya kuaminika  yanahitajika,” amesema Fatma.

Amesema ajenda ya kampuni ni kuifanya Zanzibar kuwa suluhisho la nishati kwa kiwango cha kimataifa na kuchangia katika ajira za ndani, na kujiimarisha kuwa mshirika wa kutegemewa katika maendeleo.

Katika kuendeleza utoaji wa huduma, kampuni hiyo imeiomba Serikali iwapatie maeneo ya uwekezaji ya nishati mbalimbali ikiwemo mafuta ya gari na anga.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi  Kampuni hiyo, Dk Majige Selemeni amesema wanatambua kwamba upatikanaji wa huduma za nishati ndio  msingi imara wa maendeleo.

Kituo hicho ni sehemu ya mkakati wa kupanua wigo katika kanda zote kuhakikisha huduma zao zinafikiwa ili kutoa mafuta yenye ubora na salama.

Naye, Bodaboda wa kituo cha Fuoni Melitano, Asaa Shaaban amesema awali ilikuwa wanaenda masafa marefu kupata huduma hiyo ila kwa sasa itakuwa ahueni kwa upande wao.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading