Jeshi la Zimamoto kuajiri watumishi wapya 1,000

Jeshi la Zimamoto kuajiri watumishi wapya 1,000

Jeshi la Zimamoto kuajiri watumishi wapya 1,000

Morogoro. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Juma Mkomi, amesema katika bajeti ijayo Serikali imepanga kuajiri watumishi wapya 1,000 wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini.

Mkomi amesema hayo leo Jumatatu, Machi 10, 2025, wakati akifungua kikao cha Baraza Dogo la Wafanyakazi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kilichofanyika mkoani Morogoro.

Pia, amelitaka jeshi hilo kuziwajibisha ofisi zote ambazo hazitakuwa na vifaa vya kuzimia moto, kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria za zimamoto.

Amesema kwenye bajeti ya mwaka 2025/2026 Serikali imepanga kuajiri watumishi 1,000 kwenye Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Pia, amelitaka jeshi hilo kufuata utaratibu wakati wa kufanya mchujo wa kuwapata watumishi wapya na kusisitiza vipimo vifanyike kabla ya kuajiri watumishi wapya.

Mkomi, kwenye hotuba yake, pia amelitaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini kufanya ukaguzi wa vifaa vya kuzimia moto kwenye ofisi za umma ili kuona kama vinafanya kazi ama vimewekwa kama mapambo.

“Ukaguzi huo uende sambamba na utoaji wa elimu ya kutosha kwa umma kuhusu namna ya kuzuia majanga ya moto na kukabiliana nayo. Kitengo cha mawasiliano kwa umma kiongezewe nguvu, kuna mambo mengi yanayohusu Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambayo wananchi wanapaswa kujua kupitia kitengo hiki,” amesema Mkomi.

Akitoa taarifa ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali wa Zimamoto na Uokoaji, John Masunga, amesema katika mwaka wa fedha 2024/2025 jeshi hilo limetenga zaidi ya Sh6.5 bilioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ikiwemo uendelezaji wa ujenzi wa vituo saba vya kuzimia moto na uokoaji katika mikoa ya Songwe, Simiyu, Kagera, Njombe, Manyara, Katavi, na Geita.

Aidha, katika bajeti hiyo wataweza kununua vifaa vya kuzimia moto na uokoaji, pamoja na uchunguzi na ukarabati wa kituo cha kuzimia moto na uokoaji katika Mkoa wa Morogoro na kuendeleza ujenzi wa majengo mawili ya ghorofa kwa ajili ya makazi ya askari Kikombo, jijini Dodoma.

Kamishna Masunga amesema jeshi lina jumla ya vituo 80 vya zimamoto na uokoaji katika mikoa ya Tanzania Bara, ambapo kati ya vituo hivyo, 56 vipo katika ngazi ya wilaya na 24 kwenye viwanja vya ndege.

“Jeshi lina uhitaji wa vituo vipya 237 katika wilaya na maeneo mengine ili kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi,” amesema Kamishna Masunga.

Amesema utaratibu wa upatikanaji wa mkopo wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 100 tayari umesainiwa Februari 15, 2024, kati ya Serikali na Taasisi ya Abu Dhabi Export Office (ADEX) kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Mkopo huo ni kwa ajili ya ununuzi wa vitendeakazi mbalimbali, vikiwemo magari 150 ya kuzima moto na uokoaji, magari 40 ya kubebea wagonjwa, boti 23 za kuzimia moto, na helikopta moja ya kuzimia moto.

Kamishna Masunga ametaja changamoto zinazolikabili Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kuwa ni pamoja na uhaba wa vifaa na vitendeakazi kwa ajili ya utoaji huduma, uchache wa vituo vya kujazia maji ya kuzimia moto, na ujenzi holela katika maeneo mengi hasa mijini, hali inayosababisha askari kushindwa kufika kwa urahisi wakati wa dharura za moto na majanga mengine.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Top News
Investment News Editor

ZSSF money not for projects, says Ali Karume

Unguja. Veteran politician and diplomat Ali Karume has called on authorities of the Zanzibar Revolutionary Government (SMZ) to refrain from using the Zanzibar Social Security Fund money for establishing commercial projects.Continue Reading

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Confirms Outbreak of Marburg Virus Disease

Dodoma — Tanzania today confirmed an outbreak of Marburg virus disease in the northwestern Kagera region after one case tested positive for the virus following investigations and laboratory analysis of suspected cases of the disease.

President of the Republic of Tanzania, Her Excellency Samia Suluhu Hassan, made the announcement during a press briefing alongside World Health Organization (WHO) Director-General, Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus, in the country’s administrative capital Dodoma.

“Laboratory tests conducted in Kabaile Mobile Laboratory in Kagera and later confirmed in Dar es Salaam identified one patient as being infected with the Marburg virus. Fortunately, the remaining suspected patients tested negative,” the president said. “We have demonstrated in the past our ability to contain a similar outbreak and are determined to do the same this time around.”

A total of 25 suspected cases have been reported as of 20 January 2025, all of whom have tested negative and are currently under close follow-up, the president said. The cases have been reported in Biharamulo and Muleba districts in Kagera.

“We have resolved to reassure the general public in Tanzania and the international community as a whole of our collective determination to address the global health challenges, including the Marburg virus disease,” said H.E President Hassan.

WHO is supporting Tanzanian health authorities to enhance key outbreak control measures including disease surveillance, testing, treatment, infection prevention and control, case management, as well as increasing public awareness among communities to prevent further spread of the virus.

“WHO, working with its partners, is committed to supporting the government of Tanzania to bring the outbreak under control as soon as possible, and to build a healthier, safer, fairer future for all the people of Tanzania,” said Dr Tedros. “Now is a time for collaboration, and commitment, to protecting the health of all people in Tanzania, and the region, from the risks posed by this disease.”

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

“The declaration by the president and the measures being taken by the government are crucial in addressing the threat of this disease at the local and national levels as well as preventing potential cross-border spread,” said Dr Matshidiso Moeti, WHO Regional Director for Africa. “Our priority is to support the government to rapidly scale up measures to effectively respond to this outbreak and safeguard the health of the population,”

Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in March 2023 – the country’s first – in Kagera region, in which a total of nine cases (eight confirmed and one probable) and six deaths were reported, with a case fatality ratio of 67%.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Marburg virus is transmitted to people from fruit bats and spreads among humans through direct contact with the bodily fluids of infected people, surfaces and materials. Although several promising candidate medical countermeasures are currently undergoing clinical trials, there is no licensed treatment or vaccine for effective management or prevention of Marburg virus disease. However, early access to treatment and supportive care – rehydration with oral or intravenous fluids – and treatment of specific symptoms, improve survival.

Source: allafrica.com

Continue Reading