Dk Mwinyi ataka wimbo mmoja wa amani, mshikamano 2025

Dk Mwinyi ataka wimbo mmoja wa amani, mshikamano 2025

Dk Mwinyi ataka wimbo mmoja wa amani, mshikamano 2025

Unguja. Wakati Watanzania leo wakiuaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka 2025, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani na mshikamano.

Amesema mwaka 2025 ni wa uchaguzi mkuu, hivyo ni wajibu wa viongozi wa kisiasa, taasisi za kijamii, viongozi wa dini na wananchi wote kukumbushana umuhimu wa kudumisha na kuilinda amani ya nchi, kwa lengo kuu moja la maendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Katika hotuba yake aliyoitoa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari jana, Dk Mwinyi amesema ni jambo la kujivunia kuona wananchi wanauaga mwaka wakiwa na amani na utulivu huku kukiwa na maendeleo makubwa ambayo Zanzibar imeyapata. 

Rais huyo amesema, itakumbukwa Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, tukio alilosema ni la muhimu la kidemokrasia linalowawezesha wananchi kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka.

“Serikali zote mbili; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kupitia Tume za Uchaguzi (NEC na ZEC), zimeanza kuchukua hatua za maandalizi ili kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa misingi ya haki na sheria,” amesema Rais Mwinyi.

Rais huyo ametumia fursa ya kuuaga mwaka kutoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanadumisha amani nchini kabla, wakati, na baada ya uchaguzi,” amesema.

Miradi ya maendeleo

Kwa mujibu wa Dk Mwinyi, kutokana na misingi ya amani, mshikamano na umoja, nchi imepata mafanikio makubwa katika kukuza uchumi, kuimarisha miundombinu, biashara na uwekezaji, huduma za jamii, pamoja na kuimarisha demokrasia na utawala bora.

“Tumepata mafanikio makubwa katika kukuza uchumi kwa kuongeza udhibiti na ukusanyaji wa mapato na kuimarisha uwekezaji na biashara,” amesema Dk Mwinyi.

Aidha, amesema mafanikio makubwa yameonekana katika ujenzi wa barabara mijini na vijijini, viwanja vya ndege na bandari, nyumba za makazi, pamoja na usambazaji wa huduma za umeme na maji safi bila kusahau sekta ya elimu na afya alizosema zimeendelea kuimarishwa karibia Zanzibar nzima.

“Tumefanikiwa kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia programu za utoaji wa mikopo nafuu na kuanzisha masoko ya kisasa ya Mwanakwerekwe na Jumbi,” ameongeza.

Hata hivyo, amewashukuru wananchi, viongozi wa serikali, viongozi wa dini, asasi za kiraia, sekta binafsi na washirika wa maendeleo kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha mipango ya maendeleo kwa mwaka unaomalizika wa 2024.

Pia ametoa shukrani maalumu kwa Rais Samia Suluhu Hassan na watendaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushirikiano wao.

“Naomba tuendeleze ushirikiano huu kwa mwaka mpya ili tuzidi kupiga hatua za maendeleo katika kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa jamii yetu,” amesema.

Akizungumzia sekta ya michezo, Dk Mwinyi amesema jitihada kubwa zimefanyika katika kuimarisha sekta ya michezo kwa ukarabati wa viwanja vya Amani Complex na Gombani, sambamba na ujenzi wa viwanja vipya vya michezo.

Amesema jitihada hizo zinalenga kuimarisha sekta ya michezo na kuchochea utalii kupitia matamasha na mashindano ya kimataifa.

Hivyo, amesema Serikali inalenga kuwa na miundombinu inayokidhi mahitaji ya mashindano ya CHAN kwa mwaka 2025 na Afcon mwaka 2027, yatakayoshirikisha Tanzania, Kenya na Uganda.

Maadhimisho ya Mapinduzi

Kutokana na umuhimu wa Mapinduzi ya mwaka 1964, Dk Mwinyi amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika sherehe za miaka 61 ya Mapinduzi Januari 12, 2025.

Matukio hayo yatashirikisha uzinduzi wa miradi ya maendeleo, uwekaji wa mawe ya msingi, michezo, na shughuli za kitamaduni. Sherehe hizi zitafikia kilele chake Januari 12, 2025, katika Uwanja wa Gombani, Pemba.

“Sherehe hizi ni zetu sote, hivyo nawakaribisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kuzifanikisha,” amesema.

Tunapouaga mwaka 2024 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2025, tunao wajibu wa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kudumisha amani, mshikamano, na umoja wa kitaifa katika nchi yetu.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Britam half-year net profit hits Sh2bn on higher investment income

Insurer and financial services provider Britam posted a 22.5 percent jump in net earnings for the half-year ended June 2024, to Sh2 billion, buoyed by increased investment income.

The rise in half-year net profit from Sh1.64 billion posted in a similar period last year came on the back of net investment income rising 2.5 times to Sh13.27 billion from Sh5.3 billion.

“We are confident in the growth and performance trend that Britam has achieved, supported by its subsidiaries in Kenya and the region. Our business is expanding its revenue base while effectively managing costs,” Britam Chief Executive Officer Tom Gitogo said.

“Our customer-centric approach is fueling growth in our customer base and product uptake, particularly through micro-insurance, partnerships, and digital channels.”

The investment income growth was fueled by interest and dividend income rising 34 percent to Sh9.1 billion, which the insurer attributed to growth in revenue and the gains from the realignment of the group’s investment portfolio.

Britam also booked a Sh3.79 billion gain on financial assets at a fair value, compared with a Sh1.8 billion loss posted in a similar period last year.

The increased investment income helped offset the 12.7 percent decline in net insurance service result to Sh2.13 billion in the wake of claims paid out rising at a faster pace than that of premiums received.

Britam said insurance revenue, which is money from written premiums, increased to Sh17.8 billion from Sh16.6 billion, primarily driven by growth in the Kenya insurance business and regional general insurance businesses, which contributed 30 percent of the revenue.

The group has a presence in seven countries in Africa namely Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, South Sudan, Mozambique, and Malawi.

Britam’s insurance service expense hit Sh13.6 billion from Sh11.3 billion, while net insurance finance expenses rose 2.6 times to Sh12.3 billion during the same period.

“Net insurance finance expenses increased mainly due to growth in interest cost for the deposit administration business driven by better investment performance. This has also been impacted by a decline in the yield curve, which has led to an increase in the insurance contract liabilities. The increase has been offset by a matching increase in fair value gain on assets,” said Britam.

Britam’s growth in profit is in line with that of other Nairobi Securities Exchange-listed insurers, which have seen a rise in profits.

Jubilee Holdings net profit in the six months increased by 22.7 percent to Sh2.5 billion on increased income from insurance, helping the insurer maintain Sh2 per share interim dividend.

CIC Insurance Group posted a 0.64 percent rise in net profit to Sh709.99 million in the same period as net earnings of Liberty Kenya nearly tripled to Sh632 million from Sh213 million, while Sanlam Kenya emerged from a loss to post a Sh282.2 million net profit.

Continue Reading