Jinsi vituo vya umahiri Tanzania vitakavyochochea mapinduzi ya teknolojia

Jinsi vituo vya umahiri Tanzania vitakavyochochea mapinduzi ya teknolojia

Dar es Salaam. Ujenzi wa vituo vya umahiri nchini Tanzania vinatajwa kuleta mapinduzi katika utoaji wa elimu na kuzalisha wataalamu wa kutosha katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), usafirishaji, utengenezaji wa bidhaa za ngozi pamoja na nishati jadidifu.

Pia, katika kuwapa ujuzi vijana utakaowawezesha kuendana na matakwa ya soko la ajira lililopo sasa pamoja na namna ya kutumia fursa zilizopo katika mazingira yao kujiajiri na kutengeneza ajira kwa wengine.

Vituo hivyo vya umahiri vimejengwa kupitia Mradi wa Kujenga Ujuzi kwa Maendeleo na Uingiliano wa Kikanda katika Afrika Mashariki (EASTRIP) uliofadhiliwa na Benki ya Dunia na kuanza kutekelezwa tangu mwaka 2019 na kugharimu zaidi ya Sh172 bilioni.

Hayo yameelezwa leo Jumatatu, Septemba 9, 2024 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Elimu Ufundi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Fredrick Salukeke katika kikao kazi kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa mradi huo.

Salukeke amesema moja ya lengo la mradi na vituo hivyo vya umahiri ni kuongeza upatikanaji na kuboresha ubora wa programu katika Vyuo vya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi vya Kikanda (TVET).

Amesema uboreshaji huo unafanyika kwa kufanya mambo mbalimbali, ikiwemo kusomesha wakufunzi, kuwawezesha kupata uzoefu kutoka katika taasisi nyingine ndani na nje ya nchi, kuboresha mitaala na kuimarisha ushirikiano kati ya vyuo na viwanda ili wanafunzi watakaomaliza wapate ujuzi unaotakiwa viwandani.

“Moja kati ya changamoto tulioigundua ni pamoja na kutokuwa na muunganiko wa moja kwa moja kati ya wakufunzi na waajiri, hivyo kupitia mradi huu tunataka kuimarisha ushirikiano huo wenye lengo la kuboresha elimu ya ujuzi wanaopatiwa wanafunzi,” amesema.

Amesema kwa sasa mradi huo hapa nchini umewezesha kujengwa kwa vituo vya umahiri vinne ambavyo ni kituo cha umahiri cha mafunzo ya Tehama (RAFIC) katika Taasisi ya Teknolojia kampasi ya Dar es Salaam (DIT).

Pia kituo cha umahiri cha mafunzo ya taaluma za anga na operesheni za usafirishaji (CoEATO) katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Kituo cha mafunzo na utafiti wa nishati jadidifu (Kikuletwa) katika chuo cha ufundi Arusha pamoja na kile  cha Uchakataji Ngozi (CELPAT) kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam kampasi ya Mwanza.

“Pamoja na nchi ya Tanzania, mradi huo pia unatekelezwa katika nchi ya Kenya pamoja na Ethiopia,” amesema.

Kwa upande wake, mkuu wa kituo cha umahiri cha mafunzo ya taaluma za anga na operesheni za usafirishaji (CoEATO) katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Dk Chacha Ryoba amesema kupitia mradi huo imewezesha kupatikana kwa vifaa na mitambo mipya ya kisasa ya kufundishia na kujifunzia, ili kitoe mafunzo yanayoendana na teknolojia ya kisasa na kuzalisha wataalamu watakaoweza kushindani katika soko la ajira.

Pia amesema kuanzishwa kwa vituo hivyo ni kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kuwa kila kimoja kitakuwa na mchango chanya katika kutatua changamoto za jamii na pia kuchochea maendeleo ya taifa

Naye mkaguzi wa mradi kutoka kituo cha umahiri cha uchakataji ngozi (CELPAT) kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) kampasi ya Mwanza, amesema pamoja na kusaidia kuboresha utolewaji wa elimu ya ufundi nchini, pia itasaidia katika kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa.

Hiyo itawezekana kutokana na uboreshwaji wa miundombinu, ikiwemo ujenzi wa madarasa pamoja na hosteli kwa ajili ya malazi kwa wanafunzi.

“Hilo litasaidia kuongezea uwezo vyuo ambayo vina vituo hivyo vya umahiri kuongeza uwezo wake wa kupokea wanafunzi, jambo ambalo litasaidia katika kuchochea kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa katika vyuo hivyo,” amesema.

Ametolea mfano katika kampasi hiyo mradi ukikamilika wanatarajia kupokea wanafunzi takribani 2500, 2100 wakiwa wa kozi ndefu na 400 kozi za muda mfupi.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Tanzania Declares Marburg Outbreak – Africa CDC Mobilizes Immediate Response

Addis Ababa, January 20, 2025</Strong> — Tanzania has declared a Marburg virus disease (MVD) outbreak after confirming one case and identifying 25 suspected cases in the Kagera Region of Northwestern Tanzania. The Marburg virus, a highly infectious and often fatal disease, is similar to Ebola and is transmitted to humans from fruit bats and monkeys. This outbreak marks the nation’s second encounter with the deadly virus, following the outbreak in Bukoba District of Kagera Region in March 2023, which resulted in nine cases and six deaths.

In response to this urgent threat, the Africa CDC is mobilizing strong support to help Tanzania contain the outbreak. A team of twelve public health experts will be deployed as part of an advance mission in the next 24 hours. The multidisciplinary team includes epidemiologists, risk communication, infection prevention and control (IPC), and laboratory experts to provide on-ground support for surveillance, IPC, diagnostics, and community engagement.

The Director-General of Africa CDC, Dr. Jean Kaseya, has engaged with Tanzania’s President Samia Suluhu Hassan and the Minister of Health to ensure coordinated efforts and secure political commitment for the response.

“Africa CDC stands firmly with Tanzania in this critical moment. To support the government’s efforts, we are committing US$ 2 million to bolster immediate response measures, including deploying public health experts, strengthening diagnostics, and enhancing case management. Building on Tanzania’s commendable response during the 2023 outbreak, we are confident that swift and decisive action, combined with our support and those of other partners, will bring this outbreak under control,” Dr. Kaseya stated.

Africa CDC has recently supported efforts to enhance the diagnostic and sequencing capacity of public health laboratories in Tanzania. PCR Test kits and genomic sequencing reagents have been dispatched, with additional supplies in the pipeline. To ensure rapid identification and confirmation of cases, the institution will also provide technical assistance to strengthen detection and genome sequencing for better characterization of the pathogen. Additionally, support will be provided to improve case management protocols and enhance the capacity to deliver safe and effective treatment.

Africa CDC is committed to working closely with the Government of Tanzania, regional partners, international organizations, and global stakeholders, including the World Health Organization, to stop the spread of the Marburg virus.

Source: allafrica.com

Continue Reading