Jinsi Dola 3,900 zilivyomtupa jela bosi wa  kampuni ya Utalii Arusha

Jinsi Dola 3,900 zilivyomtupa jela bosi wa  kampuni ya Utalii Arusha

 Arusha. Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, imemhukumu Mkurugenzi wa kampuni ya Expedition Africa Limited, Majaliwa Gogo, kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela na kulipa faini ya Sh2 milioni kwa kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Gogo alipokea kundi la watalii 17 kutoka India walioingia nchini kupitia mpaka wa Namanga kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Manyara, Serengeti na Ngorongoro kwa gharama ya Dola 18,657 za Marekani (Sh47 milioni).

Kwa kuwa kampuni yake ilikuwa haijakata leseni ya utalii inayojulikana kama Tourist Agency License (Tala), mshitakiwa alimuomba shahidi wa pili, Christian Ayo ili atumie kampuni yake ya West Way Safaris kwa ajili ya kuwapeleka watalii hao hifadhini.

Licha ya kulipwa fedha hizo na Pradeep Mogasati ambaye ni mmiliki wa kampuni ya utalii inayofanya shughuli zake Jijini Nairobi Kenya, Gogo hakulipa ada stahiki katika malango ya kuingia katika hifadhi hizo akisingizia akaunti zake zimefungwa na Serikali.

Safari ya watalii hao ilianza Desemba 22,2022 wakielekea Hifadhi ya Taifa ya Manyara, lakini wakiwa njiani, Mogasati akapokea ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa mkurugenzi huyo kuwa ada katika hifadhi hizo hakuwa amezilipa kwa sababu akaunti zimefungwa.

Mkurugenzi huyo akamuomba Mogasati kulipa ada hizo kwa masharti kuwa angezirejesha fedha hizo mara tu akaunti yake ikifunguliwa na Serikali, hivyo Mogasati akalipa Dola 7,800 za Marekani, sawa na zaidi ya Sh19.5 milioni za Tanzania.

Kulingana na hukumu hiyo iliyotolewa na Hakimu Mkazi, Regina Oyier,  Machi 15,2024 na nakala yake kupatikana leo Alhamisi Aprili 11, 2024, inasema mshitakiwa hakurejesha fedha hizo na Mogasati alipokuwa akimpigia simu na kumtumia SMS, alikuwa hapokei wala kujibu.

Hata hivyo, siku moja walikutana Jijini Arusha ambapo aliahidi kulipa fedha hizo Januari 3, 2024 lakini hakulipa ndipo Mogasati akafungua malalamiko kituo cha Polisi cha Utalii na Diplomasia na kesi kupelelezwa kwa weledi na Mrakibu wa Polisi (SP), Waziri Tenga.

Baada ya upelelezi kukamilika, mkurugenzi huyo akafikishwa mahakamani na kufunguliwa mashitaka mawili ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuendesha biashara ya utalii, makosa ambayo mahakama ilimtia hatiani Machi 15,2024.

Katika utetezi wake, mkurugenzi huyo alikana kumfahamu shahidi wa tatu, Mogasati wala kufanya naye biashara yoyote inayohusiana na utalii na pia akakana kumiliki kampuni yoyote ya utalii, bali anajishughulisha na asasi ya kulinda haki za watalii.

Hukumu ilivyokuwa

Akisoma hukumu dhidi ya mshitakiwa, Hakimu Oyier alisema shahidi wa tatu alieleza  kuwa Novemba 2022 alikuja Arusha na kupokelewa na mshitakiwa ambaye alimpeleka hotelini, na siku iliyofuata walifanya mazungumzo kuhusiana na biashara ya watalii 17.

“Ni mshitakiwa ndiye aliyependekeza maeneo ambao watalii hao watatembelea na gharama ya safari nzima. Lakini hiyo haikuwa siku pekee ambapo walikutana bali walikutana tena Arusha Desemba 22,2022 na Mto wa Mbu Desemba 26,2022”alieleza.

“Ni dhahiri kuwa shahidi huyo alimfahamu mshitakiwa vizuri na Dola 12,000 ambazo mshitakiwa alipokea kutoka kwa shahidi wa tatu, zilikuwa ni kwa ajili ya kugharamia safari ambayo yeye ndio aliipanga kwa watalii 17 walioletwa na Mogasati,”alisema.

“Mahakama hii inaona hakuna sababu ya kutilia mashaka ushahidi wa shahidi huyo wa tatu. Hii ni kwa sababu  hata ushahidi wa shahidi wa 2 ambaye naye anafanya biashara ya utalii anamfahamu mshitakiwa kama mkurugenzi wa Expedition Africa Ltd”

Mbali na kumfahamu, lakini ofisi zao zilikuwa katika jengo moja la Kwa Kondo.

Hakimu alisema kampuni hiyo haikuwa na leseni ya kuendesha biashara ya utalii kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, pia  kitendo cha mshitakiwa kumuomba shahidi wa pili atumie kampuni yake inathibitisha kuwa kampuni ya mshitakiwa haikuwa na leseni.

“Kulingana na ushahidi tunaona namna mshitakiwa alivyojitambulisha kama mmiliki wa kampuni ya Expedition Africa Limited ambayo inafanya biashara jijini Arusha na kwa mwavuli huo, ndio maana shahidi wa tatu alimwamini na kumpa fedha.

Hakimu alisema ni jambo lililo wazi kuwa mshitakiwa alipaswa kulipa ada za kuingia kwenye malango ya hifadhi za Manyara, Serengeti na Ngorongoro, lakini badala yake akaja na hadithi kwamba alishindwa kulipa kwa kuwa Serikali imefunga akaunti zake.

Alisema shahidi wa tatu aliieleza mahakama kuwa alitumia Dola 7,800 kulipa katika malango, lakini baada ya kupitia kielelezo P3 cha upande wa mashitaka anaona fedha ambazo shahidi huyo alizilipa kwenye malango ni Dola 3,974 na Sh229,920 tu.

Hakimu huyo alisema akaunti za mshitakiwa hazikuwa zimefungwa na Serikali kama mshitakiwa alivyomuongopea shahidi wa tatu, kwani ushahidi uliofanywa na SP Tenga ulibaini akaunti hiyo  haikuwa imefungwa na Serikali katika kipindi cha Desemba 2022.

Kulingana na ushahidi huo,  Desemba 16,2022 kiasi cha Dola 5,000 kilitolewa kwenye akaunti hiyo na Desemba 21, 2022 kiasi kingine Dola 400 kilitolewa kwenye akaunti na Hakimu akasema kama aliweza kutoa fedha hizo, kwa nini hakulipa ada za hifadhini.

Hakimu alisema upande wa mashitaka uliweza kuthibitisha mashitaka dhidi ya mkurugenzi huyo pasipo kuacha mashaka, hivyo anamhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kwanza, na kulipa faini ya Sh2 milioni kwa shitaka la pili.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading