JWTZ kutoa matibabu bure kwa siku tano

JWTZ kutoa matibabu bure kwa siku tano

Dar es Salaam. Katika kuadhimisha miaka 60 ya kuanzishwa kwake, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), litatoa huduma za upimaji na matibabu ya afya bila malipo kwa siku tano kuanzia kesho Agosti 26, mwaka huu.

Huduma hizo kwa mujibu wa jeshi hilo, zitatolewa bure hadi Agosti 30, mwaka huu na Septemba Mosi, zitatolewa huduma za matibabu ya dharura.

Hayo yameelezwa katika taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa  leo, Agosti 25, 2024 na kusainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ Makao Makuu, Kanali Gaudentius Ilonda.

Amesema kilele cha maadhimisho hayo ni Septemba Mosi, mwaka huu siku ambayo huduma za matibabu ya dharura zitatolewa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Huduma za jumla zitakazotolewa katika siku hizo, amesema ni ushauri na upimaji wa magonjwa yanayoambukizwa na yasiyoambukizwa yakiwemo Malaria, saratani ya tezi dume kwa njia ya damu, magonjwa ya kinywa na meno na saratani ya matiti na shingo ya uzazi.

Huduma hizo kwa mujibu wa Kanali Ilonda, zitatolewa katika Uwanja wa Zakhem Mbagala, Uwanja wa Bububu Unguja, Uwanja wa Magereza Arusha, Uwanja wa Tarafani Mbeya, Uwanja wa Furahisha Mwanza, Uwanja wa Chipukizi Tabora na Uwanja wa Shule ya Sekondari Morogoro mkoani Morogoro.

Maeneo mengine, amesema ni Uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe Ruvuma, Uwanja wa Gombani Pemba, Uwanja wa Nyerere Square- Dodoma na Uwanja wa Stendi ya zamani Nachingwea Lindi.

Hata hivyo, amesema wanajeshi katika kambi zote watachangia damu salama, shughuli itakayoendeshwa na hospitali zote za jeshi kwa kushirikiana na Kitengo cha Taifa cha Damu Salama.

“Wananchi wote wanakaribishwa ili kunufaika na huduma za tiba zitakazotolewa pamoja na kujitolea kuchangia damu salama,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading