Madaktari wa wanyama 120 waondolewa sifa

Madaktari wa wanyama 120 waondolewa sifa

Dar es Salaam. Baraza la Veterinari Tanzania (TVA) limewafutia usajili madaktari wa wanyama 120 kwa kushindwa kutimizwa matakwa ya sheria ya baraza hilo.

Uamuzi wa kuwaondolea sifa wataalamu hao umefikiwa na baraza hilo katika kikao chake kilichoketi Desemba 23, 2024.

Taarifa iliyotolewa Desemba 30, 2024 na Baraza la Vetenari, inaeleza kuwa, kwa mamlaka iliyopatiwa kwa kifungu 25 (a), (b)(i)(ii) ya Sheria ya Veterinaria, sura 319, taarifa inatolewa kwa umma ya kuwa usajili wa madaktari wa wanyama 120 umefutwa.

“Baraza la Veterinari Tanzania katika kikao kilichofanyika Desemba 23, 2024 majina ya madaktari hao yameondolewa kwenye rejesta ya madaktari,” inaeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kutoka ofisi ya Msajili wa Baraza la Vetenari madaktari hao hawaruhusiwi kujihusisha na shughuli yoyote inayohusiana na utoaji wa huduma ya afya ya wanyama.

“Majina ya madktari wa wanyama waliofutwa kwenye rejesta yameambatishwa na pia yanapatikana kwenye ya Baraza la Veterinari ambayo ni www.vct.go.tz,” imeandikwa kwenye taarifa hiyo.

Baraza la Vetenari Tanzania limeundwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Veterinari, sura 319 likiwa na jukumu la kusimamia wataalamu wa afya ya wanyama na utolewaji wa huduma ya afya ya wanyama nchini.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

CCM ready to task state organs on Zanzibar Airport deal

Ruling party Chama Cha Mapinduzi-Zanzibar has said it is ready to task state organs to investigate some of the claims against its government that have been raised by opposition politicians on the Abeid Amani Karume International Airport (AAKIA).Continue Reading

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading