Dorothy ajitosa kupambana na Samia

Dorothy ajitosa kupambana na Samia

Dorothy ajitosa kupambana na Samia

Dar es Salaam. Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Dorothy Semu ametangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu, akitaja mambo manne yaliyomsukuma kuitaka nafasi hiyo.

Iwapo atapitishwa na chama chake kuwania nafasi hiyo, atakuwa mgombea wa mwingine mwanamke katika uchaguzi wa mwaka huu. Anatarajiwa kuchuana na Rais Samia Suluhu Hassan wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Semu ametangaza nia kuwania nafasi hiyo leo Januari 16, 2025 ikiwa ni siku moja baada ya chama hicho kuwaalika wanachama kujitokeza kutangaza nia za kuwania nafasi za udiwani, ubunge na urais katika uchaguzi wa Oktoba, mwaka huu.

Amesema katika kipindi cha miaka kadhaa iliyopita, Taifa limekumbwa na changamoto zilizosababisha kudumaa kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

“Pamoja na ujio wa 4R za Rais Samia Suluhu Hassan, kuna upungufu mkubwa unaohitaji uongozi thabiti, wa uwazi na wenye malengo halisi kwa manufaa ya Watanzania wote,” amesema.

Ametaja mambo yanayohitaji uongozi thabiti kuwa ni kushuka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi, kupanda kwa gharama za maisha, changamoto za ajira kwa vijana na Serikali ya CCM chini ya Rais Samia kuwa na udhaifu katika usimamizi wa rasilimali za Taifa.

Amesema licha ya Serikali kueleza uchumi unakua, ripoti ya Benki ya Dunia ya mwaka 2024 inaonyesha kasi ya ukuaji wa uchumi imeshuka kutoka asilimia 6.8 mwaka 2019 hadi asilimia 4.6 mwaka 2023, akidai hali hiyo inasababishwa na sera zisizo thabiti za uwekezaji na utekelezaji hafifu wa miradi ya maendeleo.

Amesema takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kiwango cha mfumuko wa bei kimefikia asilimia 5.6 mwaka 2023, ikilinganishwa na asilimia 3.5 mwaka 2020, hali aliyodai inaendelea kujirudia na inaathiri uwezo wa wananchi kumudu mahitaji ya msingi, hususani vyakula na huduma za afya.

“Kwa mujibu wa ripoti ya Taasisi ya Utafiti na kupunguza Umasikini Tanzania (REPOA) ya 2019, takribani vijana milioni moja wanahitimu kila mwaka huku idadi inayoajiriwa serikalini na sekta binafsi ni 250,000, kwa wastani wa kila mhitimu anatumia wastani miaka 5.5 kupata ajira,” amesema.

Amesema Serikali imeshindwa kuwekeza vya kutosha katika sekta zinazoweza kuzalisha ajira kama kilimo, viwanda, na teknolojia, hivyo akipata ridhaa ya chama chake, atahakikisha anasimamia vyema eneo hilo kuwezesha vijana kujiajiri na kuajiriwa.

Amesema Tanzania inahitaji uongozi mpya utakaolinda masilahi ya Taifa na uchumi imara, jamii yenye fursa sawa na uongozi wa uwazi.

Anavyoweza kuwa Rais

Semu amesema uzoefu alionao kwenye uongozi ni turufu anayoamini itambeba.

“Nipo kwenye uongozi na kwenye siasa kwa miaka 10 naamini nimeiva, pia nipo kwenye chama chenye sera na ilani bora, kinaonyesha tofauti na kujisimamia chenyewe.

“ACT ina miaka 10 tangu kuanzishwa, kinazidi kukua kwa kasi na kutekeleza masuala mbalimbali kama chama makini chenye mikakakati bora na endelevu. Mikakati hii inatuongoza katika hatua ya kwenda kushika dola na itatuletea matokeo bora na kutupa majimbo ya kutosha kuunda Serikali,” amesema.

Wadau wa siasa

Mchambuzi wa masuala ya siasa, Dk Richard Mbunda amesema alichofanya Semu ni demokrasia na ni haki ya mtu mwenye vigezo kudhani anaweza kugombea hiyo nafasi.

“Hapo sasa ni jukumu la chama chake kumpitisha ili atimize azma yake hiyo, ukiangalia siasa za Semu na alivyokuwa Anna Mghwira (aliwahi kugombea urais) ni watu ambao wanafanana katika kujenga hoja na masuala mengine ya kisiasa,” amesema.

Amesema Semu kama atapata fursa hiyo bila shaka atatoa changamoto ya kutosha kwenye uchaguzi huo ambao suala la usawa wa kijinsia litapewa kipaumbele.

Mwanasiasa mkongwe, Hashimu Rungwe amesema Semu yuko sahihi kutangaza nia kwa kuwa amejipima na kuona anatosha kugombea.

“Ni haki yake na yupo sahihi, ajaribu aone, chama chake kikimpitisha na uchaguzi mkuu ukawa huru na wa haki anaweza kufanya kitu,” amesema Rungwe.

Semu ni nani

Semu aliamua kuacha kazi kama mtumishi wa umma katika Wizara ya Afya na kuingia kwenye siasa, akilenga kushiriki michakato itakayochochea mabadiliko yatakayoleta maisha bora kwa wananchi.

Wasifu wake kama mtaalamu wa tiba  mazoezi, ulimfanya anafanikiwe kuajiriwa serikalini na kabla ya kuingia rasmi kwenye siasa, amefanya kazi wizarani kwa miaka 12 mfululizo kama ofisa wa programu ya kifua kikuu na ukoma nchini, ndipo akaamua kuacha kazi.

Dorothy aliyezaliwa mwaka 1975 alipata Shahada ya Uzamili katika tiba ya mazoezi ya mwili (Physiotherapy) kutoka Chuo Kikuu cha Western Cape, Afrika Kusini.

Kazi zake zilihusisha kutibu wagonjwa na kusimamia programu za afya, hasa katika eneo la kudhibiti ulemavu wa ukoma.

Dorothy ndani ya ACT-Wazalendo amefanya kazi akiwa Katibu wa Sera na Utafiti wa chama hicho.

Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo kati ya mwaka 2017 na 2020, kisha alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo (Bara).

Amekuwa Waziri Mkuu Kivuli wa ACT-Wazalendo kuanzia mwaka 2020 mpaka mwaka 2022.

Machi 6, 2024 alichaguliwa kuwa Kiongozi wa ACT-Wazalendo, akichukua nafasi ya Zitto Kabwe aliyemaliza muda wake.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Popular
Swahili News Editor

MGAO WA MAJI WAWATESA WAZANZIBARI

Wananchi wengi hasa katika maeneo ya Mjini Unguja, wanalalamikia ukosefu wa maji safi na salama huku Mamlaka ya Maji Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ujuzi na wataalam katika masuala ya uandisi wa Maji na fani nyengine.Continue Reading

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

‘No Marburg Confirmed In Tanzania’, But Mpox Remains ‘Public Health Emergency’

Monrovia — The Director General of the African Centers for Disease Control, Jean Kaseya, has said the center stands ready to support Tanzania and other countries in the region where suspected cases of the infectious Marburg Virus Disease have been identified. The World Health Organization earlier this week issued an alert warning of a possible outbreak in the country, although the Tanzanian Health Ministry has said tests conducted on available samples did not show the existence of Marburg in the East African nation.

“As of the 15 of January 2025, laboratory results from all suspected individuals were negative for Marburg Virus,” Tanzanian Health Minister Jenista Mhagama said in a statement. This would have marked the country’s second experience with the highly infectious disease that recently killed over a dozen people in neighboring Rwanda. Tanzania previously reported an outbreak of Marburg in 2023 in the  Kegara region, said to have been the epicenter of the new suspected cases.

At the Africa CDC online briefing on Thursday, Kaseya also said another infectious disease, Mpox, “remains a public health concern”. He said that while in December 2024, the disease had afflicted 20 countries, a new country – Sierra Leone – has been added to the number after recent outbreak there. Sierra Leonean health authorities said on January 10 that two cases of Mpox had been confirmed in the country and dozens of contacts are being traced.

With thousands of confirmed cases of Mpox across Africa and more than 1000 people having died of the disease  – mainly in Central Africa – Kaseya emphasized the need to increase testing, a theme he’s heralded before. The Africa CDC boss said over the next few months the continental health watchdog will deploy additional epidemiologists and community health workers to areas considered hot spots of infectious diseases in the region.

Source: allafrica.com

Continue Reading