Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dar es Salaam. Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Dorothy Semu amesema alishtuka baada ya kuona wanatengwa kwa makundi baada ya kuzuiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro jijini Luanda, Angola.

Semu, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Othman Masoud ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar na Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu walizuiwa na mamlaka za Angola kuingia nchini humo jana Machi 13, 2025.

Si hao pekee, bali hata viongozi wengine mashuhuri wakiwemo marais wastaafu kutoka Botswana na Colombia, Waziri Mkuu mstaafu wa Lesotho na baadhi ya wakuu wa vyama vya siasa kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika walikumbwa na kadhia hiyo.

Viongozi hao, pamoja na wanaotoka mataifa mbalimbali yakiwemo ya Uganda, Botswana na Kenya walikwenda Angola kushiriki mazungumzo ya Jukwaa la Demokrasia Afrika (PAD). Mazungumzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya The Brenthurst Foundation.

Lengo la jukwaa hilo ni kuwaleta pamoja wanademokrasia wa Afrika ili kutafakari kuhusu demokrasia na kubadilishana uzoefu na mikakati ya kuimarisha demokrasia.

Semu aliyerejea nchini usiku wa kuamkia leo Ijumaa, Machi 14, 2025 amesema kundi lao liliwasili uwanjani hapo kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia lakini walilazimishwa kurejea nyumbani kwa ndege hiyohiyo.

“Kwanza tulikuwa tumechoka sana, kwa sababu tulisafiri takribani saa nane kutoka Dar es Salaam hadi Addis Ababa, kisha Luanda.

“Kwa uzoefu wa nchi za Afrika, ulipoanza mchakato wa kukusanya hati zetu za kusafiria na kuanza kuitwa wachache pembeni, kisha kuamriwa ‘kaa hapa’, baada ya muda unaona wenzako kwenye msafara wa kueleka Benguela wanaongezwa katika kundi, nilijua kuna tatizo,” amesema.

Semu akizungumza na Mwananchi leo Machi 14, amesema jambo jingine lililowafanya kujua kama kuna tatizo ni viongozi wakiwemo wanasiasa mashuhuri kutopitishwa eneo la VIP (wageni mashuhuri) wala kupokewa na watu wa Serikali na uhamiaji.

“Nilivyoona kundi letu limetangulizwa, hisia zikanijia kuna kitu hakipo sawa, tukajiuliza kwa nini tupo hivi? Mwanzoni tuliitwa kundi la watu watano, akiwemo waziri mkuu mstaafu wa Lessotho.

“Sasa tulipoanza kupitishwa kwenye korido za uwanja wa ndege na kila tukijaribu kuwauliza watuambie kitu gani tumekosea, hatukupewa ushirikiano. Niliamua kuwa mtulivu kwa sababu nipo Afrika na kazi ninayoifanya ni ya siasa na demokrasia,” amesema.

Amesema aliamua kuwa mpole baada ya sintofahamu hiyo, akitambua yupo nchi ya watu na kazi anayoifanya ni kuzungumzia masuala ya wananchi.

“Nilijua kuna shida, sikuwa na wasiwasi kwa sababu tumezoea mambo ya maagizo kutoka juu, kwa sababu kila mtu alikuwa anasema ameagizwa, tulisubiri kuona maagizo yataendelea hadi wapi.

“Ni kama vile walikuwa wanatusubiri na walishapanga, lazima tuondoke,” amesema Semu.

Amesema msafara wa ACT-Wazalendo, ulikuwa na yeye, Othman, Katibu wa Haki za Binadamu na Makundi Maalumu, Pavu Abdallah na Naibu Katibu wa Mambo ya Nje, Dk Nasra Nassor Omar.

“Mimi pamoja na Dk Nasra na Pavu tuliopanda ndege ya Ethiopia, tumesharejea Tanzania. Wakati tunakuwa deported (tunarejeshwa) tuliwaacha wenzetu (Othman na msafara wake) mambo yao yakiendelea, kwa sababu tulilazimishwa kurudi na ndege iliyotupeleka ndani ya saa mbili tulikuwa tayari tumeishaingia kwenye ndege.

“Hatukujua kilichoendelea huko nyuma maana tulikwenda kwanza Addis Ababa kisha Dar es Salaam,” amesema Semu.

Dk Nasra ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa ACT-Wazalendo, amesema kabla ya kufika eneo la uhamiaji baada ya kushuka kwenye ndege, walipanga foleni kusubiri taratibu za ukaguzi, lakini katikati ya eneo la dawati la uhamiaji, palikuwa na ofisa wa Angola.

“Ofisa huyo ndiye aliyekuwa akichukua hati zetu za kusafiria, baada ya kuchukuliwa hati zetu tuliwakuta wenzetu (Othman), pamoja na marais wastaafu kutoka mataifa mbalimbali waliowekwa pembeni.

“Tulijua wamewekwa pembeni ili kusubiria taratibu za kuchukuliwa, kwa sababu ukiona marais au viongozi wengine wamesimamishwa pembeni. Tulifanya mazungumzo nao ya kawaida kwa muda saa mbili, kabla ya kuanza kutenganishwa,” amesema.

Dk Nasra amesema baadaye waliwekwa kwenye ukumbi bila kuelezwa chochote, kisha wakarejeshwa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Chief Editor

Insecurity prompts Zanzibar to review its lucrative island leasing

The Tanzanian central government is planning to boost its security presence in the Zanzibar archipelago. A commission tasked with auditing the country’s security forces was appointed in July by President Samia Suluhu Hassan. It says it is concerned about the situation in the country’s Indian Ocean islands that are under the control of the semi-autonomous Zanzibar local government.Continue Reading

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading