JWTZ kutoa matibabu bure kwa siku tano

JWTZ kutoa matibabu bure kwa siku tano

Dar es Salaam. Katika kuadhimisha miaka 60 ya kuanzishwa kwake, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), litatoa huduma za upimaji na matibabu ya afya bila malipo kwa siku tano kuanzia kesho Agosti 26, mwaka huu.

Huduma hizo kwa mujibu wa jeshi hilo, zitatolewa bure hadi Agosti 30, mwaka huu na Septemba Mosi, zitatolewa huduma za matibabu ya dharura.

Hayo yameelezwa katika taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa  leo, Agosti 25, 2024 na kusainiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ Makao Makuu, Kanali Gaudentius Ilonda.

Amesema kilele cha maadhimisho hayo ni Septemba Mosi, mwaka huu siku ambayo huduma za matibabu ya dharura zitatolewa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Huduma za jumla zitakazotolewa katika siku hizo, amesema ni ushauri na upimaji wa magonjwa yanayoambukizwa na yasiyoambukizwa yakiwemo Malaria, saratani ya tezi dume kwa njia ya damu, magonjwa ya kinywa na meno na saratani ya matiti na shingo ya uzazi.

Huduma hizo kwa mujibu wa Kanali Ilonda, zitatolewa katika Uwanja wa Zakhem Mbagala, Uwanja wa Bububu Unguja, Uwanja wa Magereza Arusha, Uwanja wa Tarafani Mbeya, Uwanja wa Furahisha Mwanza, Uwanja wa Chipukizi Tabora na Uwanja wa Shule ya Sekondari Morogoro mkoani Morogoro.

Maeneo mengine, amesema ni Uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe Ruvuma, Uwanja wa Gombani Pemba, Uwanja wa Nyerere Square- Dodoma na Uwanja wa Stendi ya zamani Nachingwea Lindi.

Hata hivyo, amesema wanajeshi katika kambi zote watachangia damu salama, shughuli itakayoendeshwa na hospitali zote za jeshi kwa kushirikiana na Kitengo cha Taifa cha Damu Salama.

“Wananchi wote wanakaribishwa ili kunufaika na huduma za tiba zitakazotolewa pamoja na kujitolea kuchangia damu salama,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’
Top News
Chief Editor

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Africa: Rwanda Gets a Grip Of Marburg, But Mpox ‘Not Yet Under Control’

Monrovia — The Rwanda Minister of State responsible for Health, Dr. Yvan Butera, cautioned that while the country is beginning to see positive signals in its fight against the Marburg virus, the outbreak is “not yet over”. He, however, expressed hope that  “we are headed in that direction”. The minister said the epidemiology trend, since the disease was first discovered in the country more than a month ago, is moving towards fewer cases.

Dr. Butera, who was giving updates during an online briefing yesterday, said in the past two weeks, only two deaths were recorded while 14 people recovered from the disease. He said Rwanda was expanding its testing capacity with 16,000 people already inoculated against the disease.

The priority right now, Butera said, is “rapid testing and detection”.

Marburg is a highly virulent disease transmitted through human-to-human contact or contact with an infected animal. The fatality rate of cases, which has varied over the period, is more than 50%, according to the World Health Organization.  WHO said the highest number of new confirmed cases in Rwanda were reported in the first two weeks of the outbreak. There’s been a “sharp decline” in the last few weeks, with the country now tackling over 60 cases.

At Thursday’s briefing, a senior official of the Africa Centers for Disease Control, Dr. Ngashi Ngongo, said mpox – the other infectious disease outbreak that countries in the region are fighting – was been reported in 19 countries, with Mauritius being the latest country to confirm a case. He said although no new cases have been recorded in recent weeks in several countries where outbreaks occurred previously –  including Cameroon, South Africa, Guinea, and Gabon – Uganda confirmed its first Mpox death. This, he said, is one of two fatalities reported outside Central Africa.

Dr. Ngashi revealed that there was an increase in cases in Liberia and Uganda. He said mpox cases were still on an upward trend.

“The situation is not yet under control.”

Source: allafrica.com

Continue Reading