EU yamwaga Sh17.8 bilioni kuimarisha demokrasia, utawala wa sheria nchini

EU yamwaga Sh17.8 bilioni kuimarisha demokrasia, utawala wa sheria nchini

EU yamwaga Sh17.8 bilioni kuimarisha demokrasia, utawala wa sheria nchini

Dar es Salaam. Jumuiya ya Ulaya (EU) imetoa ufadhili wa zaidi ya Sh17. 8 bilioni kwa asasi za kiraia 11 nchini Tanzania, kwa lengo la kukuza demokrasia kwa kujenga jamii yenye uwazi, haki, na ujumuishi zaidi, kwa kuimarisha sauti za wananchi na taasisi.

Ufadhili huo wa miaka mitatu uliotolewa kupitia Mpango wa Asasi za Kiraia na Mpango wa Fedha kwa Ukuaji, umezingatia maeneo muhimu kama utawala bora, uhuru wa vyombo vya habari, uwezeshaji wa vijana, na uwajibikaji wa kifedha wa umma.

Akizungumza wakati wa kutoa ruzuku hizo leo Februari 14, Mkuu wa EU Tanzania, Marc Stalmans amesema asasi za kiraia ni kiungo muhimu kwa jumuiya hiyo na katika jamii.

“Tunazungumzia vita, uhalifu wa kiuchumi, tunazungumzia kuibuka kwa watu wenye misimamo mikali, tunazungumza zaidi na zaidi kuhusu ugumu wa kuchapisha kile ulichonacho.

“Kwa hiyo ni muhimu kuweka mshikamano na watu wa Afrika na ni muhimu kwa azaki kuwa pamoja nasi, kwani zinakuza demokrasia na ni sauti ya wanajamii,” amesema.

Amesema wanatarajia kuona asasi za kiraia zikipigania utawala bora, usimamizi wa fedha, demokrasia na utawala wa sheria.

“Sisi Umoja wa Ulaya tunashiriki tunu za kimataifa ambazo ni utawala wa sheria, demokrasia, ustawi wa wanawake na vijana katika jamii.

“Tulipoamua kujipanga upya mwaka 2021 tuliweka mambo mawili, kwanza haki za binadamu na demokrasia na pili kuwa pamoja na Azaki na mashirika yasiyo ya kiserikali,” amesema.  

Amezitaka Azaki zilizopewa ufadhili kutumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Balozi wa EU nchini Tanzania, Christine Grau amesema ruzuku hiyo inalenga kujenga ushirikiano unaotegemea uaminifu, matarajio ya pamoja na dhamira ya kutoa sauti kwa wale ambao mara nyingi husahaulika.

“Asasi za kiraia zenye nguvu ni nguzo muhimu zinahakikisha uwajibikaji, zinaboresha utawala wa kidemokrasia, na zinaimarisha jamii zetu,” amesema.

Akizungumzia ufadhili huo, Fausta Musokwa, Meneja wa Programu ya Kimataifa ya ufadhili wa vyombo vya habari (IMS Tanzania), amesema

“Sasa zaidi ya wakati wowote, uandishi wa habari bora ni muhimu sio tu kwa kupambana na hotuba za chuki na habari potofu, bali pia kwa kusaidia kujenga jamii yenye uwazi, uwajibikaji, na demokrasia nchini Tanzania,” amesema

Arafat Lesheve, kiongozi kijana kutoka mradi wa Vijana Plus ukiongozwa na Save the Children na Tanzania Bora Initiative, amesema watafaidika kwa kukuza sauti za vijana.

“Kupitia mpango huu, sisi vijana sio tu washauri; bali ni wabunifu wa suluhisho na waelimishaji wenzao. Kuwezesha mashirika yanayoongozwa na vijana ni sawa na kuwezesha mustakabali wetu,” amesema.

Mradi mwingine uliofadhiliwa ni wa utetezi wa haki za binadamu kupitia Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki na Chama cha Wanasheria wa Afrika (PALU), na Chama cha Wanasheria Wanawake wa Zanzibar (Zafela).

“Kutetea haki, kuimarisha haki na kupanua nafasi ya kiraia mpango huu unawawezesha wananchi, wataalamu wa sheria, na asasi za kiraia kusimamia utawala wa sheria na kuimarisha uwajibikaji nchini Tanzania,” amesema Onesmo Olengurumwa, Mratibu wa Kitaifa wa THRDC.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading