Kitita cha uzazi chaleta tumaini mikoa mitano Tanzania

Kitita cha uzazi chaleta tumaini mikoa mitano Tanzania

Kitita cha uzazi chaleta tumaini mikoa mitano Tanzania

Dar es Salaam.  Kitita cha uzazi salama (SBBC) kimepunguza vifo vya watoto wachanga katika vituo vya afya 30 na kwenye mikoa mitano nchini kwa asilimia 75.

Mikoa iliyofikia malengo hayo ni Manyara, Shinyanga, Tabora, Geita na Mwanza ambayo mradi huo ulikuwa ukitekelezwa kuanzia mwaka 2021 hadi 2023.

Kupitia kitita hicho cha uzazi kwenye mikoa hiyo,  idadi ya kina mama na watoto waliofikiwa ni 300,000, vifo vya watoto kabla ya kuzaliwa vilipungua kwa asilimia 18 na kupunguzwa vifo vinavyotokea kwa kila saa 24 kwa asilimia 40.

Kwa takwimu za wiki, vifo vya watoto ambao hawajazaliwa vilipungua kwa asilimia 16 na asilimia 75 vifo vya uzazi. 

Mafanikio hayo kupitia kitita cha SBBC ni kutokana na mafunzo ya mara kwa mara wanayopewa watoa huduma wa afya ngazi ya jamii ya namna ya kukabiliana na matatizo ya kina mama wakati na baada ya kujifungua pamoja na kupatiwa vifaa.

Pia, wauguzi waliwezeshwa kushughulikia kesi ngumu zinazohusiana na ujauzito.

Kwa mujibu wa Mtafiti Mkuu wa SBBC, Dk Benjamin Kamala, kitita hicho kilichoanza kutekelezwa tangu 2021 hadi 2023 kililenga  kupunguza vifo vya uzazi na vya watoto wachanga kwa kuwapa watoa huduma wa afya ngazi ya jamii ujuzi wa kukabiliana na changamoto za uzazi katika hali ngumu.

Hivi karibuni, Dk Kamala amesisitiza kuwa, programu ya SBBC imebadili mfumo wa utamaduni wa vituo vya afya nchini kwa watoa huduma kujengewa uzoefu na kuwa washindani ambao wamechangia kupunguza rufaa zisizo za lazima.

 “Hapo awali, rufaa nyingi zilitokana na wakunga kukosa kujiamini katika kutoa huduma, watoa huduma tulionao sasa wamejiandaa kushughulikia changamoto zinazowakabili wajawazito na kuondoa rufaa zisizo za lazima,”amesema Dk Kamala.

Katika hatua nyingine, amesema takwimu zinazozalishwa kupitia vituo vya afya ndizo zinapaswa kutumiwa na watoa huduma za afya kukabiliana na eneo linaloonekana linachangamoto.

Tanzania imepiga hatua kufikia lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) 3.1, linalolenga kupunguza vifo vya uzazi kuwa chini ya 70 kwa kila vifo 100,000 vya watoto wanaozaliwa hai ifikapo mwaka 2030.

Hatua hiyo imefikiwa kupitia mipango mbalimbali ya kimkakati ya afya ya kuboresha huduma za uzazi na huduma za watoto wachanga ikiwemo mpango wa SBBC.

Februari mwaka huu, Waziri wa Afya, Jenista Mhagama akiwa katika mkutano wa 74 wa Mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Afya ya Nchi za Afrika Mashariki, Kati, na Kusini (ECSA – HC) uliofanyika Lilongwe nchini Malawi, alieleza juhudi zilizochukuliwa kukabiliana na vifo vitokanavyo na uzazi nchini, huku akidokeza  vifo vitokanavyo na uzazi vimepungua kutoka 1,744 mwaka 2018 hadi 1,477 mwaka 2022.

Pia, vifo vya watoto wachanga vimepungua kutoka 11,524 mwaka 2018 hadi 6,342 mwaka 2022.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading