Lissu aendelea na Mnyika katibu mkuu, awateua Dk Nshala, Lema kamati kuu

Lissu aendelea na Mnyika katibu mkuu, awateua Dk Nshala, Lema kamati kuu

Dar es Salaam. Mwenyekiti mpya wa Chadema, Tundu Lissu, ameanza kusuka safu za uongozi ndani ya chama hicho kwa kupendekeza majina ya Katibu Mkuu na Manaibu Katibu Wakuu wawili, Bara na Zanzibar.

Lissu ameunda safu ya viongozi hao wa sekretarieti wakiongozwa na Katibu Mkuu, John Mnyika, anayeendelea kushika wadhifa huo.

Akimpendekeza Mnyika mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho jioni ya leo, Jumatano, Januari 22, 2025, katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Lissu amewasilisha jina la Mnyika na manaibu wake kwa uthibitisho.

Ukumbi ukiwa umetulia, Lissu ametamka:”Amekulia kwenye chama, kijana wa chama kwelikweli, ameshika dhamana kubwa kwenye chama, ameshika dhamana kwenye Bunge. Sitawaleteeni ‘surprise’.”

“Ni mmoja wa wafanyakazi waadilifu sana wa chama chetu, na kama kulikuwa na uhitaji wa uthibitisho wa uwajibikaji wake ni John Mnyika. Sasa nawaleteeni John John Mnyika kuwa Katibu Mkuu wa chama chetu,” amesema Lissu huku ukumbi ukilipuka kwa shangwe.

Baada ya kutaja jina la Mnyika, aliuliza kama wanamthibitisha, ambapo wajumbe wote walinyoosha mikono kuonyesha ridhaa yao. Wajumbe mbalimbali walikwenda kumpa pongezi Mnyika, ambaye alianza kutumikia nafasi hiyo mwaka 2019.

Kisha, Lissu amemtaja Katibu wa Kanda ya Unguja Zanzibar, Wakili Ali Ibrahim Juma, kuwa Naibu Katibu Mkuu – Zanzibar, akichukua nafasi ya Salum Mwalimu, huku Katibu wa Kanda ya Kaskazini, Aman Golungwa, akiteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu – Bara, akichukua nafasi ya Benson Kigaila.

Juma na Golungwa walithibitishwa na Baraza Kuu kushika nafasi hizo.

Katika hatua nyingine, Lissu ametumia mamlaka yake ya kikatiba kuwateua wajumbe wa Kamati Kuu na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, ambao pia walithibitishwa na Baraza hilo.

Waliochaguliwa ni Godbless Lema-  aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini, Rose Mayembe – aliyekuwa Mwenyekiti wa chama Mkoa wa Njombe na Dk Rugemeleza Nshalla – aliyewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ambaye ameteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa chama.

“Huyu Rose amepitishwa katika misukosuko mingi. Ndiye sababu Mkoa wa Njombe usifanye uchaguzi hadi sasa ili asiwe kiongozi. Haya ndiyo makovu tunayosema yanapaswa kutibiwa, na mtakubaliana nami anafaa kuwa mjumbe wa kamatiKuu,” amesema Lissu.

Pia, amemteua Salima Kasanzu, Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza:

“Wakati wa usaili wa wagombea wa Bawacha (Baraza la Wanawake), baadhi ya wajumbe walihoji jina lake kuwepo kwenye orodha, lakini fomu yake haikuwepo. Tukafanya manuva fulani ambayo siwezi kuyasema hapa, akaitwa. Naye anafaa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu yetu.”

Mjumbe wa mwisho aliyeteuliwa ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba, Hafidh Ali Saleh.

“Kuanzia leo, hawa watano ni wajumbe wa Kamati Kuu ya chama chetu. Ninawaomba muwape maua yao. Karibuni sana katika kamati kuu,” amesema Lissu.

Baada ya kumaliza kuzungumza, alimkaribisha Salum Mwalimu, ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa miaka kumi, na mwaka 2020 alikuwa mgombea mwenza wa Lissu katika uchaguzi mkuu.

Mwalimu ametoa shukrani zake na kuwaomba radhi wote aliowakosea, huku akieleza uzoefu wake katika nafasi hiyo:

“Miaka kumi haikuwa miepesi hata kidogo. Kuacha suti na tai na kuvaa gwanda; kuacha kupanda ndege na kupanga magari na pikipiki. Miaka kumi ya Naibu Katibu Mkuu imenifundisha uvumilivu na ustahimilivu.”

Mwalimu amebainisha kwamba alishamweleza Mnyika mwaka 2021 kuwa hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho katika nafasi hiyo, akisisitiza kuwa dhamana hiyo si ndogo.

“Leo inaweza kuwa siku ngumu kwangu, kama ilivyokuwa siku ngumu miaka kumi nyuma katika ukumbi huu, Septemba 2014, nilipokabidhiwa nafasi hii. Ninawashukuru kwa kunivumilia. Kama kuna mtu yeyote niliyemkosea, naomba radhi,” amesema Mwalimu.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading