Kesi mauaji ya polisi wanne, raia watatu Sitakishari kusikilizwa faragha

Kesi mauaji ya polisi wanne, raia watatu Sitakishari kusikilizwa faragha

Kesi mauaji ya polisi wanne, raia watatu Sitakishari kusikilizwa faragha

Dar es Salaam. Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imetoa amri kuzuia kutajwa majina ya mashahidi katika kesi ya mauaji ya askari wanne na raia watatu, tukio lililohusisha kundi la watu wenye silaha za kivita.

Kwa mujibu wa kiapo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Faustine Mafwele, washirika wa washtakiwa bado hawajakamatwa na kwamba, wamemuua mmoja wa mashahidi wa Jamhuri, mgambo MG 472454 Mussa Koti.

Amedai kundi hilo la watu wenye silaha lililovamia Kituo cha Polisi Stakishari kilichopo Ilala, Dar es Salaam, pia liliiba bunduki 11 aina ya Sub Machine Gun (SMG), bunduki tisa aina ya Semi-Automatic Rifles (SAR) na risasi 90.

Uamuzi wa Mahakama Kuu kuzuia kutajwa majina ya mashahidi na kesi kuendeshwa faragha, umetolewa Machi 17, 2025 na Jaji Hussein Mtembwa. Hukumu hiyo imewekwa kwenye mtandao wa Mahakama leo Machi 19, 2025.

Ombi lililotolewa uamuzi huo, liliwasilishwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupitia maombi ya jinai namba 5569 ya mwaka 2025 dhidi ya wajibu maombi 13 ambao ni washtakiwa katika kesi ya mauaji. Maombi hayo yalisikilizwa upande mmoja.

Wajibu maombi ni Omari Makota, Rajabu Mohamed, Ramadhani Hamis, Fadhil Lukwembe, Ally Salum, Khamis Salum, Nassoro Abdala, Seleman Salum, Said Chambeta, Hamis Masamba, Mohamed Ungando, Abdalla Kalupula na Mnemo Mwatumbo.

Maombi hayo yaliwasilishwa mahakamani kupitia kifungu cha 34(3) cha Sheria ya Kuzuia Ugaidi namba 21 ya mwaka 2002, ikisomwa pamoja na vifungu namba 188(1)(a)(b)(c) na (d) na kifungu cha (2) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA).

DPP aliomba amri ya kutotajwa majina na anuani au mahali walipo mashahidi kwa sababu za kiusalama wakati wa usikilizwaji wa uhamishaji wa shauri la mauaji kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenda Mahakama Kuu.

Aliomba hilo lifanyike pia wakati wa usikilizaji wa shauri la msingi la mauaji na mahakama itoe amri ya kutoweka wazi maelezo ya mashahidi na nyaraka yoyote inayoweza kuwatambulisha na mahali walipo.

Kiapo cha ACP Mafwele

Katika kiapo cha ACP Mafwele kilichoambatanishwa na maombi hayo, ameeleza Julai 12, 2015 Kituo cha Polisi cha Stakishari kilivamiwa na kundi la watu wenye silaha. Katika uvamizi huo polisi wanne na raia watatu waliuawa.

ACP Mafwele ambaye ni Mkuu wa Upelelezi (ZCO) wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam amesema askari waliofariki dunia ni D.6252 Sajini Adam Ryoba, E.1279 Koplo Peter Sabuni, E.3962 Koplo Gaudin na G.3010 Konstebo Anthony Komu. Wengine wawili ingawa walikuwa na majeraha makubwa walinusurika kifo.

Amewataja raia waliofariki dunia kwa kupigwa risasi katika uvamizi huo kuwa ni Jackline Duma, Erick Swai na Salehe Simkoko.

Katika kiapo hicho, amesema washambuliaji waliiba SMG 11, SAR tisa na risasi 90. Baada ya upelelezi ilibainika waliofanya tukio hilo walikuwa wamejificha katika msikiti wa Ulatule, ulioko Mkuranga.

Amesema upelelezi zaidi ulifanyika ambao watuhumiwa 13 walikamatwa na kwamba, vitendo vyao vilikuwa na dhamira ya kuvuruga Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hali ya kisiasa, kiuchumi na mfumo mzima wa jamii.

ACP Mafwele katika kiapo amedai kuna washirika wa washtakiwa hao ambao bado hawajakamatwa na jitihada za kuwakamata na baadaye kuwafikisha mbele ya mkono wa sheria kujibu tuhuma zao zinaendelea.

Amedai wajibu maombi (washtakiwa) kwa kushirikiana na washirika wao ambao bado hawajakamatwa, wanajaribu kupata utambulisho wa mashahidi wa Jamhuri ili kuwazuia wasitoe ushahidi.

Amedai washirika hao wa washtakiwa ambao bado hawajakamatwa, tayari wamemuua shahidi mmoja wa Jamhuri, MG 472454 Mussa Koti, ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Mamdikongo, Mkuranga baada ya kutoa maelezo Polisi.

Ni kutokana na mazingira hayo, unyeti na ukubwa wa mashtaka yanayowakabili washtakiwa na ukweli kuwa wapo washirika wao ambao hawajakamatwa, DPP anaona kutoa majina ya mashahidi ni kuhatarisha usalama wao na familia zao.

Uamuzi wa jaji

Baada ya kusikiliza hoja za DPP, Jaji amesema kulingana na kiapo cha ACP Mafwele na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Ashura Mzava, washirika wa washtakiwa wanajaribu kupata majina ya mashahidi ili kuwazuia kutoa ushahidi wao.

“Imeelezwa katika viapo hivyo kuwa tayari hao walioko uraiani maeneo mbalimbali ya Tanzania ambao bado hawajakamatwa, wamemuua mmoja wa mashahidi wa Jamhuri mara tu baada ya kutoa maelezo ya ushahidi polisi,” amesema jaji na kuongeza: “Hizi sababu kwangu naziona zina msingi sana.”

Katika uamuzi huo, jaji amesema: “Mawakili na maofisa wa mahakama hawajawahi kuzingatia kutofichuliwa kwa utambulisho wa mashahidi au ushahidi wowote au jambo lingine linaloweza kusababisha utambulisho wa shahidi kama kizuizi cha usikilizwaji wa haki.

“Inachukuliwa kama njia ya kuruhusu shahidi kutoa ushahidi wake kwa uhuru kuhusu kile anachokifahamu bila kutishwa na nguvu kutoka ndani au nje. Ni jukumu la mahakama kuhakikisha inamlinda shahidi, ndugu au marafiki zake.”

Kwa msingi huo, mahakama imeamuru utambulisho wa mashahidi wote wa Jamhuri usitajwe katika hatua za usikilizwaji wa hatua za mwanzo (committal) za kuhamisha kesi kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenda Mahakama Kuu ya Tanzania.

Pia ameamuru wakati wa usikilizwaji, shauri hilo litasikilizwa faragha na Ofisi ya Taifa ya Mashitaka (NPS) ipitie kwa makini maelezo yote ya mashahidi na nyaraka na kufuta majina na anuani zao ambazo zitaweza kuwatambulisha.

Mbali na amri hizo, ili kuhakikisha usikilizwaji wa shauri hilo unakuwa wa haki, Jaji ameitaka NPS kuandaa muhtasari wa ushahidi huo bila kutaja utambulisho wao kuwawezesha washtakiwa kujua aina ya ushahidi dhidi yao.

“Katika usikilizwaji wa ‘committal’ na usikilizwaji wa kesi hiyo, hakuna kusambaza au kuchapishwa nyaraka yoyote ya ushahidi ambayo itakuwa na utambulisho wa shahidi, pia taarifa yoyote inayoonyesha anuani zao nayo isichapishwe,” ameamuru jaji.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Second Marburg Outbreak After WHO Chief Visit

Dar es Salaam — Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan has declared an outbreak of Marburg virus, confirming a single case in the northwestern region of Kagera after a meeting with WHO director-general Tedros Adhanom Ghebreyesus.

The confirmation follows days of speculation about a possible outbreak in the region, after the WHO reported a number of deaths suspected to be linked to the highly infectious disease.

While Tanzania’s Ministry of Health declared last week that all suspected cases had tested negative for Marburg, the WHO called for additional testing at international reference laboratories.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”Amelia Clemence, public health researcher

Subsequent laboratory tests conducted at Kagera’s Kabaile Mobile Laboratory and confirmed in Dar es Salaam identified one positive case, while 25 other suspected cases tested negative, the president told a press conference in Dodoma, in the east of the country today (Monday).

“The epicentre has now shifted to Biharamulo district of Kagera,” she told the press conference, distinguishing this outbreak from the previous one centred in Bukoba district.

Tedros said the WHO would release US$3 million from its emergencies contingency fund to support efforts to contain the outbreak.

Health authorities stepped up surveillance and deployed emergency response teams after the WHO raised the alarm about nine suspected cases in the region, including eight deaths.

The suspected cases displayed symptoms consistent with Marburg infection, including headache, high fever, diarrhoea, and haemorrhagic complications, according to the WHO’s alert to member countries on 14 January. The organisation noted a case fatality rate of 89 per cent among the suspected cases.

“We appreciate the swift attention accorded by the WHO,” Hassan said.

She said her administration immediately investigated the WHO’s alert.

“The government took several measures, including the investigation of suspected individuals and the deployment of emergency response teams,” she added.

Cross-border transmission

The emergence of this case in a region that experienced Tanzania’s first-ever Marburg outbreak in March 2023 has raised concerns about cross-border transmission, particularly following Rwanda’s recent outbreak that infected 66 people and killed 15 before being declared over in December 2024.

The situation is particularly critical given Kagera’s position as a transport hub connecting four East African nations.

Amelia Clemence, a public health researcher working in the region, says constant vigilance is required.

“We never know when an outbreak might occur in a neighbouring nation. So we ensure infection prevention control assessments at every point of care as routine as a morning greeting at our workplaces.”

The Kagera region’s ecosystem, home to fruit bats that serve as natural reservoirs for the Marburg virus, adds another layer of complexity to disease surveillance efforts.

The virus, closely related to Ebola, spreads through contact with bodily fluids and can cause severe haemorrhagic fever.

Transparency urged

Elizabeth Sanga, shadow minister of health for Tanzania’s ACT Wazalendo opposition party, says greater transparency would help guide public health measures.

“This could have helped to guide those who are traveling to the affected region to be more vigilant and prevent the risk of further spread,” she said.

WHO regional director for Africa Matshidiso Moeti says early notification of investigation outcomes is important.

“We stand ready to support the government in its efforts to investigate and ensure that measures are in place for an effective and rapid response,” she said, noting that existing national capacities built from previous health emergencies could be quickly mobilised.

The situation coincides with leadership changes in Tanzania’s Ministry of Health, with both the chief medical officer and permanent secretary being replaced.

This piece was produced by SciDev.Net’s Sub-Saharan Africa English desk.

Source: allafrica.com

Continue Reading