Dakika saba za Kamala Harris Makumbusho ya Taifa

Dakika saba za Kamala Harris Makumbusho ya Taifa

Dar es Salaam. Makamu wa Rais wa Marekani, Kamala Haris ametembelea Makumbusho ya Taifa leo Alhamisi Machi 30, 2023 na kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya mabomu yaliyolipuka kwenye balozi za Marekani nchini Tanzania na Kenya mwaka 1998.

Kamala ametembelea mnara huo wa kumbukumbu ambao upo katika Makumbusho ya Taifa ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu nchini Tanzania.

Kabla ya kuwasili kwake, ulinzi uliimarishwa kwenye eneo hilo kukiwa na watu wachache walioshuhudia tukio hilo wakiwemo maofisa wa ubalozi wa Marekani.

Saa 9: 34 alasiri Kamala aliwasili katika viwanja vya Makumbusho na kupokelewa na waliokuwa na wafanyakazi wa ubalozi wa Marekani wakati mlipuko unatokea wakiongozwa na aliyekuwa balozi Charles Stith.

Baada ya kusalimiana na wafanyakazi hao wa zamani wa ubalozi moja kwa moja Kamala alielekea eneo ulipo mnara na kuweka shada la maua kisha kuwaombea kwa dakika moja kabla ya kuondoka.

Kamala ambaye aliwasili nchini jana saa 5:05 usiku, leo alianza kwa mazungumzo na mwenyeji wake Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu jijini Dar es Salaam.

Source: mwananchi.co.tz

Original Media Source

Share this news

Facebook
Twitter
LinkedIn
WhatsApp

This Year's Most Read News Stories

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns
Tanzania Foreign Investment News
Chief Editor

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns

European Union Bans Air Tanzania Over Safety Concerns

Kampala — The European Commission added Air Tanzania to the EU Air Safety List, banning the airline from operating within European Union airspace. This decision follows the denial of Air Tanzania’s Third Country Operator (TCO) authorization by the European Union Aviation Safety Agency (EASA), citing significant safety deficiencies.

The EU Air Safety List includes airlines that fail to meet international safety standards. Commissioner Tzitzikostas emphasized the importance of passenger safety, stating: “The decision to include Air Tanzania in the EU Air Safety List underscores our unwavering commitment to ensuring the highest safety standards. We strongly urge Air Tanzania to take swift action to address these safety issues. The Commission has offered its assistance to Tanzanian authorities to enhance safety performance and achieve compliance with international aviation standards.”

Air Tanzania joins several African airlines banned from EU airspace, including carriers from Angola, the Democratic Republic of Congo, Sudan, and Kenya. Notable names include Congo Airways, Sudan Airways, and Kenyan carriers Silverstone Air Services and Skyward Express. The ban reflects the EU’s strict approach to aviation safety worldwide.

Source: allafrica.com

Continue Reading