LHRC, THBUB zataka hatua matukio ya utekaji, mauaji nchini

LHRC, THBUB zataka hatua matukio ya utekaji, mauaji nchini

Dar/Dodoma. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimetoa wito kwa Serikali kuona haja ya kuridhia mkataba wa kimataifa wa ulinzi kwa watu wote dhidi ya kupotea na kutekwa wa mwaka 1994, ili kukabiliana na ongezeko la matukio ya kupotea na kutekwa watu yanayoripotiwa nchini.

Shirika hilo limesema Tanzania haijaridhia mkataba huo ili kuufanya kuwa sehemu ya sheria zake.

Mbali ya hayo, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imelaani mauaji ya watu yanayoendelea nchini, ikiitaka jamii kuishi kwa kufuata sheria na kuheshimu haki ya msingi ya kila mtu kuishi.

Akizungumza Dar es Salaam leo Agosti 30, 2024 katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya waathirika wa matukio ya kutoweka na kutekwa, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC,  Anna Henga amesema kutokana na ongezeko la matukio hayo nchini, hiyo ni sababu tosha ya kuifanya Tanzania kuridhia mkataba huo ili kuweka ulinzi thabiti kwa wananchi.

“Manufaa ya mkataba huu katika ibara ya kwanza unabainisha na kuweka katazo la watu kuwekwa vizuizuini na matukio ya kutekwa kuwa ni kinyume na ulinzi wa haki za binadamu.

“Ibara ya pili mkataba unatafsiri vitendo vya kutoweka na utekaji ikijumuisha vitendo vya kutekwa, kuwekwa kizuizini au namna yoyote ya kumnyima mtu uhuru iwe kwa kufanywa na serikali, vyombo vyake au kwa maelezo ya serikali kwa kuelekeza chombo au mtu kuficha taarifa za alipo mtu aliyekamatwa au kutekwa,” amesema.

Amesema ibara ya sita ya mkataba huo inataka mamlaka kufanya uchunguzi na kuchukua hatua stahiki na kuwafikisha watu wote waliohusika na matukio ya kuficha taarifa za mtu aliyetekwa katika vyombo vya kisheria.

“Ibara ya 24 ya mkataba huo inaweka sharti kwa mamlaka husika zilizoridhia mkataba huo kutoa fidia kwa waathirika wote wa matukio ya utekaji ikiwemo, kutoa fedha za matibabu, fidia ya madhila na huduma ya kisaikolojia kwa waathirika na familia zao,” amesema.

Pamoja na ulinzi uliowekwa na ibara za 14 na 15 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 katika kulinda haki ya kuishi na uhuru wa mtu, amesema ni wakati kwa Serikali kuridhia sasa.

“Kuridhia mkataba huu si tu itaonesha kujizatiti katika jumuiya ya Umoja wa Mataifa kudhibiti vitendo hivyo, bali itaongeza imani kwa wananchi juu ya ulinzi na usalama wao,” amesema.

Amependekeza hatua zingine zinazopaswa kufanywa na dola ni kuimarisha mifumo ya ulinzi na usalama katika ngazi za jamii kwa kushirikiana na wananchi ili kudhibiti matukio hayo.

“Serikali kupitia vyombo vya ulinzi na usalama ifanye uchunguzi wa kina wa malalamiko dhidi ya matukio hayo, hususani katika kipindi cha hivi karibuni,” amesema.

Mauaji ya watu

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Jaji mstaafu Mathew Mwaimu amesema tume inalaani mauaji ya watu yanayoendelea nchini, akiitaka jamii kuishi kwa kufuata sheria na kuheshimu haki ya msingi ya kila mtu kuishi.

Jaji Mwaimu ametoa kauli hiyo leo Ijumaa, Agosti 30, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio ya mauaji yanayoendelea jijini Dodoma.

Amesema hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mauaji ya kutisha yanayoripotiwa na vyombo vya habari na Jeshi la Polisi.

Amesema tume inalaani wimbi la mauaji, baadhi yakitokana na wananchi kujichukulia sheria mkononi.

“Pamoja na Serikali na wadau kulaani vitendo hivyo mauaji hayo yameendelea kushika kasi licha ya Jeshi la Polisi kufanya jitihada za kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria,” amesema.

Baada ya kufuatilia mauaji hayo, tume imebaini kujengwa tabia za baadhi ya wananchi kutozingatia sheria za nchi na kujichukulia sheria mkononi.

“Katika baadhi ya mauaji yaliyotokea kuna viashiria vya ulipaji kisasi, wivu wa mapenzi, imani za kishirikina na baadhi ya wananchi wanajenga imani kuwa wanaweza kutenda uovu na wasikamatwe,” amesema.

Amesema baadhi ya wananchi hawana imani na vyombo vya usimamizi wa sheria na haki, na uwepo wa wananchi wasiopenda kufanya kazi halali na hivyo kuwa na tamaa ya mali.

Ili kukabiliana na matukio hayo, tume imependekeza Jeshi la Polisi liendelee kuchukua hatua mahususi kuimarisha mifumo ya ulinzi kwenye maeneo ya wananchi kuwezesha upatikanaji wa taarifa za mapema kuhusu kuwepo kwa viashiria vya uvunjifu wa sheria vinavyosababisha mauaji na vitendo vya ukatili kabla matukio hayo kutokea.

“Jeshi la Polisi liendelee kuchukua hatua kuhakikisha watu wote wanaohusika na mauaji hayo wanakamatwa ili sheria ichukue mkondo,” amesema,

Mamlaka katika ngazi zote zimetakiwa kuwa na mipango madhubuti kuhakikisha zinakuwapo taratibu za kuimarisha ulinzi na usalama wa raia kwa kushirikiana na Polisi.

Viongozi wa dini wametakiwa kuongeza nguvu katika utoaji wa elimu ya dini, maadili na kukemea uovu.

Wananchi wametakiwa washirikishe vyombo vya dola wanapoona maovu yakitendeka ndani ya jamii na kufichua uvunjifu wowote wa sheria na haki za binadamu.

Tume imependekeza asasi za kiraia na vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa umma, kuhusu taratibu zilizopo za namna ya kushughulikia masuala ya kijamii kupitia sheria.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Top News
Investment News Editor

ZSSF money not for projects, says Ali Karume

Unguja. Veteran politician and diplomat Ali Karume has called on authorities of the Zanzibar Revolutionary Government (SMZ) to refrain from using the Zanzibar Social Security Fund money for establishing commercial projects.Continue Reading

High Court rejects Transworld’s application
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

High Court rejects Transworld’s application

The High Court in Dar es Salaam has struck out an application in which Transworld Aviation, a ground handler at the Abeid Aman Karume International Airport (AAKIA) was seeking permission to sue the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA).Continue Reading

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading