Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dorothy Semu asimulia walivyozuiwa kwa saa nane Angola

Dar es Salaam. Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Dorothy Semu amesema alishtuka baada ya kuona wanatengwa kwa makundi baada ya kuzuiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Quatro de Fevereiro jijini Luanda, Angola.

Semu, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, Othman Masoud ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar na Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu walizuiwa na mamlaka za Angola kuingia nchini humo jana Machi 13, 2025.

Si hao pekee, bali hata viongozi wengine mashuhuri wakiwemo marais wastaafu kutoka Botswana na Colombia, Waziri Mkuu mstaafu wa Lesotho na baadhi ya wakuu wa vyama vya siasa kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika walikumbwa na kadhia hiyo.

Viongozi hao, pamoja na wanaotoka mataifa mbalimbali yakiwemo ya Uganda, Botswana na Kenya walikwenda Angola kushiriki mazungumzo ya Jukwaa la Demokrasia Afrika (PAD). Mazungumzo hayo yaliandaliwa na Taasisi ya The Brenthurst Foundation.

Lengo la jukwaa hilo ni kuwaleta pamoja wanademokrasia wa Afrika ili kutafakari kuhusu demokrasia na kubadilishana uzoefu na mikakati ya kuimarisha demokrasia.

Semu aliyerejea nchini usiku wa kuamkia leo Ijumaa, Machi 14, 2025 amesema kundi lao liliwasili uwanjani hapo kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia lakini walilazimishwa kurejea nyumbani kwa ndege hiyohiyo.

“Kwanza tulikuwa tumechoka sana, kwa sababu tulisafiri takribani saa nane kutoka Dar es Salaam hadi Addis Ababa, kisha Luanda.

“Kwa uzoefu wa nchi za Afrika, ulipoanza mchakato wa kukusanya hati zetu za kusafiria na kuanza kuitwa wachache pembeni, kisha kuamriwa ‘kaa hapa’, baada ya muda unaona wenzako kwenye msafara wa kueleka Benguela wanaongezwa katika kundi, nilijua kuna tatizo,” amesema.

Semu akizungumza na Mwananchi leo Machi 14, amesema jambo jingine lililowafanya kujua kama kuna tatizo ni viongozi wakiwemo wanasiasa mashuhuri kutopitishwa eneo la VIP (wageni mashuhuri) wala kupokewa na watu wa Serikali na uhamiaji.

“Nilivyoona kundi letu limetangulizwa, hisia zikanijia kuna kitu hakipo sawa, tukajiuliza kwa nini tupo hivi? Mwanzoni tuliitwa kundi la watu watano, akiwemo waziri mkuu mstaafu wa Lessotho.

“Sasa tulipoanza kupitishwa kwenye korido za uwanja wa ndege na kila tukijaribu kuwauliza watuambie kitu gani tumekosea, hatukupewa ushirikiano. Niliamua kuwa mtulivu kwa sababu nipo Afrika na kazi ninayoifanya ni ya siasa na demokrasia,” amesema.

Amesema aliamua kuwa mpole baada ya sintofahamu hiyo, akitambua yupo nchi ya watu na kazi anayoifanya ni kuzungumzia masuala ya wananchi.

“Nilijua kuna shida, sikuwa na wasiwasi kwa sababu tumezoea mambo ya maagizo kutoka juu, kwa sababu kila mtu alikuwa anasema ameagizwa, tulisubiri kuona maagizo yataendelea hadi wapi.

“Ni kama vile walikuwa wanatusubiri na walishapanga, lazima tuondoke,” amesema Semu.

Amesema msafara wa ACT-Wazalendo, ulikuwa na yeye, Othman, Katibu wa Haki za Binadamu na Makundi Maalumu, Pavu Abdallah na Naibu Katibu wa Mambo ya Nje, Dk Nasra Nassor Omar.

“Mimi pamoja na Dk Nasra na Pavu tuliopanda ndege ya Ethiopia, tumesharejea Tanzania. Wakati tunakuwa deported (tunarejeshwa) tuliwaacha wenzetu (Othman na msafara wake) mambo yao yakiendelea, kwa sababu tulilazimishwa kurudi na ndege iliyotupeleka ndani ya saa mbili tulikuwa tayari tumeishaingia kwenye ndege.

“Hatukujua kilichoendelea huko nyuma maana tulikwenda kwanza Addis Ababa kisha Dar es Salaam,” amesema Semu.

Dk Nasra ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa ACT-Wazalendo, amesema kabla ya kufika eneo la uhamiaji baada ya kushuka kwenye ndege, walipanga foleni kusubiri taratibu za ukaguzi, lakini katikati ya eneo la dawati la uhamiaji, palikuwa na ofisa wa Angola.

“Ofisa huyo ndiye aliyekuwa akichukua hati zetu za kusafiria, baada ya kuchukuliwa hati zetu tuliwakuta wenzetu (Othman), pamoja na marais wastaafu kutoka mataifa mbalimbali waliowekwa pembeni.

“Tulijua wamewekwa pembeni ili kusubiria taratibu za kuchukuliwa, kwa sababu ukiona marais au viongozi wengine wamesimamishwa pembeni. Tulifanya mazungumzo nao ya kawaida kwa muda saa mbili, kabla ya kuanza kutenganishwa,” amesema.

Dk Nasra amesema baadaye waliwekwa kwenye ukumbi bila kuelezwa chochote, kisha wakarejeshwa.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania: Samia Hands Over NBC’s 354m/ – Crop Insurance Compensation to Farmers Affected By Hailstorms

President Samia Suluhu Hassan, has handed over a cheque of 354m/- from the National Bank of Commerce (NBC) as compensation to tobacco farmers, who were affected by hailstorms during the previous farming season in various regions across the country.

Handing over the cheque in Dodoma, the compensation is part of the crop insurance service provided by NBC in collaboration with the National Insurance Corporation (NIC).

Furthermore, President Samia has also handed over health insurance coverage to members of the Lindi Mwambao Cooperative Union based in Lindi Region, through the Farmers’ Health Insurance service provided by the bank in partnership with Assurance Insurance Company.

While visiting the bank’s pavilion at the Nanenane Agricultural Exhibition and being received and briefed by the bank’s Managing Director, Mr. Theobald Sabi, she said: “This crop insurance is one of the crucial solutions in ensuring farmers have a reliable income, without fear of challenges such as natural disasters, including hailstorms.

“I call upon all farmers in the country to make the best use of this important opportunity by accessing these kinds of insurance services. I also highly commend NBC and all the stakeholders participating in this programme.”

Elaborating further on the crop insurance service, the Minister of Agriculture, Hussein Bashe, stated that it will help to recover the loss farmers incurred, especially in various calamities beyond their control.

Citing them as floods, fires, and hailstorms, which have significantly affected the well-being of farmers and caused some to be reluctant to invest in the crucial sector, Mr Bashe added: “However, our President, this step by NBC is just the beginning, as this is the second year since they started offering this service, and the results are already visible.

“As the government, we promise to continue supporting the wider implementation of this service, with the goal of ensuring that this crop insurance service reaches more farmers.”

ALSO READ: NBC participates in TFF 2023/24 awards, promises to enhance competition

On his part, Mr Sabi said that the farmers who benefited from the compensations are from 23 primary cooperative unions in the regions of Shinyanga, Geita, Tabora, Mbeya, Katavi, and Kigoma.

He added: “In addition to these insurance services, as a bank, through this exhibition, we have continued with our programme of providing financial education and various banking opportunities to farmers, alongside offering them various loans, including loans for agricultural equipment, particularly tractors, to eligible farmers.:

At the NBC booth, President Samia also had the opportunity to be briefed on the various services offered by the bank to the farmers namely crop insurance and health insurance services.

There, the President had the chance to speak with some of the beneficiaries of the services, including the Vice-Chairman of the Lindi Mwambao Primary Cooperative Union, Mr. Hassan Mnumbe, whose union has been provided with a health insurance card from the bank.

Source: allafrica.com

Continue Reading