Dakika saba za Kamala Harris Makumbusho ya Taifa

Dakika saba za Kamala Harris Makumbusho ya Taifa

Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Haris ametembelea Makumbusho ya Taifa leo Alhamisi Machi 30, 2023 na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya mabomu yaliyolipuka kwenye balozi za Marekani nchini Tanzania na Kenya mwaka 1998.

Kamala ametembelea mnara huo wa kumbukumbu ambao upo katika Makumbusho ya Taifa ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu nchini Tanzania.

Kabla ya kuwasili kwake, ulinzi uliimarishwa kwenye eneo hilo kukiwa na watu wachache walioshuhudia tukio hilo wakiwemo maofisa wa ubalozi wa Marekani.

Saa 9: 34 alasiri Kamala aliwasili katika viwanja vya Makumbusho na kupokelewa na waliokuwa na wafanyakazi wa ubalozi wa Marekani wakati mlipuko unatokea wakiongozwa na aliyekuwa balozi Charles Stith.

Baada ya kusalimiana na wafanyakazi hao wa zamani wa ubalozi moja kwa moja Kamala alielekea eneo ulipo mnara na kuweka shada la maua kisha kuwaombea kwa dakika moja kabla ya kuondoka.

Kamala ambaye aliwasili nchini jana saa 5:05 usiku, leo alianza kwa mazungumzo na mwenyeji wake Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu jijini Dar es Salaam.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

Karume faults lease of Zanzibar Islets
Tanzania Foreign Investment News
Investment News Editor

Karume faults lease of Zanzibar Islets

Diplomat Ali Karume has faulted the decision by the revolutionary government of Zanzibar to lease the islets that surround the islands of Unguja and Pemba to private developers saying it was absolutely not in Zanzibar’s national interests.Continue Reading