Lissu aendelea na Mnyika katibu mkuu, awateua Dk Nshala, Lema kamati kuu

Lissu aendelea na Mnyika katibu mkuu, awateua Dk Nshala, Lema kamati kuu

Dar es Salaam. Mwenyekiti mpya wa Chadema, Tundu Lissu, ameanza kusuka safu za uongozi ndani ya chama hicho kwa kupendekeza majina ya Katibu Mkuu na Manaibu Katibu Wakuu wawili, Bara na Zanzibar.

Lissu ameunda safu ya viongozi hao wa sekretarieti wakiongozwa na Katibu Mkuu, John Mnyika, anayeendelea kushika wadhifa huo.

Akimpendekeza Mnyika mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho jioni ya leo, Jumatano, Januari 22, 2025, katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Lissu amewasilisha jina la Mnyika na manaibu wake kwa uthibitisho.

Ukumbi ukiwa umetulia, Lissu ametamka:”Amekulia kwenye chama, kijana wa chama kwelikweli, ameshika dhamana kubwa kwenye chama, ameshika dhamana kwenye Bunge. Sitawaleteeni ‘surprise’.”

“Ni mmoja wa wafanyakazi waadilifu sana wa chama chetu, na kama kulikuwa na uhitaji wa uthibitisho wa uwajibikaji wake ni John Mnyika. Sasa nawaleteeni John John Mnyika kuwa Katibu Mkuu wa chama chetu,” amesema Lissu huku ukumbi ukilipuka kwa shangwe.

Baada ya kutaja jina la Mnyika, aliuliza kama wanamthibitisha, ambapo wajumbe wote walinyoosha mikono kuonyesha ridhaa yao. Wajumbe mbalimbali walikwenda kumpa pongezi Mnyika, ambaye alianza kutumikia nafasi hiyo mwaka 2019.

Kisha, Lissu amemtaja Katibu wa Kanda ya Unguja Zanzibar, Wakili Ali Ibrahim Juma, kuwa Naibu Katibu Mkuu – Zanzibar, akichukua nafasi ya Salum Mwalimu, huku Katibu wa Kanda ya Kaskazini, Aman Golungwa, akiteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu – Bara, akichukua nafasi ya Benson Kigaila.

Juma na Golungwa walithibitishwa na Baraza Kuu kushika nafasi hizo.

Katika hatua nyingine, Lissu ametumia mamlaka yake ya kikatiba kuwateua wajumbe wa Kamati Kuu na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, ambao pia walithibitishwa na Baraza hilo.

Waliochaguliwa ni Godbless Lema-  aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini, Rose Mayembe – aliyekuwa Mwenyekiti wa chama Mkoa wa Njombe na Dk Rugemeleza Nshalla – aliyewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ambaye ameteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa chama.

“Huyu Rose amepitishwa katika misukosuko mingi. Ndiye sababu Mkoa wa Njombe usifanye uchaguzi hadi sasa ili asiwe kiongozi. Haya ndiyo makovu tunayosema yanapaswa kutibiwa, na mtakubaliana nami anafaa kuwa mjumbe wa kamatiKuu,” amesema Lissu.

Pia, amemteua Salima Kasanzu, Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza:

“Wakati wa usaili wa wagombea wa Bawacha (Baraza la Wanawake), baadhi ya wajumbe walihoji jina lake kuwepo kwenye orodha, lakini fomu yake haikuwepo. Tukafanya manuva fulani ambayo siwezi kuyasema hapa, akaitwa. Naye anafaa kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu yetu.”

Mjumbe wa mwisho aliyeteuliwa ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba, Hafidh Ali Saleh.

“Kuanzia leo, hawa watano ni wajumbe wa Kamati Kuu ya chama chetu. Ninawaomba muwape maua yao. Karibuni sana katika kamati kuu,” amesema Lissu.

Baada ya kumaliza kuzungumza, alimkaribisha Salum Mwalimu, ambaye ametumikia nafasi hiyo kwa miaka kumi, na mwaka 2020 alikuwa mgombea mwenza wa Lissu katika uchaguzi mkuu.

Mwalimu ametoa shukrani zake na kuwaomba radhi wote aliowakosea, huku akieleza uzoefu wake katika nafasi hiyo:

“Miaka kumi haikuwa miepesi hata kidogo. Kuacha suti na tai na kuvaa gwanda; kuacha kupanda ndege na kupanga magari na pikipiki. Miaka kumi ya Naibu Katibu Mkuu imenifundisha uvumilivu na ustahimilivu.”

Mwalimu amebainisha kwamba alishamweleza Mnyika mwaka 2021 kuwa hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho katika nafasi hiyo, akisisitiza kuwa dhamana hiyo si ndogo.

“Leo inaweza kuwa siku ngumu kwangu, kama ilivyokuwa siku ngumu miaka kumi nyuma katika ukumbi huu, Septemba 2014, nilipokabidhiwa nafasi hii. Ninawashukuru kwa kunivumilia. Kama kuna mtu yeyote niliyemkosea, naomba radhi,” amesema Mwalimu.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading