Dk Mwinyi ataka safari za ATCL Zanzibar kukuza uchumi

Dk Mwinyi ataka safari za ATCL Zanzibar kukuza uchumi

Unguja/Dar. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Mwinyi amelitaka Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kuangalia zaidi safari zitakazopitia Zanzibar ili kukuza uchumi.

Kwa mujibu wa Dk Mwinyi, hatua hiyo itawezesha kuvutia watalii wanaotembelea vivutio vilivyopo Zanzibar na Tanzania kwa jumla.

Rais Mwinyi ametoa kauli hiyo leo Agosti 20, 2024 alipohutubia wananchi katika hafla ya mapokezi ya ndege aina ya Boeing 878-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sheikh Abeid Amani Karume.

Amesema ni muhimu shirika hilo likaangalia zaidi safari za ndege zinazopitia Zanzibar ili kuvutia watalii wanaotembelea vivutio vilivyopo.

“Serikali itaendelea kusimamia sera na sheria za usimamizi wa anga ili kuona mashirika mengi yanafanya safari hapa nchini kwa manufaa ya uchumi wa nchi,” amesema.

Kuendelea kukua kwa kasi kwa sekta ya utalii nchini na kuongezeka kwa faida inayotokana na uchumi wa buluu, amesema kunategemea ufanisi wa ATCL.

Amesema kuwepo kwa usafiri wa anga wa uhakika unaoendana na mikakati ya kukuza uchumi ni muhimu.

“Hapa nataka nisisitize umuhimu wa kufanya safari za ndege kati ya Pemba na sehemu nyingine za nchi yetu kutokana na umuhimu wa fursa za utalii zilizopo huko, ambazo bado hazijatumika,” amesema.

Kwa mujibu wa Dk Mwinyi, uwekezaji unaofanywa ndani ya ATCL una mchango mkubwa katika kukuza nchi na kuiunganisha kikanda na kimataifa.

Licha ya kukua kwa uchumi, Dk Mwinyi amesema bado kuna changamoto zinazowakabili wasafirishaji wa bidhaa nje ya nchi na kwamba, zinapaswa kutatuliwa.

Ameitaka Wizara ya Uchukuzi kuisimamia bodi ya ATCL kuhakikisha ndege zilizonunuliwa zinakuwa na tija iliyotarajiwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Profesa Godius Kahyarara amesema hiyo ni ndege ya nane kupokewa katika utawala wa awamu ya sita.

Amesema ndege hiyo ina uwezo wa kutembea saa 14 hadi 24 bila kutua, na imegharamiwa na Serikali kwa zaidi ya Sh300 bilioni.

Amesema baada ya ndege hiyo, ATCL inakuwa ya kwanza katika ushoroba wa kati, hivyo inachochea matumizi makubwa ya bandari na reli na kuongeza uchumi wa Taifa.

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kuongezeka kwa ndege za aina hiyo na kufikia tatu kunapunguza changamoto ya kukosa safari pindi ndege moja inapoharibika.

Amesema ndege hiyo inafanya shirika hilo kuwa na ndege 16.

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Zanzibar, Dk Khalid Mohamed Salum amesema Serikali inaendelea kufanya maboresho ya miundombinu ikiwamo upanuzi na ujenzi wa viwanja vya ndege Unguja na Pemba.

Ndege hiyo ilipaswa kupokewa Agosti 19, 2024 katika uwanja huo lakini ilishindikana kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutokana na hali mbaya ya hewa nchini Marekani.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading