Jeshi la Polisi lakanusha taarifa ya Polisi

Jeshi la Polisi lakanusha taarifa ya Polisi

Dar es Salaam. Sakata la kuzuiwa mikutano ya hadhara na ile ya ndani ya vyama vya siasa limechukua sura mpya, baada ya Jeshi la Polisi Tanzania kukanusha zuio la Polisi Wilaya ya Mbagala, Mkoa wa Dar es Salaam.

Kanusho hilo la Polisi Makao Makuu linatokana na taarifa ya Polisi Mbagala kwenda kwa chama cha ACT-Wazalendo kuzuia kufanyika kwa mkutano wa hadhara waliopanga kufanyika leo Jumatatu, Agosti 12, 2024 katika Kata ya Charambe, Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam.

Barua ya Polisi Wilaya ya Mbagala kwenda kwa ACT-Wazalendo ya leo Jumatatu, pamoja na mambo mengine imesema: “…napenda kukujulisha kuwa mikutano yote ya hadhara na ya ndani imezuiliwa hadi hapo yatakapotolewa maelekezo mengine.”

Baada ya barua hiyo mijadala imeshika kasi mitandaoni, huku wadau wa kisiasa wakikumbusha kile kilichotokea mwaka 2016 kwa mikutano ya hadhara kupigwa marufuku na kuruhusiwa ile ya ndani.

Zuio hilo la mikutano liliwekwa wakati wa utawala wa awamu ya tano, baada ya utawala wa awamu ya sita kuingia madarakani ukiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan uliliondoa na mikutano kurejea.

Mwananchi lilizungumza na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kutaka kujua undani wa zuio hilo la Polisi Mbagala ambapo amesema kinachojitokeza ni hali ya jeshi hilo kujichanganya, hakuna tamko rasmi lilotolewa la kufuta mikutano ya hadhara na ile ya ndani.

“Kilichotokea naona kama Polisi wamejichanganya, hakuna tamko rasmi lilotolewa la kuzuia mikutano ya hadhara na ya ndani kwa kuwa Jeshi la Polisi lina ngazi aulizwe msemaji wake anaweza kuwa na majibu sahihi,” amesema Jaji Mutungi.

Katikati ya mijadala hiyo, saa 8:20 mchana, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime akatoa taarifa kwa umma akisema: “Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa kuwa halijapiga marufuku kufanyika mikutano ya nje ya hadhara na ile ya ndani, ili mradi inafuata matakwa ya sheria za nchi.”

“Kilichopigwa marufuku ni mkusanyiko uliokuwa umeitishwa na viongozi wa Chadema huko jijini Mbeya, kwa kivuli cha kuadhimisha Siku ya Vijana Duniani,”ilieleza taarifa hiyo.
 

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading

Tanzania's opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Tanzania’s opposition party ACT Wazalendo honours veteran politician under new policy

Unguja. Opposition party ACT Wazalendo today officially bids farewell to its former Chairman, Juma Duni Haji, also known as Babu Duni, as part of a new policy designed to honor retired senior leaders at a ceremony held at Kiembesamaki, Zanzibar.

The initiative highlights the party’s commitment to recognizing and supporting individuals who have served with dedication and integrity.

Babu Duni, who stepped down earlier this year, was succeeded by Othman Masoud, now the First Vice President of Zanzibar.

The policy aims to provide ongoing respect and support to retired leaders, ensuring their continued recognition and contribution to the party’s development.

“Recognizing their significant contributions to the development and prosperity of the party, this policy ensures that retired leaders continue to be acknowledged and respected by both the party and the community,” the policy states.

To benefit from this policy, leaders must not have left or been expelled from the party. They must have served the party with honor and dedication. The national leadership committee will determine whether a leader has fulfilled these criteria.

The policy seeks to honor retired leaders, protect their dignity, acknowledge their contributions, leverage their ideas for the party’s growth, and support them to the best of the party’s ability.

In honoring these leaders, the party will provide a vehicle, the type of which will be determined by the national leadership committee. Additionally, they will receive a monthly allowance, with the amount also set by this committee.

Other benefits include health insurance. If a leader does not own a home, the party will cover their rent at a rate decided by the committee.

The leadership committee may also grant special recognition based on the leader’s contributions. Retired leaders will participate in decision-making meetings according to procedures outlined in the party’s constitution.

Depending on the party’s resources at the time, the policy may also apply to retired deputy chairpersons for both the mainland and Zanzibar, the Secretary-General, Deputy Secretary-General for both mainland and Zanzibar, and the party’s Attorney General.

Additionally, leaders, executives, or members with exceptional contributions to the party’s protection, advocacy, and defense may also benefit, as determined by the leadership committee.

Currently, those who are eligible for benefits under this policy include Juma Duni Haji (retired party Chairman) and Zitto Kabwe (retired party leader).Continue Reading