Jeshi la Polisi lakanusha taarifa ya Polisi

Jeshi la Polisi lakanusha taarifa ya Polisi

Dar es Salaam. Sakata la kuzuiwa mikutano ya hadhara na ile ya ndani ya vyama vya siasa limechukua sura mpya, baada ya Jeshi la Polisi Tanzania kukanusha zuio la Polisi Wilaya ya Mbagala, Mkoa wa Dar es Salaam.

Kanusho hilo la Polisi Makao Makuu linatokana na taarifa ya Polisi Mbagala kwenda kwa chama cha ACT-Wazalendo kuzuia kufanyika kwa mkutano wa hadhara waliopanga kufanyika leo Jumatatu, Agosti 12, 2024 katika Kata ya Charambe, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Barua ya Polisi Wilaya ya Mbagala kwenda kwa ACT-Wazalendo ya leo Jumatatu, pamoja na mambo mengine imesema: “…napenda kukujulisha kuwa mikutano yote ya hadhara na ya ndani imezuiliwa hadi hapo yatakapotolewa maelekezo mengine.”

Baada ya barua hiyo mijadala imeshika kasi mitandaoni, huku wadau wa kisiasa wakikumbusha kile kilichotokea mwaka 2016 kwa mikutano ya hadhara kupigwa marufuku na kuruhusiwa ile ya ndani.

Zuio hilo la mikutano liliwekwa wakati wa utawala wa awamu ya tano, baada ya utawala wa awamu ya sita kuingia madarakani ukiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan uliliondoa na mikutano kurejea.

Mwananchi lilizungumza na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kutaka kujua undani wa zuio hilo la Polisi Mbagala ambapo amesema kinachojitokeza ni hali ya jeshi hilo kujichanganya, hakuna tamko rasmi lilotolewa la kufuta mikutano ya hadhara na ile ya ndani.

“Kilichotokea naona kama Polisi wamejichanganya, hakuna tamko rasmi lilotolewa la kuzuia mikutano ya hadhara na ya ndani kwa kuwa Jeshi la Polisi lina ngazi aulizwe msemaji wake anaweza kuwa na majibu sahihi,” amesema Jaji Mutungi.

Katikati ya mijadala hiyo, saa 8:20 mchana, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime akatoa taarifa kwa umma akisema: “Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa kuwa halijapiga marufuku kufanyika mikutano ya nje ya hadhara na ile ya ndani, ili mradi inafuata matakwa ya sheria za nchi.”

“Kilichopigwa marufuku ni mkusanyiko uliokuwa umeitishwa na viongozi wa Chadema huko jijini Mbeya, kwa kivuli cha kuadhimisha Siku ya Vijana Duniani,”ilieleza taarifa hiyo.
 

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

Tanzania: Exim to Raise Fund for Mental Health Facilities Upgrades

EXIM Bank to raise 300m/- over the next three years for financing essential services and infrastructure upgrades in mental health facilities.

The bank’s Head of Marketing and Communications Stanley Kafu unveiled this when introducing Exim Bima Festival 2024 as a platform for bringing together individuals, organisations and various sectors for raising the funds.

“Exim’s initiative aligns with the government’s broader goals to ensure that every citizen has access to quality healthcare, including mental health services,” he said.

The initiative, which is one of the events for celebrating the bank’s 27th anniversary is scheduled for Wednesday this week in Dar es Salaam.

Mr Kafu highlights that this year’s festival is not only about raising awareness of the importance of insurance in the society but also focuses on enhancing access to mental health services and improving the overall well-being of the nation.

Statistics from the Ministry of Health shows a staggering 82 per cent increase in mental health cases over the past decade.

Mental cases have risen from 386,358 in 2012 to 2,102,726 in 2021, making the need for mental health services more urgent than ever.

ALSO READ: NBC’s Saving Campaign Empowers Customers Nationwide

Unfortunately, the country’s ability to address this growing challenge is hindered by a shortage of mental health professionals, infrastructure, medical equipment and essential medication.

For example, out of the 28 regions in the country, only five have facilities that provide adequate mental health services.

The most affected group is the youth aged 15 to 39, who represent the nation’s workforce, underscoring the need for intensified efforts to safeguard this generation for Tanzania’s future well-being and development.

Mr Kafu said by improving mental health services, Exim aims to contribute to the creation of a network of communities that can access care quickly and affordably.

Exim Insurance Department Manager Tike Mwakyoma said they are appreciating the support from partners in the insurance industry, who have stood by them since the last festival.

“Let’s continue this unity for the development of all Tanzanians and our nation as a whole,” the manager said.

Source: allafrica.com

Continue Reading