Dk Mpango: Mapambano mabadiliko ya tabia nchi yawe jumuishi

Dk Mpango: Mapambano mabadiliko ya tabia nchi yawe jumuishi

Arusha. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amesema ni muhimu kuwa na usawa katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, huku akieleza Tanzania imeendelea kusisitiza ujumuishaji wa masuala ya jinsia na mabadiliko kupitia sera, programu na mikakati kwenye ngazi zote.

Dk Mpango amesema hayo leo Jumatatu, Septemba 2, 2024 jijini Arusha, alipofungua Jukwaa la 24 na mkutano wa 35 wa kamati ya kudumu ya fedha ya mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi (UNFCCC).

Amesema ni muhimu kufanywa jitihada za haraka za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ambayo athari zake zimejitokeza katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na usalama wa chakula, afya na ikolojia huku wanawake, vijana na watoto wakiathirika zaidi.

Dk Mpango amesema dunia inasubiri ripoti za tathmini na muktasari wa fedha za masuala ya hali ya hewa, ripoti ya maendeleo kuhusu Dola bilioni 100  za Marekani ili kufanikisha utekelezaji wa mkataba wa Paris kutoka kwa nchi zinazoendelea kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Amesema Tanzania inaendelea kukuza ujumuishaji wa kijinsia na mabadiliko ya tabianchi katika sera, programu na mikakati katika ngazi zote pamoja na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa vijana, wanawake na wenye ulemavu.

“Mabadiliko ya tabianchi athari zake kubwa ni kwenye mifumo ya ikolojia, usalama wa chakula na mifumo ya afya, kijamii ikiwemo usawa wa kijinsia. Mabadiliko ya tabia nchi na ukosefu wa usawa wa kijinsia ni masuala yanayohusiana,” amesema.

Dk Mpango amesema vitu muhimu vinavyoendelezwa ni pamoja na usawa wa kijinsia katika upatikanaji wa fursa za kiuchumi kwa wanawake na wanaume, kuunda mazingira ya kuruhusu wanawake kushiriki kikamilifu katika ngazi za uamuzi.

Nyingine ni usawa wa kijinsia katika upatikanaji wa elimu, matumizi ya teknolojia katika uwezeshaji wa wanawake, matumizi ya nishati safi ya kupikia katika maeneo ya mijini na vijijini.

“Kaulimbiu ya jukwaa hili inaonyesha fedha zinazozingatia usawa wa kijinsia hazitafikiwa bila mchakato wa uamuzi unaojumuisha, unaoendana na mahitaji na unaoshirikisha,” amefafanua.

Akitolea mfano hapa nchini, Dk Mpango amesema athari kubwa za mabadiliko ya tabianchi zilizoathiri maeneo mbalimbali nchini ni pamoja na mafuriko, ukame, kuenea kwa majani vamizi na maporomoko ya udongo.

Amesema Desemba 2023 kutokana na mvua kubwa ilisababisha maporomoko ya tope, miti na mawe wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara na kusababisha vifo vya watu 89, majeruhi 139 na watu zaidi ya 1,500 kuathirika na tukio hilo.

Kuhusu nishati mbadala, amesema Tanzania imechukua hatua madhubuti kuongeza uzalishaji wa nishati mbadala kutoka vyanzo vinavyotumika sasa, ikiwemo umeme wa maji na kuwa imepanga kuzalisha megawati 950 kutoka nishati ya jua, upepo na mbadala mwingine.

“Tanzania imeweka lengo la kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya mijini na vijijini kutoka asilimia 86 na 67.7 mwaka 2020 hadi asilimia 100 ifikapo mwaka 2030,” amesema.

Kuhusu uchafuzi wa hewa unaotokana na matumizi ya kuni na mkaa, amesema Tanzania imeipa kipaumbele ajenda ya nishati safi ya kupikia na wanashirikiana na wadau wa maendeleo.

“Lengo letu ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wanapika kwa kutumia nishati safi kutoka asilimia saba ya sasa,” amesema.

Kwa upande wake, mshauri mwandamizi wa mabadiliko ya tabia nchi katika Kamisheni za Umoja wa Ulaya (EU), Apollonia Miola amesema mkutano huo unaongozwa na kaulimbiu isemayo; ‘kuongeza kasi katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia ufadhili unaozingatia jinsia’ na umekutanisha washiriki kutoka nchi 80 duniani.

Amesema lengo la Kamati ya Kudumu ya Fedha (SCF) ni kuangalia masuala yanayohusiana na mifumo ya kifedha na fedha za masuala ya hali ya hewa, ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, (Muungano na Mazingira), Dk Ashatu Kijaji amesema mvua za el nino ziliharibu shughuli za kijamii, kiuchumi na kusababisha vifo, huku kimbunga Hidaya kikiharibu nyumba, mbiundombinu katika baadhi ya maeneo.

“Tanzania imejizatiti kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kupitia mipango mbalimbali, tumepitisha sera na mipango mikakati, ikiwemo Sera ya Mazingira ya Taifa ya mwaka 2021, mpango wa kitaifa wa mazingira wa muda mrefu wa mikataba ya mkakati (2022-2032),” amesema.

Dk Ashatu amesema Tanzania inashirikiana na wadau wa maendeleo katika maeneo manane, ikiwemo  kukuza teknolojia za kupikia safi na nishati safi, kutekeleza mbinu za usimamizi wa taka endelevu katika miji mikubwa na kudhibiti aina za mimea vamizi katika mfumo ikolojia wa Serengeti-Ngorongoro.

Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba, amesema katika vikao vya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ajenda ya mabadiliko ya mabadiliko ya tabia nchi wameipa kipaumbele sambamba na masuala ya jinsia.

“Tutahakikisha masuala haya yanapewa kipaumbele na tuna uhakika kuwa hili litatuwezesha kuhakikisha kuwa rasilimali zote zitakazokusanywa zitatumika kwa uangalifu ili kufikia malengo,” amesema.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania Declares End of Marburg Virus Disease Outbreak

Tanzania today declared the end of Marburg virus disease outbreak after recording no new cases over 42 days since the death of the last confirmed case on 28 January 2025.

The outbreak, in which two confirmed and eight probable cases were recorded (all deceased), was the second the country has experienced. Both this outbreak, which was declared on 20 January 2025, and the one in 2023 occurred in the north-eastern Kagera region.

In response to the latest outbreak, Tanzania’s health authorities set up coordination and response systems, with support from World Health Organization (WHO) and partners, at the national and regional levels and reinforced control measures to swiftly detect cases, enhance clinical care, infection prevention as well as strengthen collaboration with communities to raise awareness and help curb further spread of the virus.

Growing expertise in public health emergency response in the African region has been crucial in mounting effective outbreak control measures. Drawing on experience from the response to the 2023 Marburg virus disease outbreak, WHO worked closely with Tanzanian health authorities to rapidly scale up key measures such as disease surveillance and trained more than 1000 frontline health workers in contact tracing, clinical care and public health risk communication. The Organization also delivered over five tonnes of essential medical supplies and equipment.

“The dedication of frontline health workers and the efforts of the national authorities and our partners have paid off,” said Dr Charles Sagoe-Moses, WHO Representative in Tanzania. “While the outbreak has been declared over, we remain vigilant to respond swiftly if any cases are detected and are supporting ongoing efforts to provide psychosocial care to families affected by the outbreak.”

Building on the momentum during the acute phase of the outbreak response, measures have been put in place to reinforce the capacity of local health facilities to respond to potential future outbreaks. WHO and partners are procuring additional laboratory supplies and other equipment for disease detection and surveillance and other critical services.

Marburg virus disease is highly virulent and causes haemorrhagic fever. It belongs to the same family as the virus that causes Ebola virus disease. Illness caused by Marburg virus begins abruptly. Patients present with high fever, severe headache and severe malaise. They may develop severe haemorrhagic symptoms within seven days.

In the African region, previous outbreaks and sporadic cases have been reported in Angola, the Democratic Republic of the Congo, Ghana, Kenya, Equatorial Guinea, Rwanda, South Africa and Uganda.

Source: allafrica.com

Continue Reading