Mabadiliko tabianchi yanavyowakimbiza jamii ya wafugaji

Mabadiliko tabianchi yanavyowakimbiza jamii ya wafugaji

Arusha/Manyara. “Tulikuwa na ng’ombe watano na mbuzi 10. Ukame ulipozidi ng’ombe wote walikufa na kubakiwa na mbuzi watano pekee.”
Ni kauli ya Helena Leiyan, mama wa watoto wanne aliyeachwa na mume wake tangu mwaka 2019.

Helena, anayeishi katika Kijiji cha Terrat wilayani Simanjiro, Mkoa wa Manyara anasema hali ya ukame ilipozidi, mume wake aliuza mbuzi waliosalia kisha kutoweka.
“Maisha yalizidi kuwa magumu baada ya baba kuondoka.

Awali alikuwa akifanya kazi za vibarua kwenye mashamba ya watu na shughuli nyingine, lakini haikutosha. Ilibidi aondoke bila kuaga. Hatujui kama yuko hai au amekufa, hajawahi kuwasiliana nasi,” anasema Helena, ambaye watoto wake wana umri wa miaka tisa, 11, 16, na 17.

Helena Leiyan mama wa watoto wanne aliyetelekezwa na mume wake tangu 2019, baada ya maisha kuwa magumu. Kushoto ni mwandishi wa gazeti hili Halili Letea. Picha na Ombeni Daniel

Helena anasema mume wake, Leiyan Nelukendo alipoondoka aliendelea kulea wanawe kwa shida hadi mwaka 2023 hali ilipozidi kuwa ngumu zaidi, akatafuta msaada kwa ndugu wa mume wake.

“Tulikuwa wake wawili, mwenzangu na watoto wake wawili walirudi kwao baada ya mume kuondoka. Nilikaa hadi mwaka jana nilipokuja hapa, walinikaribisha,” anasema.
Helena na watoto wake wanaishi kwa kaka wa mume wake, Isaya Nelukendo.
Watoto wawili walikuwa shuleni wakati huo, ingawa ilikuwa Jumamosi kwa sababu wanajiandaa kwa mtihani wa Taifa.

“Tunashukuru kuwa na mahali pa kuishi, lakini nahitaji kuwa na shamba au mifugo. Mume wangu hakuacha, lakini kama nikipata nitampunguzia mzigo huyu baba,” anaeleza.

Isaya anasema, “Hatujui alipo (Leiyan), niliwahi kusikia yuko Mirerani. Hii ni familia yake (Helena na watoto wake), kwa hivyo ni yangu pia, na nina wajibu wa kuwasaidia.”

Akizungumzia kuhusu kumpatia Helena ardhi au mifugo, Isaya anasema angefanya hivyo kama angekuwa navyo, lakini alichonacho hakitoshi.

“Tutakula tulicho nacho Mungu atakavyojalia. Pia watakaa hapa hadi watakapoweza kujitegemea,” amesema.

Kuondoka kwa wanaume na kuacha familia zao si jambo geni katika maeneo haya. Nilikutana na mama wa makamo aliyejitambulisha kwa jina la Naitapuaki Lukas anayeishi katika Kijiji cha Oloswaki.

Naitapuaki, anayeishi na mume wake mzee anasema: “Tulikuwa na watoto wawili, walipokua waliondoka na hatujui walipo.”

Anaamini wanawe wapo mjini akisema, “Sijui kama wako Mirerani au Dar es Salaam. Hawajawasiliana nasi kabisa tangu walipoondoka.”

Naitapuaki na wanawake wengine sita wanaeleza si kijiji chao pekee, wanaume wameondoka kutoka vijiji jirani pia.
Kuna wanaume ambao licha ya ugumu wa maisha, wameendelea kujihusisha na shughuli nyingine.

Nilikutana na Noah Lukas katika Kijiji cha Oloswaki, anayejishughulisha na kilimo cha umwagiliaji na ufugaji.

“Ufugaji umekuwa mgumu kutokana na kupungua ardhi ya malisho. Ingawa nina mbuzi wachache, lengo langu kuu ni kilimo. Tunashukuru Serikali kuleta maji karibu. Nauza mboga na naweza kusaidia familia yangu,” anasema.

Wamasai mijini

Katika maeneo mengine ya mijini kama vile Dar es Salaam na Zanzibar, kuna watu wa Kabila la Masai wanaojihusisha na biashara ndogondogo, kazi za ulinzi na wengine wanajihusisha na ususi wa nywele.

Katika eneo la Mwenge, Dar es Salaam, nilikutana na Naranda Saling’o, anayefanya biashara ndogo ndogo za kuuza pochi, mikanda, vikatakucha na vitambaa katika maeneo ya jirani.
Licha ya kuishi Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka saba tangu alipoondoka nyumbani kwao Engarenaibor wilayani Longido, Mkoa wa Arusha, anakiri kupoteza mawasiliano na ndugu zake.

“Sina simu,” anasema kijana huyo, anayedai maisha yake hayajabadilika sana kwa sababu fedha anazopata hazitoshi kumudu maisha yake, ikiwemo kupata mahali pa kulala.
“Usiku ukiingia, ninalala popote. Hata nguo hii ndiyo pekee niliyonayo, naifua na kusubiri ikauke nivae.

Naoga mtoni na maeneo ninayoona kuwa ni safi,” anasema Naranda.
Akiwa na umri wa miaka 25, hana mipango ya kuanzisha familia kwa sababu hana mahali pa kumweka mwenza. Anasema hawezi kumudu mahitaji yake ya kila siku.

“Sina pesa, familia inahitaji pesa. Na ataishi wapi?” anahoji.
Kijana mwingine Joseph Nendukai, mlinzi wa moja ya majengo katika mitaa ya Sinza anasema alikuja Dar es Salaam mwaka 2017 kutafuta riziki.

“Nilikuwa na ng’ombe 20 na mbuzi 50, walikufa wakaacha ndama watatu tu na mbuzi 10. Hakukuwa na malisho na wengine walipata magonjwa,” anasema kijana huyo kutoka Kijiji cha Nanja, wilayani Monduli.

Nendukai anasema alimuacha mke na watoto wake wawili nyumbani chini ya uangalizi wa kaka yake. Anaeleza huwasiliana nao na huwasaidia.
Anasema huwa akiwatembelea angalau mara moja kwa mwaka au baada ya miaka miwili.

“Jamii zetu zimeathiriwa na ukame, mifugo mingi ilikufa, ndiyo maana wengi wetu tuliondoka nyumbani kutafuta riziki ili kusaidia familia,” anasema.

Viongozi wa vijiji

Kukiwa na matukio ya baadhi ya wanaume kuondoka na kuacha familia zao, viongozi wanasema si kwa kiwango kikubwa.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Terrat, Kone Medukenya, anasema shughuli kuu za wakazi wa kijiji hicho ni kilimo na ufugaji.

Anasema kilimo kimekuwa kikienea zaidi kutokana na hali ngumu kwa ufugaji.
Anasema ukame umeathiri upatikanaji wa malisho na ustawi wa kaya nyingi.

“Kuna kesi nyingi tunazoshughulikia zinazohusu migogoro ya kifamilia inayosababishwa na ugumu wa maisha, watu wanahangaika kutafuta chakula na mifugo yao inakufa… wengine wameondoka na kuacha familia zao, ingawa si kwa kiwango kikubwa,” anasema.

Kiongozi wa kimila wa Kimasai, maarufu kama Laigwanani, Lesira Samburi anasema kuna kesi nyingi za watu kuondoka, hasa vijana.

“Watu wanakimbia kaya, hasa vijana. Unajua, maisha yamebadilika sana. Licha ya kuwapo kwa ukame siku hizi, mifumo ya maisha imeathiri vijana,” anasema.
Anaeleza kuwapo kwa vifaa vya mawasiliano na ukosefu wa maadili miongoni mwa vijana waliosoma ni sababu nyingine ya wao kuhama.
Samburi anasema vijana wengi waliosoma wanasahau walikotoka.

“Nawaambia vijana wasisahau walikotoka, hapa ni nyumbani kwao,” anasema.
Kuhusu wanaume kukimbia kaya na familia zao kutokana na ugumu wa maisha, Laigwanani huyo anasema:

“Kamati ya kijiji, kwa kushirikiana na jamaa wa karibu wa mume, inajadili suala hilo, na wale wasio na mifugo wanapewa kiasi kidogo ili waendelee kukaa na familia zao.”

Kauli za wataalamu

Takwimu kutoka Kituo cha Ufuatiliaji wa Uhamaji wa Ndani Duniani (IDMC) zilionyesha kufikia mwaka 2020 hali mbaya ya hewa ilisababisha zaidi ya watu milioni 24 kuhama makazi yao, wakati Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) lilitabiri kufikia mwaka 2050, athari za mabadiliko ya tabianchi, ikiwa mabadiliko makubwa hayatafanyika sasa yatasababisha mamilioni ya watu zaidi kuhama.

Wakati huohuo, mtandao wa Groundswell unakadiria zaidi ya watu milioni 216 watahama, watatu kati ya watano watatoka Bara la Afrika.

Mhadhiri katika Kituo cha Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabianchi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Pius Yanda, anasema katika maeneo yanayoathiriwa na ukame, mafuriko au ukosefu wa malisho ya mifugo, watu wanalazimika kuhama kwenda mengine.

Profesa Yanda anasisitiza umuhimu wa kuhakikisha mazingira ambayo watu wanahama yawe na miundombinu ya kuwasaidia, hivyo kuzuia migogoro katika maeneo wanakohamia.

“Miradi kama vile BBT – Jenga Kesho iliyo Bora inatoa msaada mkubwa, lakini inahitaji kupanuliwa ili kufikia maeneo mengi zaidi. Miundombinu ya umwagiliaji na utafiti wa kusaidia kilimo endelevu ni muhimu,” anasema.

Dk Wessam El Beih kutoka Kituo cha IDMC alisema baadhi ya sera zinazoweza kuwalinda watu walio katika hatari kubwa ya kuhamishwa ni kuimarisha mazingira ya watu kustahimili, hasa kwa jamii za vijijini.

Anasema hilo linaweza kufanikiwa kwa kuwezesha upatikanaji wa huduma za msingi, fursa za kujipatia kipato na hatua za kupunguza athari za majanga kama vile mafuriko na ukame.

Habari hii imedhaminiwa na Bill & Melinda Gates Foundation

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Zanzibar airport operators decry job losses over Dubai deal

Tanzania air operators say over 600 workers are set to lose their jobs after the semi-autonomous government of Zanzibar awarded a Dubai-based company exclusive rights to handle ground services at a refurbished airport.

The Tanzania Air Operators Association (Taoa) said in a statement that the contract awarded to Dnata, which is registered at the London Stock Exchange, was in breach of the law banning any company from having exclusive rights to ground-handling services at major airports.Continue Reading

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Air Tanzania Banned From EU Airspace Due to Safety Concerns

Several airports have since locked Air Tanzania, dealing a severe blow to the Tanzanian national carrier that must now work overtime to regain its certification or go the wet lease way

The European Commission has announced the inclusion of Air Tanzania on the EU Air Safety List, effectively banning the airline from operating in European airspace.

The decision, made public on December 16, 2024, is based on safety concerns identified by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), which also led to the denial of Air Tanzania’s application for a Third Country Operator (TCO) authorisation.

The Commission did not go into the specifics of the safety infringement but industry experts suggest it is possible that the airline could have flown its Airbus A220 well past its scheduled major checks, thus violating the airworthiness directives.

“The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards for passengers in Europe and worldwide,” said Apostolos Tzitzikostas, EU Commissioner for Sustainable Transport and Tourism.

“We strongly urge Air Tanzania to take swift and decisive action to address these safety issues. I have offered the Commission’s assistance to the Tanzanian authorities in enhancing Air Tanzania’s safety performance and achieving full compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania has a mixed fleet of modern aircraft types including Boeing 787s, 737 Max jets, and Airbus A220s.

It has been flying the B787 Dreamliner to European destinations like Frankfurt in Germany and Athens in Greece and was looking to add London to its growing list with the A220.

But the ban not only scuppers the London dream but also has seen immediate ripple effect, with several airports – including regional like Kigali and continental – locking out Air Tanzania.

Tanzania operates KLM alongside the national carrier.

The European Commission said Air Tanzania may be permitted to exercise traffic rights by using wet-leased aircraft of an air carrier which is not subject to an operating ban, provided that the relevant safety standards are complied with.

A wet lease is where an airline pays to use an aircraft with a crew, fuel, and insurance all provided by the leasing company at a fee.

Two more to the list

The EU Air Safety List, maintained to ensure passenger safety, is updated periodically based on recommendations from the EU Air Safety Committee.

The latest revision, which followed a meeting of aviation safety experts in Brussels from November 19 to 21, 2024, now includes 129 airlines.

Of these, 100 are certified in 15 states where aviation oversight is deemed insufficient, and 29 are individual airlines with significant safety deficiencies.

Alongside Air Tanzania, other banned carriers include Air Zimbabwe (Zimbabwe), Avior Airlines (Venezuela), and Iran Aseman Airlines (Iran).

Commenting on the broader implications of the list, Tzitzikostas stated, “Our priority remains the safety of every traveler who relies on air transport. We urge all affected airlines to take these bans seriously and work collaboratively with international bodies to resolve the identified issues.”

In a positive development, Pakistan International Airlines (PIA) has been cleared to resume operations in the EU following a four-year suspension. The ban, which began in 2020, was lifted after substantial improvements in safety performance and oversight by PIA and the Pakistan Civil Aviation Authority (PCAA).

“Since the TCO Authorisation was suspended, PIA and PCAA have made remarkable progress in enhancing safety standards,” noted Tzitzikostas. “This demonstrates that safety issues can be resolved through determination and cooperation.”

Another Pakistani airline, Airblue Limited, has also received EASA’s TCO authorisation.

Decisions to include or exclude airlines from the EU Air Safety List are based on rigorous evaluations of international safety standards, particularly those established by the International Civil Aviation Organization (ICAO).

The process involves thorough review and consultation among EU Member State aviation safety experts, with oversight from the European Commission and support from EASA.

“Where an airline currently on the list believes it complies with the required safety standards, it can request a reassessment,” explained Tzitzikostas. “Our goal is not to penalize but to ensure safety compliance globally.”

Airlines listed on the EU Air Safety List face significant challenges to their international operations, as the bans highlight shortcomings in safety oversight by their home regulatory authorities.

For Air Tanzania, this inclusion signals an urgent need for reform within Tanzania’s aviation sector to address these deficiencies and align with global standards.

The path forward will require immediate and sustained efforts to rectify safety concerns and regain access to one of the world’s most critical aviation markets.

Source: allafrica.com

Continue Reading